SIMULIZI ZA MAPENZI

SIMULIZI FUPI ,,,LOVE STORY

Kijana mmoja alitokea kumpenda sana dada mmoja ijapokuwa dada huyo alikuwa akimtolea nje mara kwa mara lakini kijana hakukata tamaa, akiendelea kurusha ndoano huku akiamini siku moja atafanikiwa.Siku moja dada huyo akiwa yupo nyumbani aliamua kumpigia simu huyu kaka na kumtaka aje nyumbani kwake, yule kijana alifurahi na kuhisi sasa ombi lake limekubaliwa. 

Akiwa nyumbani kwake dada huyo , alikuwa amevalia kanga moja laini, kutokana na hali ya hewa ya joto la Dar es salaam.Kwa upande wa yule kijana alikuwa amefurahi sana na haraka alijiandaa na kuanza safari kuelekea kwa huyu dada, njia ni kaka huyu alikuwa akijiuliza maswali mengi, huku akiwa haamini kama yule dada amemuita nyumbani kwake. Alipofika, alibisha hodi na yuel dada akafungua mlango huku akionyesha tabasamu pana katika paji la uso wake. 

Kaka huyu aliingia ndani huku kijasho kikimteremka mithili ya mtu aliyekuwa anakimbia. Dada huyu alimkaribisha vizuri, yule kaka aliomba maji ya kunywa huku muda wote akimtizama kwa umakini dada huyu mrembo, aliyeumbika kila idara na ile kanga nyepesi aliyovaa ilikuwa ikionyesha umbo zuri la dada huyu ambaye waswahili huwa wanasema, mtoto kajaaliwa (mashalaah) Kaka alikuwa akivuta pumzi kwa haraka haraka, na kusema "Nimefurahi sana, umenikaribisha nyumbani kwako ni pazuri sana." Yule dada alitabasamu na kusema "Asante sana, nimefurahi pia umeitikia wito wangu, samahani kwa usumbufu wangu".
Yule kaka alitabasamu huku akijisogeza sogeza "Hakuna tatizo, usijali kabisa, mimi nipo kwa ajili yako, naimani sasa nina...." Kabla hajamilizia kuongea yule dada alimshika mikono yake miwili huku akimtizama machoni, kwa macho yake malegevu, mithili ya mtu aliyekula kungu "Samahani kaka, mimi nimekuita hapa kuna jambo nataka unishauri, nataka kujua ni zawadi gani nzuri unaweza kumpatia mwanaume unayempenda" Kaka yule alikuwa akitetemeka na kusema "Chochote tu, zawadi ni zawadi, alimradi kuwe na mapenzi ya kweli" Dada yule alitabasamu na kusema "Ni kweli, mapenzi ya kweli ndiyo jambo la msingi, nitampenda maisha yangu yote" Kaka yule akauliza "Utampenda? Nani huyo"
.
 Yule dada alitabasamu tena na kusema "Samahani, rafiki nilikuwa sijakuambia, wiki ijayo nafunga ndoa na mpenzi wangu wa muda mrefu ambaye nampenda sana, na pia nilikuita ili nikupe kadi ya harusi, nitafurahi kukuona, kwani wewe ni rafiki yangu pia" Yule kaka alibaki amepigwa na butwaa, "Ati, nini unaolewa, daaah, jamani, kwahiyo." Alinyanyuka na kuondoka bila ya kuaga huku akimuacha yule dada anamuita ili ampatie kadi bila ya mafanikio.
SIYO KILA UNACHOKIWAZA MOYONI MWAKO KITATOKEA KAMA UNAVYOTAKA. KWAHIYO NI VYEMA KUJIANDAA KUKUBALIWA AU KUKATALIWA

 

FACEBOOK

“"Reshmail Manyama want to be your friend.'confirm' 'ignore' ulikuwa ni ujumbe ambao macho yangu yalikutana nao nilipofungua mtandao wa kijamii wa ‘facebook’,sikumbuki kama nilijifikiria mara mbili kwani niliona ni jambo la kawaida sana kukutana na 'notifications’ kama hizo,na mara zote neno confirm(kubali) lilipata fursa ya kutumika.hivyohivyo hata kwa Reshmail nilifanya hivyo."You and reshmail are now friends" ndio ujumbe ulionisindikiza baada ya kukubali ombi lile kutoka kwa Reshmail.
                             *   *  * * *
Ni kijana mtanashati niliyebahatika kukutana nae pale chuo kikuu cha mtakatifu Augustine Mwanza,alijipenda kuanzia ndani ya chumba chake hadi mwili wake,ilikuwa ni nadra sana kumfumania akiwa amevaa nguo aliyoivaa jana,bila kumnyima haki yake nasema alikuwa anapendeza kila siku,macho yangu ya kipelelezi na kamera zangu za kipaparazi kamwe hazikufanikiwa kumjua aliyekuwa ubavu wa pili wa bwana huyu yaani 'MPENZI'. Ukipenda waweza kuniita kimbelembele lakini ukiniita hivyo basi majina hayo yatakuwa mengi pale chuoni kwani wengi walikuwa na shauku kubwa ya kujua siri hiyo na kamwe hawakufanikiwa.
Binadamu hatuna dogo watu washaanza kusema eti huenda jamaa ana matatizo makubwa tu mwilini mwake ndio maana yuko peke yake licha ya kushobokewa na wasichana warembo, mh! mimi sikuwa mmoja wao lakin nilijiuliza pia kulikoni??
    Makala mbovu zilizokuwa zinaandikwa na gazeti la chuo lililojulikana kama ‘Saut voice’ ndo zilinizonivuta zaidi kutaka na mimi siku moja kuandika katika gazeti hilo lililokosa mvuto siku za hivi karibuni makala nzuri itakayorudisha heshima ya gazeti hilo.Taratibu nilijenga mazoea na hatimaye nikafanikiwa kumzoea "THE MOST WANTED" ucheshi wangu ndio uliomvutia zaidi kupenda kuwa karibu nami pamoja na mchezo wa mpira wa miguu kwani wote tulikuwa mashabiki wakubwa,haukupita mwezi mzima nikawa nina uwezo wa kuanza kazi yangu,ni mimi na Adam Michael kwenye meza moja chumban kwangu ananipa hadithi yake ya maisha yaliyomfanya awe kama alivyo.
"Aah!! jamani Reshmail..." alianza Adam,yangu masikio na macho nikaanza kusikiliza kwa makini.
                     **        **          **



    Hadi anafika mwaka wa pili kimasomo chuoni mtakatifu Augustine Mwanza kitivo cha sheria Adam aliitumia simu yake ya mkononi kwa ajili ya kupiga,kutuma ujumbe (sms) na kupokea ni hayo tu na kwa upande wa pili alipenda sana kucheza michezo ya simu (game) ya kwenye simu.
    Alikuwa ni Hughorito Hamada ama maarufu kama 'HUHA'.hakuwa tu rafiki yake adam bali pia alikuwa ni mshirika wake wa chumba (room mate) na pia walisoma darasa moja la sheria pale chuoni,ni huyu aliyemuingiza Adam katika ulimwengu ambao hatausahau kamwe,tabia yake ya kupenda kuazima simu ya Adam aina ya Nokia Express music kwa dhumuni la kuchat katika mtandao maarufu wa kijamii wa ‘facebook’ ndio ilimshawish Adam naye kuanza kujiuliza kulikoni hasahasa alipokuwa anamwona Huha akicheka mwenyewe kila anapokuwa anachat,"Mh! we jamaa yangu chizi kweli yaani unacheka na watu usiowaona" Adam alimkebehi Huha alipokuwa anacheka na simu yake punde tu baada ya kuanza kuchat
"Kwani we ukiwa unaota unaongea huwa kuna watu mbele yako?" Huha alijibu mashambulizi na Adam akabaki kimya na taulo yake kiunoni akaenda bafuni kuoga.
"Mwanangu nimekuunga na wewe namba yako ya siri ni..,.." hata kabla Huha hajamaliza adam akamkatisha "Nini? huo upumbavu wako sitafanya kamwe bro" ..."Hv kwan inakuwaje huo upuuzi" Adam akajikuta anauliza baada ya kuwa amevaa nguo zake "Hii kitu inaitwa FACEBOOK,yan adam ukijiunga wewe hutoki na utakuwa nayo bize kweli" Adam alisikiliza kwa makin japo alijidai kufanya dharau machon,Huha hakujali aliendelea kutoa somo had Adam akapata mwanga,"Mh. Sidhan kama itanivutia bt i wil try". Alijisemea adam wakat anachukua simu yake.
                              ****
Tabia ya Adam ilikuwa imebadilika ghafla ni Adam na facebook,facebook na yeye,iwe barabaran,club,lecture room,hostel yani kasoro mskitini tu ndio Adam aliweza kuhfadh simu yake.Sio Huha wala rafiki yake yeyote aliyejua nini zaid ya facebuk kimemuathiri adam wa watu.Hakumuazima tena Huha simu,hakutaka mazoea na wasichana ni yeye na simu yake tu!! "Adam mbona washkaji wanalalamika eti wanakuomba urafiki facebook unachomoa? siku moja Huha aliamua kumuuliza Adam baada ya kuona tabia yake imekuwa ya ajabu mno kupindukia."Sitaki that's all". Ndio jibu fup alilopewa.kisha adam akajiondokea.Huha akabaki ameduwaa asijue la kufanya,mara ghafla adam akarudi tena "Huha naomba ukamwambie Halima simtaki,usiniulize kwa nini mwambie SIMTAKI!" adam alimwambia Huha kana kwamba alimfumania huyo halima.
Mpenz msomaj Halima alikuwa binti matata pale chuon kwa kipind kile,Adam ndo alipata fursa ya kuangukia penz lake,penz lao chuo kizima walifahamu,gari ya Halima ilikuwa kama ya Adam..chumba cha Cha Halima kilipambwa picha na kad za Adam lait na Adam angekuwa anakaa peke yake basi hata yeye chumba chake kingekuwa had na nguo za ndan za Halima pamoja na pedi bas tu alikuwa anakaa na Huha.
Huha alibak mdomo waz akijiuliza ni Adam au kivuli chake kinaongea.Alikuwa Adam sio kivuli.....

Ubize aliokuwa nao mheshimiwa mbunge ulimkosesha raha mkewe bi.Gaudensia Ogunde,hakuipata haki yake ndoa kwa takribani mwezi mmoja sasa,mume alikuwa anachelewa kurudi na akirudi anakuwa amechoka sana kutokana na majukumu mazito ya kiserikali,na ikitokea siku akathubutu kujaribu kutoa huduma basi alikuwa hamridhish mkewe,taratibu mama akajaribu kuzoea lakini kuna wakat uvumilivu ulikuwa unamshnda,nyumba nzima alikuwa akiish yeye,mtoto wake wa kike na msaidiz wa kazi (House girl)."Mwanangu ni siku ya tatu baba yako halali nyumbani,najisikia mpweke sana kulala mwenyewe" bi.Gaudensia alimweleza mwanae kwa unyonge "Pole sana mamii hata mi sipend hyo tabia ya baba,leo nakuja kulala na wewe mama" alijibu yule binti mwenye miaka 17 akiwa ndio kwanza amemaliza kidato cha nne.Mama hakujibu kitu badala yake alimkumbatia mwanae kwa sekunde kadhaa kisha akamwachia huku machozi yakimlengalenga.
Majira ya saa tatu usiku mama na mwana walikuwa kitandan wote wakiwa na night dress,kitanda kilikuwa kikubwa lakin umbali wao ulikuwa karibu mno,mapigo ya moyo ya mama yalikuwa juu sana,jasho lilikuwa likimtoka mtoto kwa kasi air condition iliyokuwa inapuliza haikuwa na maana tena mama na mwana walijikuta katika hisia nzito sana za mahaba,sio mimi wala wewe tunaojua walipoanzia.
                               ******  
    Reshmail Mtoto wa mwisho na pekee wa kike kati ya watoto wanne wa mbunge wa jimbo la Kinondoni Mheshimiwa Msuruli Haruna,hakupata kujua shida katika maisha yake na urembo aliojaliwa pia hakuufaham kwa sababu hakuwepo wa kumwambia kuwa yeye ni mrembo,kuta na fensi ya sen'gen'ge iliyozunguka mji wao haikumruhusu kutoka nje hovyo hovyo,tofauti na siku ya kwenda msikitini Resh alilazimika kusubiri hadi alipofikisha miaka kumi na nne alipojiunga na kidato cha kwanza katika shule ya st.marry's international ndio alipata wasaa wa kujumuika na wananch wengne wa Tanzania na nchi za jirani,elimu yote ya darasa la kwanza hadi la saba aliipatia katika jumba la kifahari la baba yake.
Mazoea ya kuish maisha ya peke yake peke yake yalimtesa sana Resh kiasi kwamba hadi anamaliza kidato cha nne aliweza kuwa karibu kiurafiki na wanafunzi wachache na weng wao wakiwa wasichana tena watoto wa matajiri na vigogo mbalimbali wa serikali.Kampani kubwa ya Reshmail alikuwa ni mama yake mzazi,yalikuwa ni mazoea makubwa sana lakini yasiyoshangaza,mara nying walikuwa wanatembea pamoja huku wameshkana mikono huku wakifurah sana.
Kidato cha tano na sita katika shule ya Arusha international school ndio kwa mara wa kwanza ilimpeleka nje ya jiji la dar-es-salaam.
Resh alilia sana kutenganishwa na mama yake lakini hakuwa na jinsi ilimlazimu kuondoka,mama alishindwa kujizuia alilia kwa uchungu ambao mumewe hakuutambua maana yake. "Nitakuwa nakuja kukusalimia" bi Gaudensia alimnon'goneza mwanae wakati akipanda gari la baba yake kuelekea airport."Usiache mama".alijibu resh huku akimbusu mama yake shavuni.
Mwanzoni ilianza kama utani pale Adam alipokubali ombi la Reshmail kuwa marafiki,walikuwa wakiulizana mambo ya kawaida sana huku katika orodha ya marafiki wa Reshmail ni Adam peke yake alikuwa mwanaume,"Mbona una marafiki wachache au ndo umejiunga facebook?" adam alimuuliza reshmail katika moja ya 'chatings' zao "No ni uamuzi 2 iam nt interested with boys i wonder why you?" "May be iam someone special,who knows" alijibu Adam, "You might be" alijibu reshmail."Yani hadi mchumba wako hujamweka kwenye orodha?" "Sina huyo mchumba unayemdhania" "What? msichana mrembo kama wewe,au hizi picha sio zako?" "Ni zangu kwani ukiwa mrembo lazima uwe na mpenzi?"alisisitiza Resh kisha akaendelea "Naona we upo kwenye uhusiano,hongera" aliandika Resh,ni wanaume wachache sana akiulizwa na msichana mrembo kama ana mpenzi halafu akubali na hata kwa Adam ilikuwa hivyo,"Mh! nimejiandikia tu,mi sina mtu nani wa kunipenda mimi?". Alidanganya Adam,"What! hawakioni hcho kifua chako au na wewe hiyo sio picha yako?"
"Ni ya kwangu,Reshmail una utani wewe"
"Sina utani nimekipenda sana"
 "Haya asante,kwako wewe sina la kusema unavutia kila upande"
"Asante lakini we zaidi,Adam naingia kuoga nisindikize basi"
"Wee,si umeniambia mnakaa wanne sa wenzako watanielewaje?" alijibu Adam huku akiamini kwamba hayo yote yanayotokea ni utani mtupu.
"Kwa hyo ningekuwa peke yangu ungenisindikiza?" "Yeah? ningekusindikiza lakini ningefumba macho" alitania Adam.
"Vp ninatisha sana au,yan hadi ufumbe macho sawa tu" alilalamika Resh,"Natania mrembo lakin si unajua tena nitajiumiza"
"Ok! tuachane na hayo,simu yako inauwezo wa kufungua e-mail?"
"Inafungua tena sasa hivi nilikuwa ninasoma emails" alijibu adam.
"Ndio hii Adamboy@Yahoo.com?" "Yap ndio hyo" "Fungua baada ya dakika tano uone zawadi yako"
Jasho jembamba huku mikono ikitetemeka,macho yakiwa yamemtoka Adam hakuamin anachokiona kwenye simu yake.
                         ****
Mazoea ya Reshmail na mama yake kujigeuza mtu na mpenzi wake yaliwaathiri sana wawili hawa,mara kwa mara Bi.Gaudensia alifanya safari za ghafla kwenda Arusha kufaidi penzi la jinsia moja kutoka kwa mwanae mpendwa,raha alizozipata hakuwa na muda wa kumfikiria mumewe tena,tabia hii ilimuathri sana Reshmail pale shulen,licha ya urembo wake hakuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanaume yeyote pale shulen bila kujalisha uwezo wao kifedha wala sura na utanashati wao,aliwaona hawana maana kwake zaid ya mama maskin Resh hakujua tamtam ya penzi la wanaume.
Alikuwa ni Eveline,binti aliyekuwa anaish chumba kimoja na Resh,akiwa ni mzaliwa wa hapohapo Arusha anayezijua kona zote za Arusha,pombe,club na ngono ndio walikuwa marafiki zake wakubwa,alikuwa mchesh na mzuri wa sura lakin kubwa na jema zaid alikuwa mwelevu sana darasani katika mchipuo wa "H.G.E" pamoja na reshmail,ni jambo hilo lililowaweka wawil hawa karibu.Mshipa wa aibu haukuwepo kichwani mwa Eveline,na kama ulikuwemo basi haukuwa unafanya kazi vizuri,picha alizozipenda ni za uchi na movie za ngono ndio alizokuwa anaangalia tena kwa anapandisha sauti hadi vyumba vingne wanasikia.Ni huyu Eveline aliyemwingiza Resh katika maswali ya kwa nini,na inakuwaje "Mbona nikifanya na mama silii kama hao? alijiuliza Reshmail akiwa ndan ya kitanda chake huku pemben Eveline akiwa bize na laptop yake akiangalia filamu ya ngono "Ponographics" ......."Nitamuuliza Eve siku moja lakin nitaanzaje?" alijiuliza
Mara zote walizokuwa wakipeana burudani kitandani au sakafuni Mama yake alikuwa ndiye mwalimu wa kila kitu,yeye ndio alijua wapi amguse,wapi amtekenye ili mradi kuleta raha na wote kuridhika.Lakini safari yake ya mara ya tano kwenda Arusha kwa mpenzi wake huyo haramu ndipo alipokutana na mshangao.Reshmail yuleyule aliyekuwa zuzu kitandani akihudumiwa kila kitu na mama yake ili aridhike alikuwa moto wa kuotea mbali.Alimgalagaza mama yake ipasavyo kwa ku2mia vidole vya mikono yake pamoja na ulimi wake kutambaa kila kona ya sehemu husika .Mama reshmail (Bi.Gaudensia) alijikuta akiongea lugha ambazo hazipo katika ulimwengu huu.Hoteli ya Tanzanite chumba namba 18 kiligeuka kama pepo kwa wawili hawa,mama alikuwa analia sana machozi ya furaha na mbaya na ya kuchekesha eti akasema "Darling UTANIOA eeh!" jaman raha zikizidi sijui kilimfurahisha nini mama huyu kwa mwanae.Kulipokucha Bi.Gaude alimrudisha mwanae shuleni kama alivyokuwa amemwombea ruhusa."Mama huyu ni rafiki yangu anaitwa Eveline,Eve huyu ni mama yangu mpenzi" Reshmail aliwatambulisha baada ya kumkuta Eveline pale ofisini."Shkamoo mama" "Marahaba" alijibu mama bila kumwangalia usoni Eveline ambaye hakujali hilo sana "Punguza wivu sweet" Resh alimnon'goneza mama yake,ambae alitabasamu "Nakupenda mwanangu" "Nakupenda mama" waliagana mama akaondoka kurudi kwa gogo lake (Mumewe) huko dar.

                              * * * * *

"Ukitaka kuujua utamu wa ngoma ingia ucheze" ndio jibu alilopewa Resh baada ya siku moja kumuuliza eti anafaidika nini kuangalia filamu za ngono,mwanzoni alikuwa akiangalia kwa aibu san lakini baada ya kufanikiwa kuzihamishia kwenye "Laptop" yake mambo yakawa ya kawaida japo kwa kujificha,mara nying alijifunika shuka na kuweka earphone masikion kisha burudani.Ni mchezo huohuo mchafu Resh aliuiga na kwenda kujaribisha kwa 'mpenzi mama'."Hivi Eveline kuna raha kufanya au kuangalia peke yake inatosha?" "Haha haloooooo! unalo shosti,wenzio wakata viuno we wafurahia miguno looh!" Vidole vikiwa juu kama muimba taarabu Eve alimchambua Resh,"Mh! shoga si unifunze kuliko kunichambua?" alijitetea resh kwa saut ya chini,"Ulisema huna bwana weye sasa kulikoni ya nini haya tuachie sie wamama wa shughuli" "Eve we ni rafiki yangu ngoja nikwambie ukweli.....mimi nampenda mtu ambaye sijui kama ananipenda au tutaendana"
"Vipi hujawah kumwona au?"
"Nimemwona kwenye picha"
"He! una makubwa we mrembo au ndo yule kwenye kompyuta yako?"
"Haswaa ndio yeye"
"Hata kama hujamuona yule pale dume la ukweli,kile kifua usimlete kwangu nitakuibia," alitania Eve.kisha akaendelea "Najua hujui jinsi gani utampata niachie hyo kazi mimi ndan ya wiki moja nakukabidh mali yako." "Asante evely asante sana" alishukuru
* * * *

Ilikuwa ni picha ya binti mrembo sana akiwa amejifunga taulo kwa chini huku chuchu zikiwa nje,"Ndio natoka kuoga,vp nimetakata?" iliambatana na ujumbe ule.Adamu alibaki mdomo wazi,mh!! hivi inawezekana akawa Reshmail dah! alishangaa Adam.Akiwa bado mdomo wazi email nyingne iliingia ilikuwa picha tena,safari hii ilionyesha sehemu yote ya nyuma "NIPAKE MAFUTA" ndio ujumbe uliobeba picha hyo.Bila kujua muda gani na kwa misingi ipi Adam alikuta pensi laini ikiwa imembana,kuja kugundua chanzo ni sehemu flani kwenye mwili
wake ilikuwa imeongezeka ukubwa (Ha ha ha ha wanaume dhaifu sana.

Majukumu ya hapa na pale yalikuwa yamembana sana Bi.Gaudensia ambaye ni mama yake na Reshmail,pia uwepo wa mumewe katika himaya yake ilimnyima kabisa raha mama huyu na alikuwa anakosa nafasi ya kwenda Arusha mara kwa mara kufurah na mwanaye jambo ambalo lilimtesa kwa takribani mwezi mmoja na nusu.Vipindi vya bunge vilipoanza tena ndio hapo nafasi ilipatikana tena,kwa muda wote ambao alikuwa jijin dar-es-salaam Bi.Gaude alikuwa akiwasiliana na mwanae karibia kila siku kwa njia ya simu,alijua ni jinsi gan hata mwanae huyo alivyo'm-mis' hvyo aliamua kumfanyia 'surprise' ya kwenda huko Arusha shuleni bila kumwambia ili kuinogesha furaha yao ambayo ilikuwa inakamilika kitandan."Baba Resh mie kesho naenda kumsabah mwanetu,lakin hata simwambii nataka ashtukie tu,mama huyo"
"Atashangaa kweli,msalimie sana mwambie nitakuja kumsalimia bunge likimalizika" "Haya,zimefika"

* * * * * *

Penzi la ku-chat katika mtandao wa facebook lilikuwa limemchanganya sana Reshmail wa watu,Adam hakuwa nyuma kumpa maneno matamu ya hapa na pale ambayo kamwe alikuwa hajawah kuyasikia masikion mwake,Eve mwenyewe alimshangaa huyu shoga yake lakin hakuwa nyuma kumpiga tafu katika mpango mzima wa kumtia Adam majaribuni ndio maana alimshawish Resh kupga picha mbaya ambazo mwanaume yeyote akiziangalia lazima ajiulize mara mbilimbili kuhusu urembo asilia wa binti yule.
"Mi nipo peke yangu siku hizi rum-mate wangu ameenda kwao babake anaumwa" "Don't tell me kuwa unalala mwenyewe"
"Nitafanyaje sasa na wewe upo mbali?"
"ooh! my ghosh! assume nipo hapo"
"Aah,nitajiumiza bure tu mpenzi wangu"
"Anarudi lini kwani?"
"Mh! amesema atatumia kama wiki mbili hivi,njoo basi unipe 'kampan' kiaina"
Yalikuwa mazungumzo kwa njia ya simu kati ya Adam na Reshmail yaliyokatishwa na na mlio wa 'low battery' katika simu ya Reshmail "Baby boy tutaongea kesho,pole sana na ninakupenda sana" alimaliza Resh na simu ikawa imezima.
"Eveline nataka kwenda Mwanza" asubuh ya siku iliyofuata Resh alimwambia Eve.
"He! makubwa haya,imekuwaje kwan shoga" aliduwaa.
"Mi sijui lakin nataka kwenda tu" alisema Reshmail "Haya lini wataka kwenda?"
"Hata kesho mi naenda tu" "Mh! sikuwez haya jiandae kutoroka coz ruhusa hapa kupata sahau" "Vyovyote poa ninachotaka ni kuondoka na kwenda Mwanza that's all" alijibu kijasiri Resh hali iliyomduwaza eveline.

                          * * * * * *

"Reshmail hayupo? mbona jana alikuwa hapa ofisin?" mwalimu wa zamu alikuwa anamuuliza mwanafunzi aliyeagizwa kumuita Reshmail baada ya mama yake kuwa amefika,"Hata mi sijui mwalimu"
"Hapana sio jambo la kawaida reshmail kutokuwa mazingira ya shule tena jumatatu! hebu mwambie time-keeper agonge kengere mara moja" aliamrisha mwalimu.
                               ******
Hakuwa hata na chembe ya utani Reshmail wa watu,majira ya saa moja asubuhi tayari alikuwa kwenye gari la KIMOTCO ninalotoka Arusha kwenda Musoma kwa kupitia Mugumu Serengeti,kitu kinachoitwa hofu moyoni hakikuwepo hata kwa mbali,ndani ya kipochi chake kidogo alikuwa na pesa taslimu za kitanzania shiling laki mbili zikisindikizwa na kadi ya viza ya CRDB iliyokuwa na uwezo wa kutoa shiling laki tano kwa siku mara nne yaani milioni mbili zilikuwa zimehfadhiwa katika acount yake ya akiba.Mamaa wa shughuli (Eveline) alikuwa pembeni ya Reshmail,hofu kwake haikuwepo wala hakuiwaza tayari alikuwa mzoefu wa mambo hayo."Eveline yani akili ndo inakuja sasa hivi eti kwa nini tusingepanda ndege dah! gari linaenda taratibu hilo jaman" alilalama Reshmail kwa wananch wa kawaida waliomsikia walidhani ni mashauzi na majigambo ya watoto wa kike
"Mh? shoga ulivyokuwa na hamu ungekumbuka hayo,tutafika weye acha papara"
Gari lilizidi kuchanja mbuga za ngorongoro kwa kasi ya kawaida hadi majira ya saa saba tairi chakavu za gari hili zilikuwa tayari kwenye mbuga za Serengeti,Resh alikuwa macho anatazama safari inavyokwenda huku akihesabu masaa yanavyokatika kwa kasi huku mwisho wa safari ukiwa haufiki.Eve yeye alikuwa ameuchapa usingzi huku akiwa amejifunika uso wake kwa kofia yake nyeusi ambayo vumbi ilikuwa imeibadili rangi yake na kuwa ya ugoro.(Brown).
"Eve Eve Eve,amka uone wewe" Resh alikuwa anamwamsha kwa fujo."Angalia hii sms imeingia sasa hv" "Resh mazako kaja unatafutwa uko wap?" jasho jembamba likaanza kumtoka Resh lakin Eve hakushtuka sana.Walikuwa wametumiwa ujumbe mfupi na mmoja wa viranja."Eve tumeisha tumeisha"

                             * * * * * * * *

Ulikuwa mshikemshke wa ghafla pale shuleni mwalimu aliamuru kila mmoja aje mstarini hata kama ni mgonjwa,viranja walitii amri na kuita wanafunzi wote kwa haraka hakuna hata mwanafunzi mmoja aliyebaki ndani ya bweni.
Wakiwa hawajui nini kinachoendelea mwalimu wa zamu aliyeitwa Mwl.Chipeta alikuwa mbele ya wanafunzi waliokuwa kimya kumsikiliza yeye.”Kabla sijatoa tangazo hili,ni nani anatambua mwanafunzi ambaye hayupo eneo hili? (Kimya)
"Nani anaumwa na amepewa ruhusa?" (Kimya)
"Kwa hyo wote mpo?" (Ndiooo)
"Haya mchepuo wa H.G.E wote pita mbele" aliamuru mwalimu Chipeta na kwa haraka wakaanza kujongea mbele."Mamaaaaa," ghafla kelele ilisikika kuna mwanafunzi aliyekuwa mgonjwa alikuwa ameanguka chini kwa sababu ya kizunguzungu.Ustaarabu ukatoweka pale ghafla kila mwanafunzi akawa anasema lake,mara hivi mara vile. Hata mwalimu Chipeta alitimua mbio kuelekea kwenye tukio.
Ni wakat huohuo Joyce ambaye alikuwa kiranja alipata mwanya wa kutuma ujumbe kwa Reshmail kumpa taarifa.
                              *****
Roho ilikuwa inamdunda Reshmail kwa kasi sana,aliamin kila kitu kitakuwa wazi na atafukuzwa shule,"Eve watanielewaje wazazi mie mh! nimerokoroga" alijisemea Reshmail.
"Upo na steringi lazima tushinde haka kavita kadogo" Eve alimpa moyo wa ujasiri Resh,"Naomba hiyo simu si ina salio kidogo"
"Imo elfu tatu"Alijibu huku akimpa simu Eve.
"Sihitaji zote hizo natumia shiling 60 tu hapa"Alijibu kwa jeuri Eve huku akionekana kujiamini zaidi.
"Sasa hyo 60 itafanya nini shogangu au umesema elfu sitini?"Alitania Resh na wote wakajikuta wanacheka.
"Dakika tano nyingi majibu mazuri yatakuja,chukua simu yako ikiingia meseji uisome mi nalala bibie tuliza roho yako hii sio movie ya kihindi eti stering anauwawa,hili picha la kichina stering anachomwa kisu bado anapona" alimaliza Eve na kushusha kofia yake ikafunika macho.
Ni kama alivyosema dakika tano zilikuwa nyingi sana ujumbe kujibiwa
"Na ufanye kweli mi narekebisha mambo nyie tanueni kwa raha zenu na pia kuhusu yule wa H.G.L vipi?" ulisomeka ujumbe."Mungu wangu amakweli Eve steringi jamani yaani kirahisi hvyo" alijisemea Resh kwa sauti ya chini akidhani Eve amelala tayari "Futa sms ya huyo mjnga nitamalizana nae" kwa saut ya kivivu Eve alimwambia Resh.
                                    ****
Ndege ya Precion Air ilikuwa inaondoka kutoka Musoma kwenda Dar-es-salaam kupitia Mwanza majira ya saa kumi na moja wakati basi la KIMOTCO lilifika saa kumi na nusu jioni,Resh aliona akipanda gari anaweza kuchelewa kwa Adam Mwanza japo hata umbali wa Musoma kwenda Mwanza hakuufahamu."Resh ndege ya wapi tunapata sasa hv jaman" Eve alimuuliza Resh wakiwa ndani ya 'Teksi’ kutokea stendi kuu ya Musoma maeneo ya Bweri."Tunajaribu steringi wangu"
"Haya!! utamu na uchungu wa mapenzi mwachie aliyeyabeba" alitoa fumbo Eveline.
"Dereva dereva zuia kidogo tafadhali" ghafla Resh alimwomba dreva naye bila hiana akazikanyaga breki bila kuuliza kulikoni. Mbio mbio Resh akashuka akaanza kutimua mbio kurudi nyuma huku akiwa peku viatu ameacha garini Eve,Dereva na wananchi wengine wakabaki kumshangaa.
Mwalimu Chipeta aliongoza zoezi zima la kumshughulikia mwanafunzi aliyeanguka pale mstarini,shule ya Arusha international ilisifika sana kwa kujali afya za wanafunzi hivyo tukio lile lilisababisha Mwalimu Chipeta kumsahau kabisa Bi.Gaudencia mama yake Reshmail na kwenda kushughulika ipasavyo kwenye lile tukio,aliyekuwa ameanguka alikuwa Naomi Holela mwanafunzi aliyekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kifua na pale kilikuwa kimembana hasa kutokana na baridi iliyokuwepo nje. Gari ya shule ilifika haraka Mwalimu Chipeta na viranja wawili pamoja na 'matron' walimsindikiza Naomi hospitali. Akiwa ndani gari Mwalimu Chipeta alisikia simu yake ikitoa mlio wa kupokea ujumbe mwanzoni alipuuzia kutokana na ubize uliokuwa ukimkabili lakini punde alitoa simu yake na kufungua ujumbe ulioingia
"Niaje ticha mi Wa ukweli nipo na Resh mbali kimtindo kama vipi rekebisha mambo huko mi nikija nakuletea geto yule Amina wa H.K.L,niandalie tu mapene yangu" uso wake ulisahau matatizo yote yaliyokuwa mbele yake,ni muda mrefu sasa tangu Mwalimu Chipeta muhitimu wa shahada ya elimu ya fasihi andishi katika chuo kikuu cha Dodoma alikuwa amemfukuzia binti mrembo wa kawaida tu Amina bila mafanikio tegemeo lake alikuwa ni Eve au Wa ukweli kama walivyomzoea,bila kupoteza muda Chipeta alifungua sehemu ya ku'forwad' meseji na akaituma kwa Mwalimu.Madege ambaye wote lao lilikuwa moja,alikuwa ni mwalimu Madege aliyeijibu ule ujumbe na kuulizia kuhusu yeye na mpango wa kumpata binti wa H.G.L.
"Samahani wewe ndio mama yake na Reshmail "Mwalimu Madege aliuliza baada ya Bi. Gaude kuingia katika ofisi ya makamu mwalimu wa zamu .
"Ndio ni mimi baba"
"Kwanza samahan sana kwa usumbufu uliojitokeza"
"Usijali na mimi niwape pole kwa  matatizo yaliyojitokeza hapa"
"Tunashukuru ndio mambo ya shule haya,eeh! mama nimepokea ujumbe sasa hivi kwamba mwanao yupo katika mbuga za Serengeti ambapo wanafunzi watano waliofanya vizuri walipelekwa kufanya utalii wa siku tano" alidanganya mwalimu Madege.
"Jaman huyu mtoto mbona hakuniambia?... baba yake atafurahi sana akisikia maendeleo ya mwanae"mama Resh alijieleza kwa furaha iliyozidi wasiwasi aliokuwa nao.
"Tuliwashtukiza hawakuwa na taarifa hata wao wameshangaa mno" aliendelea kupanga maneno huku akichorachora mezani kwa kutumia karamu isiyokuwa na wino.
Moyo wa mama Reshmail uliridhika japo mwili ulikuwa na kinyongo kwa kukosa haki yake. Ilimbidi siku hiyo hiyo afunge safari kurudi jijini Dar na zawadi alizokuwa amemletea mwanae zikiwa mikononi mwake.

                          * * * * * *

A.T.M ya N.B.C aliyoiona maeneo ya Nyasho ilimkumbusha kuwa kadi yake ni 'VISA' inafanya kazi mashine ya A.T.M ya benki yoyote bila kujali macho ya watu alitimua mbio pekupeku hadi kwenye mashine ambapo kwa bahati nzuri hapakuwa na foleni na mtandao ulikuwepo "You can withdraw up to 1000000 with your A.T.M card daily N.B.C WE CARE" kijitangazo kwenye kioo cha mashne kiliibua tabasamu la Reshmail,na bila ajizi akabonyeza chaguo la kutoa laki tano kwa mikupuo miwili na kutimiza kiasi cha milioni moja, kisha kwa mwendo wa mbio kama alivyoingia akatoka akisindikizwa na miluzi ya wauza mitumba wa Nyasho ambayo kwake haikuwa na madhara hata chembe
"Samahani safari yenu imeahirishwa tafadhali hadi kesho asubuhi!" sauti nyororo ya mwanadada wa mapokezi aliyehusika na masuala ya Booking aliwaeleza mwanaume mmoja aliyekuwa na mpenzi wake wakitegemea kusafiri muda mfupi ujao kwenda Mwanza.
Sura zao zilizokuwa na furaha zililegea na kuwa kama watakavyokuwa pindi wakipata wajukuu,"Haiwezekani huu ni upumbavu tena ujinga ujinga ujinga,yani safari yangu inahairishwa ghafla kama vile safari za baiskeli,hapana sipo tayari nas...."
"shhhhh!!" kwa ishara ya kidole kimoja kuziba mdomo alinyamazishwa yule baba aliyetaka kuugeuza ukumbi ule uwanja wa mapambano na matusi. Kwa ishara nyingine yule dada akamwita akasogea pale alipo akamnon'goneza "Unawaona wale wasichana wawili,mmoja kimada wa mtoto wa raisi mwingne mtoto wa kamanda wa jeshi ni simu kutoka ikulu,kwa usalama wako acha kelele" alimwambia huku akimwelekezea walipo Resh na Eve. Bila kuhoji huku uoga ukimtawala hadhi yake ikashuka haraka haraka akamvuta mkewe wakaondoka wakawapisha kwa mbali Resh na Eve kama vile wanatema cheche za moto.
                           * * * * *
Ni kweli nafasi zilikuwa zimejaa lakini pesa iliongea nafasi ya mtu mwingine wakapewa wao tena harakaharaka,huku mtendaji wa jambo hilo akiweka shilingi laki mbili na nusu kibindoni. Huku Resh na Eve wakipata nafasi katika ndege ya Precision Air kiulaini,kwa mara ya kwanza Eve anapanda ndege "Mh! ushoga nao raha wakati mwingine” alijisemea wakati muhudumu wa ndani ya ndege akitoa maelekezo madogomadogo.
Ilikuwa kama safari ya kutoka Kimara Dar kwenda Mbagala,tayari walikuwa jiji la Mwanza
"Eve rushwa tamu wewe,naamini haitaisha ona sasa tupo Mwanza tayari" Resh alimwambia Eve wakati wanasafisha macho yao wajue nini cha kufanya baada ya kushuka kutoka kwenye ndege.
"Hoteli yenu ni nzuri?" Eve alimuuliza muhusika aliyekuwa ndani ya kigari kidogo kilichoandikwa Millenium Hotels kilichokuwa hapo kwa lengo la kutafuta wateja wanaotua na ndege uwanjani hapo,"Ni nzuri sana hautajuta kuwa pale.”
"Mh! haya,Resh twende giza linaingia" Eve alimwita Resh wakajitoma ndani ya gari na safari ikaanza.
"Darling umetoka kwenye michezo tayari pole mpenzi" ulikuwa ujumbe mfupi kutoka kwa Adam kuja kwa Resh,tabasamu pana likameza mdomo wake looh! lilikuwa tabasamu lililoelezea furaha ya moyo.
Adam alituma ujumbe huo akijua Resh yupo shuleni tena ilikuwa siku ya michezo ambayo Resh alipenda kushiriki hasahasa mpira wa kikapu.
"Mamaaaaa!!"Resh alipiga kelele ghafla gari ikayumba huku na huko,dereva akajaribu kwa uwezo wake wote kuirudisha barabarani "Paaaa!!" mlio mkubwa ukasikika.
    *******************
Adam alipokea ujumbe kutoka kwa Reshmail akiwa maeneo ya kijiweni barabara ya lami kuelekea chuo kikuu cha mtakatifu Augustino,kupitia shule ya wasichana ya Ngaza.Adam alikuwa pamoja na rafiki yake (Huha) katika pikipiki ya rafiki yao aliyekuwa amewaazimisha wazungukiezungukie maeneo.
"Huha hebu endesha twende hapo Nyegezi kona kuna mtu nataka kuonana naye mara moja" Adam alimwomba Huha.
"Tayari Halima ametuma meseji mwambie hatuna mafuta atufate na gari yake bwana" Alitania Huha huku akianza kuiondoa pikipiki taratibu
"Ungejua hata usingesema wewe twende ukajionee maajabu ya mwaka" alijibu Adamu huku pikipiki ikizidi kushika kasi.
Ndani ya dakika tano tayari walikuwa Nyegezi kona ambapo Huha alipaki pembezoni kidogo na barabara iendayo stendi kuu ya Nyegezi jijini Mwanza,Adam alielekea dukani kununua vocha,na Huha akasogea pembeni kidogo aweze kuvuta sigara yake.

                                     ***
Dereva akiwa mwingi wa mawazo yake binafsi yasiyomuhusu Reshmail wala Eve na hata kama yangekuwa yanawahusu ule haukuwa muda muafaka wa kuwaambia.Macho ya Reshmail yalikuwa yamekutana na bango kubwa lililoandikwa "KARIBU CHUO KIKUU CHA MTAKATIFU AUGUSTINO" kwa hamu kubwa aliyokuwa nayo ya kumwona Adam ambaye alikuwa pia mwanafunzi ndani ya chuo hicho ndio sababu kuu ya kujikuta akipiga kelele kwa nguvu hali iliyomshtua dereva kutoka katika mawazo mazito na kujikuta akiyumbisha gari huku na huko hadi ilipokutana na pikipiki iliyokuwa imepakiwa pembezoni mwa barabara na kuirusha umbali ambao si wa kutisha sana,iligeuka vurumai madereva wa teksi na bodaboda za pikipiki walikuwa wakali sana hawakutaka kusikia la mtu,wengine hasira za kukosa abiria tangu waingie kijiweni asubuhi walizihamishia katika tukio hilo. Usingekuwa upole wa yule dereva basi mawe waliyobeba wananchi yangeigeuza ile gari kuwa mkweche. Eveline alitelemka garini kwenda kumsaidia dereva kujitetea lakini Reshmail uoga ulimtawala akawa amejibana kwenye viti vya nyuma vya ile gari huku akitetemeka. "Mh! Adam hawezi kukosa mwenyeji maeneo haya ngoja nijaribu kumpigia,ah! hii safari imetawaliwa na mikosi dah!" aliwaza Resh huku akichukua simu yake kutoka katika kipochi chake.
Lakini kelele zilizokuwa pale aliamini hawezi kusikilizana vizuri na upande wa pili,taratibu huku akitetemeka alifungua mlango akashuka na kuanza kutembea kuelekea pahali ambapo kidogo pametulia. Zaidi ya asilimia 50 ya wananchi wenye hasira eneo lile wakageuza vichwa vyao kuangalia kazi ya Mungu ilivyotendeka vyema katika mwili wa Reshmail,badala ya kumpigia kelele dereva,miluzi mikali ikiongozwa na dereva mkongwe wa teksi eneo lile ndugu Sanya Bonda ikahamia kwa Reshmail,Resh akajifanya kama hasikii vile "Ilikuwa haki ya dereva kupotea njia jamani" Bonda alisema kwa sauti ya juu na kugeuza hasira za watu kuwa vicheko. Resh taratibu akaufikia mti mdogo mbali na eneo la tukio akabonyeza namba za Adam. Simu iliita muda mrefu bila kupokelewa. Alipopiga mara ya pili simu ilipokelewa."Helow Resh subiri nisogee pembeni nakupigia kuna tatizo limenipata" alijibiwa na Adam katika simu.
"Hata mi....." kabla hajamalizia kauli yake Reshmail simu ilikatwa akiwa bado anaduwaa kama dakika mbili pembeni yake alizengea kijana mmoja ambaye Resh hakutaka hata kumwangalia machoni,alijua ni walewale waliokuwa wakipiga miluzi na kumwita majina waliyotaka. Resh taratibu akajisogeza pemben."Vipi dada mbona wanikimbia au mi nanuka halafu we mrembo haya basi umebarikiwa sana najua unataka kusifiwa" aliongea yule kijana lakini Resh hakujibu.Simu yake ya mkononi iliyokuwa katika mfumo wa kimya(Silence mode) ilikuwa inatoa mwanga kuashiria aidha kuna ujumbe umeingia au kuna simu inaingia,lakini kwa jinsi alivyoandamwa na yule kaka kwa maneno hata hakuweza kugundua.
Baada ya dakika kadhaa akaondoka yule kaka ndipo kuangalia simu akagundua ilikuwa imeita mpaka imekata na hakuwa mwingine bali ni Adam alikuwa amepiga,harakaharaka akapiga tena. Ulikuwa mshangao wa hali ya juu sana Reshmail hakuamini alipomwona yule kijana aliyekuwa ametokea pale dakika chache zilizopita kuelekea kwenye zile vurugu ndio anapokea simu."Resh mbona nimekupigia hupokei mamaa" alimshuhudia yule kaka akiongea kwenye simu huku akirejea lile eneo kukwepa kelele,kama ilivyo kwa mtu aliyenaswa na umeme Reshmail alikuwa ametulia tuli na simu sikioni huku yule kaka akizidi kulikaribia eneo lile “Reshmail mbona huongei!!” aliendelea kuuliza bila kupata majibu."Adam" alijitutumua Resh na kutamka akiwa jirani naye kabisa,bila kujua yule kijana akaangusha simu yake hakuamini msichana aliyetoka kuongea nae dakika kadhaa ndio Reshmail wa Arusha.
                               ***
Vurumai lilisawazishwa haraka sana Adam na Huha ndio waliokuwa wamiliki wa ile pikipiki iliyogongwa na gari waliyokuwemo akina Reshmail."Jamani huyu hapa ni dada yangu,ndio alikuwa amenipigia simu tuonane hapa naomba haya mtuachie sisi" Adam aliuambia umati ule ambao hasira zao zilikuwa zimeanza kupoa na haraka walimwelewa wakaacha kumzonga dereva.Reshmail bila kupoteza muda akamwongoza Adam wakaingia garini akampa pesa taslimu shilingi laki tatu kwa ajiri ya matengenezo ya ile pikipiki naye Adam akamkabidhi Huha kisha akajumuika na Eve pamoja na Reshmail katika gari,huku Reshmail akiwaacha watu hoi kwa uzuri wake wa asilia ambao hata Adam alikuwa amechachawa nao na kukubaliana na ukweli kwamba picha zilizotumwa zilikuwa za Resh kweli.

                            ***
Bi Gaudensia alifika Dar-es-salaam majira ya saa tatu usiku,bado alikuwa hajaridhika kumaliza siku yake bila kuongea na mwanae,hivyo punde tu baada ya kuingia chumbani mwake aliamua kujaribu kupiga namba za simu za Reshmail ambazo zilikuwa hazipatikani siku nzima. Furaha aliyoipata ilikuwa haisimuliki,pale simu ilipoita upande wa pili"Mh! kalala nini huyu?" alijiuliza simu ilivyoita kwa muda mrefu bila kupokelewa,lakini mara ikapokelewa
 "Helow! samahani Reshmail amelala" sauti ya kiume ilijibu baada ya kupokea kisha simu ikakatwa na kuzimwa. Mama Resh hakuamini kuwa amesikia sauti ya kiume katika simu ya mwanae alidhani amekosea namba lakini alipohakikisha zilikuwa zenyewe,wivu mkali ukamshika,akajaribu kupiga mara nyingi lakini bado hali ilikuwa ileile simu ilikuwa imezimwa usingizi ulipaa,alitokwa na jasho,hisia mbaya zikamvuruga na kufanya kichwa chake kiume sana,mama huyu alikuwa amejisahau kabisa kuwa Reshmail ni mwanae wa kumzaa, alizurura kama mtu anayetafuta kitu ambacho amesahau alipokiweka pale chumbani,alitamani kupiga kelele lakini aliamini hazitasaidia kitu.
                                 ***
Reshmail akiwa usingizini Adam pembeni yake,yeye(Resh) alikuwa hoi kwa uchovu wa safari na misukosuko yote waliyopitia,na alipomaliza kuoga tu na kupata chakula alisinzia,hata simu yake ilipoita hakuisikia hata kidogo na hata angeisikia asingeweza kunyanyuka kupokea "Resh ni kipetito anapiga" Adam alimuuliza Resh aliyekuwa hoi kitandani."Ah! ni rafiki yangu mwambie nimelala" alijibu kwa taabu akiwa hata hajui anachokiongea. Naye Adam bila kugundua kwamba Resh hajui anachokisema na ile namba ni ya mama yake Resh alipokea na kuzungumza

Kitendo cha Adam kumkuta Reshmail akiwa bado ni bikra kilimzuzua sana,mapenzi yake kwa Halima yalipungua sana na kuisha kabisa hatimaye. Siku tatu mfululizo walizotumia pale Millenium Hotel zilitosha kuvunjilia mbali penzi la Adam na Halima na kujenga penzi imara kati ya Adam na Reshmail.
"Mwezi wa pili uje ujitambulishe nyumbani Adam yaani siwezi kusubiri kwa kweli nakupenda Adam wewe ni mwanaume wangu wa kwanza na ninakuahidi nitajitunza kwa ajili yako" Reshmail alikuwa anamsisitiza Adam siku alipokuwa amewasindikiza uwanja wa ndege tayari kwa wawili hawa kurejea Arusha shuleni.
"Mama anapiga! Eve" Resh alimwambia Eve pale simu yake ilivyoita."He! usiniambie huyo ndio mama,sasa mbona ulikubali niongee nae usiku ule? aliduwaa Adam.
"Eti! uliongea nae? Yesu wangu!" alishtuka Resh lakini Eve akamshauri azime simu kwanza mengineyo watajua mbele kwa mbele naye Resh akatii amri hiyo haraka akaizima simu bila kupokea Resh kwa kiasi kukuwa alikuwa amemzoea na kumwamini Eve.
Adam,Resh,na Eve waliagana kama watu waliofahamia na kukaa pamoja siku nyingi sana,Resh alimkumbatia Resh alimkumbatia Adam kwa muda mrefu hadi Eve alipowatenganisha na kuambiana Kwaheri.
***
Ilikuwa imebaki miezi minne wafanye mtihani wa kumaliza kidato cha tano,Resh akiwa amekolea katika penzi la Adam na kusahau kuhusu
Mama yake ambaye alikuwa amezuiwa na mwanaye huyo kwenda pale shuleni kumsalimia kwa madai kwamba yeye(Reshmail) anataka ajikite zaidi katika masomo. Reshmail kwa maksudi akabadilisha namba yake ya simu ili mama yake asiweze kumpata mara kwa mara badala yake muda mwingi akawa anawasiliana na Adam.
Mwezi wa pili ilikuwa ni likizo ya mwezi mzima kwa wanafunzi wa kidato cha tano na cha sita na pia wakati huohuo wanafunzi wa chuo kikuu cha mtakatifu Augustino huwa katika mapumziko mafupi baada ya kumaliza muhula(Semister) ya kwanza. Kwa Reshmail ulikuwa wakati muafaka wa kumtambulisha Adam kwa wazazi wake jambo ambalo aliamini lingesaidia kupunguza makali ya mama yake. Tangu akiwa mtoto kamwe hakuwahi kuwakwaza wazazi wake kwa sababu ya wanaume hata siku moja hivyo alitegemea hawatampinga.
Ilikuwa siku ya furaha kubwa sana kwa Bi. Gaudencia na familia yote kwa ujumla kumwona tena Reshmail nyumbani baada ya miezi mingi tena akiwa mwingi wa furaha. Lakini tofauti na mama yake alivyofikiria kwamba mwanae huyo anafurahia kurudi katika ulimwengu wao wa mapenzi haramu yeye(Reshmail) alikuwa anafuraha ya kumtambulisha Adam ndani ya siku chache.
Kwa kujua wazi kabisa mama yake atachukizwa na maamuzi yake hayo,Reshmail aliamua kulifikisha hilo mbele ya Mzee. Manyama ambaye ni baba yake.
"Kwa sababu ni uchumba tu na hakupeleki popote hamna tatizo hata kidogo,mlete tu mwanangu mlete una maamuzi mazuri sana sio kama wasichana wengine wanafanya upuuzi kimyakimya mambo yanapokuwa mabaya ndio wanasema" alijibu mzee.Manyama huku akimshika mwanae huyo shavuni,Resh akatabasamu na kumkumbatia baba yake "I love you dad(Nakupenda baba)" Resh akamwambia kwa furaha tele mzazi wake huyo,huku moyoni akijiaminisha kwamba hapatakuwa na kikwazo tena kwa mama yake kwani baba ndiye kichwa cha familia.
Baada ya siku tano Adam aliwasili ndani ya kasri la mbunge huyu.Alikuwa anaogopa na hakuamini kama angepokelewa na kama angepokelewa alijua yatakuwa mapokezi mabaya sana kwani katika simulizi mbalimbali anazozisikia kwa watu zilimwonyesha kwamba ni vigumu sana kwa wazazi kumwelewa mtoto wa kike linapokuja suala la kumtambulisha mwanaume kama mchumba wake.
"Da Rosemary nina hofu mie" Adam alimwambia dada yake kipenzi waliyekuwa wameongozana naye "Acha uoga bro mbona hata sisi babu yetu alikuwa chifu? kwani chifu na mbunge nani zaidi" alitania Rosemary kumwondoa hofu kaka yake.Mapokezi waliyoyapata kutokea kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo yaliwashangaza mno waliwakuta watu wa kuwapokea na kwenda nao kwenye gari mbili walizokuja nazo,waliwafikisha hadi getini ambapo kina dada wawili kwa heshima kabisa waliwaongoza hadi sehemu maalum iliyoandaliwa kwa ajili yao,japo usoni waliuficha mshangao wao lakini moyoni uliwajaa tele.Adam akiwa ndani ya suti nyeusi wanazotumia wanasheria katika shughuli zao na Rosemary aliyevaa suti pia walielekezwa wapi walipo wazazi wa Reshmail wakaenda kutoa salamu zao,ilikuwa ni hafla kubwa sana ndugu,jamaa na marafiki wapatao miamoja walikuwa wamealikwa na mheshimiwa huyu. Ilikuwa kama harusi kwa asiyejua lakini ulikuwa utambulisho tu.
Bwana na bibi Manyama walipendeza kwelikweli na walikuwa na kila haki ya kuitwa wakwe na Adam. Furaha ya Bi. Gaudencia ilificha chuki aliyokuwa nayo moyoni dhidi ya Adam kwa kumchukua mwanae ambaye ndio alikuwa anampa raha zote za dunia.
Hadi hafla inafikia tamati majira ya saa mbili usiku kila mtu alikuwa amepata furaha kubwa sana,wabunge na madiwani ambao ni marafiki wa karibu wa Manyama walitoa zawadi nyingi kwa wawili hawa huku babu yake Reshmail akitoa mawaidha yenye maana kubwa sana katika maisha waliyotarajia kuyaishi Reshmail na Adam siku za usoni.
Mzee Manyama kwa ombi la mwanae aliwasiliana na wazazi wa Adam kuwa muda wa mapumziko ya siku tano alizobakiza Adam amalizie katika familia yake,hapakuwa na kinyongo wala kipingamizi chochote walikubali kwa moyo mmoja na Adam akaendelea kuishi pale huku dada yake akirejea Mwanza kwa usafiri wa ndege ambao gharama zote zilikuwa juu ya mheshimiwa Manyama. Kila alipowasiliana na wazazi wake Adam hakusita kuelezea upendo wa kipekee anaoupata kutoka familia ya Reshmail hata wao walifarijika sana.
                      ***
Ilikuwa jumapili moja tulivu sana baada ya kutoka kanisani familia yote akiwemo pia Adam,baba yake Reshmail aliongozana na mwanae kwenda mjini kwa lengo kuu la kuonana na walimu mbalimbali wa masomo ya ziada(Tution) watakaompendeza Reshmail basi waweze kumfundishia nyumbani.
Huku nyuma alibaki Adam pamoja na mkwewe (Mama Reshmail) baada ya kupata kifungua kinywa Adam alimwaga mkwewe kuwa anaenda kuzungukazunguka bustanini "Tena nilitaka nikwambie leo unataka uondoke hata bustanini hujawahi kufika,afadhali nenda mwanangu" alijibu mama Reshmail.
     Ulikuwa mpango kabambe uliosukwa na Bi.      Gaudencia,kwa dhumuni kuu la kumwondolea mamlaka Adam ya kuwa na Reshmail. Kwa kuwatumia vijana kutoka katika ngome ya vigogo,ngome maalum iliyokuwa inatumiwa na watu wenye pesa zao kwa ajili ya kuwatenda vibaya watu wanaoonekana kuingilia mambo yao aidha kimapenzi au kibiashara.Alipoaga anaenda bustanini Gaudencia alitumia fursa hiyo kupiga simu kwa wanaume hao wa shoka ambao tayari alikiwa ameelewana nao bei.
"Ndani ya dakika tano tutakuwa hapo” ndio jibu lililotolewa upande wa pili
Bila kuongezea lolote Bi.Gaudencia alikata simu yake na kutoka nje.
"Babu kwa mama Veneranda si unapajua?" alitoa swali hlo Bi. Gaudencia kwenda kwa mlinzi wao wa getini.
"Ndio si yule mama anayesuka pale mbele"
”Hapo hapo haya haraka nenda kaniangalizie kama kuna foleni kubwa" aliamrisha Bi. Gaude na mlinzi akatii amri hiyo haraka haraka akaondoka katika lindo lake akaenda kutimiza amri ya bosi wake.
Baada ya dakika takribani kumi alirejea mlinzi yule "Yupo mmoja tu anamaliziwa" alileta taarifa hiyo kwa furaha.
"Haya mi ninatoka nimemwacha Adam ndani amelala akiamka mwambie nimetoka kidogo" alisema mama Reshmail huku akiondoka.
“sawa bosi nitamwambia”
Masaa mawili badae alirejea akiwa amesukwa tayari nywele zake,ni muda huohuo Reshmail na baba yake walikuwa wametoka mizungukoni,walimkuta Gaudencia anatokea ndani. "Babu Adam alivyoamka ameenda wapi? au bustanini?"Aliuliza Gaudencia na kuongezea "Maana nimegonga chumbani kwake kimya,hebu Reshmail ingia ukamwangalie ndani mwake humo huenda amelala bado" kwa mwendo wa maringo lakini harakaharaka Reshmail alijongea ndani.
"Babu unasema Adam hajatoka?" Resh aliuliza baada ya kurejea akiwa na hofu kidogo usoni.
"Hajatoka na mimi hapa sijatoka tangu mama alipoenda kusuka na kumwacha Adam amelala" alijieleza mlinzi yule jibu lililopokelewa kwa furaha na Bi.Gaudencia.
Jambo gumu zaidi kwa ambao hawakujua janja ya mama huyu ni kwamba simu ya Adam ilikuwa haipatikani hali hiyo ilileta wasiwasi sana,walisubiri huenda atarudi hadi jioni hali ilikuwa tete ndipo mzee Manyama alipoamua kupiga simu kituo cha polisi maeneo ya jirani kwa sababu alikuwa mbunge msako ulianza usiku huohuo.
        Siku tatu zilipita bila taarifa yoyote kutoka katika kituo cha polisi,Reshmail alikuwa amepooza sana kupita maelezo mara kwa mara alimpigia baba yake simu na kuuliza kulikoni lakini jibu bado lilikuwa lilelile kuwa hajapatikana.
"Mama niache tafadhali,tena niache nasema upuuzi wako siutaki tena niache!" alifoka Reshmail pale mama yake alivyomkuta amekaa sebuleni na kujaribu kumpapasa huku akimpa pole ya kupotelewa na Adam wake ghafla.
"Mwanangu usiwe na hasira kiasi hicho polisi watafanikisha upelelezi na watamrejesha Adam akiwa mzima wa afya" alibembeleza Bi. Gaudencia lakini Reshmail hakujibu kitu akajiondokea akiwa ameuvuta mdomo wake sana.
    Siku ya tano polisi waliopewa jukumu la kufanya upelelezi huo walirejea na taarifa yao huku wakiambatana na ushahidi. Zilikuwa nguo aliyokuwa amevaa Adam kwenda kanisani ikiwa na matundu sita ya risasi na ikiwa imetapakaa damu pote,suruali ilikuwa na matundu matatu ya risasi.
 "Hapana hawezi kuwa Adam hata kidogo nasema hawezi kuwa yeye" alifoka Manyama huku akiwa wimawima mbele ya mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai jiji la Dar-es-salaam Chacha Boniphace au maarufu kama Chacha B.
"Mheshimiwa lakini huu ni upelelezi wa awali tunaendelea zaidi na zaidi tutazidi kutoa taarifa kadri tunavyopata majibu mapya" alijieleza kwa utulivu bila wasiwasi kabisa jambo ambalo kidogo lilirejesha amani ya Manyama japo hofu tayari ilishaukumba moyo wake kwamba huenda Adam ameuwawa tena kikatili.
Ilikuwa ni shughuli pevu kwa Reshmail kuamini kile ambacho alikuwa anaelezwa na baba yake kwamba Adam anadhaniwa kuuwawa kwa risasi nane kisha mwili wake hauonekani. Bi. Gaudencia tayari alikuwa anaangua kilio kikubwa hata kabla maelezo hayajaisha ikawa kazi kwa mumewe kumbembeleza.
"Mke wangu Adam hajafa ila inadhaniwa pia upelelezi bado unaendelea jamani,ukilia hivyo unakuaribisha msiba mama watoto sawa" alibembeleza mzee Manyama huku amemkumbatia mkewe.
"Baba haiwezekani baba haiwezekani nguo za Adam zipatikane katika hali hiyo halafu mnasema hajafa,jamani Adam wangu wamemuua" alipiga mayowe Reshmail ikamlazimu mzee Manyama kufanya kazi mara mbili jambo ambalo lilimtoa jasho mzee huyu.
"Reshmail mwanangu,tulia hiyo siyo taarifa rasmi jamani ni majibu ya awali mbona mnanifanyia hivyo au mnataka nipate presha nife?" alijieleza Manyama huku akijifuta jasho kwa kutumia shati lake. Reshmail mbio mbio akaondoka pale sebuleni akaanza kuzipanda ngazi kuelekea chumbani kwake huku akilia,mzee Manyama nae huyo nyuma yake.
"Reshmail mwanangu,njoo malkia wangu,njoo mwanangu" aliyazungumza hayo huku akimkimbiza kwa nyuma. Wakati huo Bi. Gaudencia tayari alikuwa amenyamaza kimya kabisa,akijaribu kupikicha
macho yake.Reshmail hakusimama hadi chumbani kwake akajifungia,baba yake alibembeleza mpaka akachoka hakupata jibu zaidi ya kilio cha kwikwi kutoka ndani.
"Baba Resh twende chumbani mume wangu,twende utakaa hapa hadi saa ngapi cha msingi tumwombe Mungu asije akajidhuru mwanetu" Gaudencia alimnyanyua mumewe wakajikongoja kuelekea chumbani kwao,Manyama akiwa amelegea kabisa.
Asubuhi ya siku iliyofuata naibu waziri wa ulinzi na usalama,alifika na msafara wake wa magari matano kwa mbunge Manyama kuja kutoa pole ya kutokewa tukio hilo lenye utata kwa mwenzao. Shughuli ngumu iliyokuwa mbele yao ni jinsi gani watawaeleza wazazi wake Adam ambao hadi dakika hiyo waliamini Adam yupo salama na mwenye furaha kwa mchumba wake Reshmail,Manyama alimuomba waziri ashughulikie hilo suala na bila kupoteza muda alinyanyua simu yake ya mkononi na kutoa taarifa hiyo kwa mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai Mwanza pamoja na mawasiliano anayoweza kumpata baba yake Adam. Ilikuwa vigumu sana kwa baba Adam kuelewa anachoelezwa lakini kwa kadri ya uwezo wake na taaluma yake mkuu huyo alifanikiwa kumwelewesha ambapo baba yake Adam aliondoka akiwa na matumaini kwamba ipo siku Adam atapatikana.
Nyumba nzima ya kina Adam ilipooza sana dada yake Adam (Rosemary) alikuwa analia muda wote kwa uchungu hakuamini kwamba siku ile pale uwanja wa ndege alivyosindikizwa na familia nzima ya mhe.Manyama ndio ilikuwa mara ya mwisho kumwona kaka yake kipenzi(Adam).
Uongozi wa polisi uliifikisha taarifa hiyo pale chuoni ambao pia walipokea kwa simanzi kubwa.

"MAUAJI YA KUTISHA", ndivyo mandishi meusi kabisa kwenye magazeti mbalimbali yalisomeka,hali hiyo ilithibitisha kabisa kuwa Adam hayuko hai tena. Picha yake iliyoambatanishwa na habari hizo akiwa na mtoto wa mbunge iliteka na kuumiza mioyo ya watu wengi hasahasa vijana."Tumempoteza mwanasheria" ndilo neno la pamoja walilosema wasomi wa chuo kikuu cha mtakatifu Augustino Mwanza katika misa ya pamoja kumwombea mema Adam kama yupo hai au kumtakia pumziko jema la milele kama tayari Mungu ameichukua roho yake,kila uso ulikuwa na simanzi kubwa ilikuwa kama tamthilia.
Reshmail alikuwa kama zezeta,hamwelewi mtu yeyote,roho yake ilimwambia kwamba mama yake mzazi anahusika kwa namna moja au nyingine katika tukio hili lililojaa utata. Lakini ataanzia wapi kumweleza baba yake,atajisikiaje mzee Manyama akigundua kwamba mke na mtoto wake walikuwa katika ndoa haramu ya siri ndani ya nyumba yake."Hapana sitaki kuongeza tatizo juu ya tatizo nitasubiri liwalo na liwe,kama Mungu alimpanga Adam awe wangu naapa sitaolewa na mwingine kamwe,lakini kama hakuwa halali yangu basi ataletwa mwanaume duniani kwa ajili yangu tena"Alijipa ujasiri wa hali ya juu Reshmail huku akijipigapiga kifuani."Nitarejea shule na nitasoma tena kwa bidii sana,sitamwaza mwanaume yeyote tena alikuwa Adam na atabaki kuwa Adam hadi Mungu aamue tena" aliendelea kujipa matumaini."Bibi yangu aliniambia maneno ya mdomo huumba halisi,na nina uhakika ninachokiongea kwa mdomo wangu Mungu ataniumbia" aliendelea kuongea huku machozi yakifumba macho yake na kitambaa alichokuwa anatumia kujifuta kilikuwa kimelowana tayari kwa wingi wa machozi alikuwa kama yatima vile,Resh alikuwa akifungasha baadhi ya mizigo yake tayari kwa kurejea shuleni tena,tangu tukio la Adam kupotea hakuna aliyetegemea hata siku moja Resh atawaza kurudi tena shuleni kwani waziwazi akili yake ilionekana kuathirika kwa kiasi kikubwa kwa kumpoteza Adam katika mazingira yasiyoeleweka.
"Baba kesho narejea shule si unajua tayari shule imefunguliwa?" Reshmail alimkurupua mzazi wake huyo kutoka alipokaa kwa mshangao
"Umesema nini malkia wangu!" alihoji Manyama huku akiwa wima
"Narejea shule kesho" kwa msisitizo na tabasamu alijibu Reshmail. Mzee Manyama hakuamini kwani alikuwa akiwaza ni namna gani atamshawishi mwanae aweze tena kurejea shuleni baada ya matatizo yote yaliyojitokeza kwa mchumba wake Adam ambaye hadi wakati huo bado mwili wake ulikuwa haujapatikana wala taarifa yoyote zaidi ya nguo zikiwa na matundu ya risasi na damu."asante sana mwanangu nakupenda sana" mzee Manyama aliongea kwa furaha huku akimkumbatia mwanae.
     Tangu kupotea kwa Adam aliyehisiwa kuwa tayari amekufa kulipokelewa kwa hisia tofauti na wananchi huku asilimia kubwa ikiegemea upande wa imani potofu za kishirikina wakihusisha tukio hilo na utajiri alionao Mh. Manyama na uchaguzi uliokuwa mbele yake.
                        ****     *******
           "Wamemtoa mwanangu kafara ili waongeze utajiri,nilimwambia Adam aoe msukuma mwenzake ona sasa,watoto wa siku hizi wabishi wanajifanya wanajua sana na elimu yao inawadanganya" mama yake Adam alikuwa analaani vikali mbele ya mume wake wakiwa ndani ya nyumba yao maeneo ya Igoma kwa 'one-way'
"Usiseme hivyo mama Adam kumbuka sisi ni wakristu,tumwachie Mungu yeye ndio atajua nini cha kufanya" Babaye Adam alimtuliza mkewe huku akimgongagonga mgongoni kwa kutumia kiganja cha mkono wake wa kuume.
Mawasiliano baina ya familia hizi mbili ya Adam jijini Mwanza na ya Reshmail jijini Dar-es-salaam yalikuwa yamekatika licha ya baba yake Adam (mzee Michael) kutangaza kuwa kutoka moyoni mwake amesamehe yote yaliyotokea na anaamini ni mipango ya Mungu lakini kinyongo kilionekana dhahiri kwa matendo,upendo wa zamani haukuwepo tena jambo hilo lilimfadhaisha sana mzee Manyama kiasi cha kukondeana na kukosa umakini katika utendaji wake wa kazi jambo lililoishusha sana heshima yake kama mbunge aliyekuwa anaheshimika sana kuanzia bungeni hadi jimboni kwake,wapinzani walitumia fursa hiyo kumchafua hasahasa na kweli uchafu huo ukakubalika kwa wananchi kwa ujumla Manyama hakuwa na lake tena pale,wananchi walimpuuzia sana tofauti na zamani na hata hiyo miaka miwili iliyobaki wananchi waliiona kama ni mingi sana kuwa na kiongozi wa aina yake.
Kuliko fedheha yote hiyo Mh. Manyama kwa hiari yake mwenyewe alipitisha kura ya maoni ya wananchi kuhusu imani waliyonayo kwake kama mbunge wao. Asilimia 70 ya waliopiga kura walidai hawana imani naye huku asilimia kumi na nne tu ndio wakidai bado wana imani naye na kura zilizobaki zikiharibika,rasmi Manyama akawa ametolewa bungeni na katika uchaguzi mdogo uliofanyika akachaguliwa mbunge kutoka chama cha upinzani na maisha yakaendelea huku Mh.Manyama akiendelea na biashara zake mikoani.
                             * **
Adam akiwa pale bustanini alivamiwa ghafla na wanaume wawili wa shoka wakiwa na bunduki,ishara ya kidole mdomoni ilimfanya atulie tuli kisha wakamwonyesha ishara kwamba awafuate alifanya kama walivyotaka hadi kwenye gari iliyokuwa imepaki pembeni kidogo ya nyumba yao Adam alishangazwa sana na ukimya uliokuwepo hakuwepo mlinzi wala mama mkwe wake.Safari yao ilikwenda mpaka Iringa gari iliyokuwa na vioo vyeusi 'tinted' ilimzuia Adam kujua ni wapi alipo,gari ilizimishwa ndani ya jumba kubwa sana ambapo alipelekwa kwenye chumba kikubwa tu,hofu kubwa ilimtawala hakujua kwa nini yuko pale,hakupigwa wala kupewa bughudha yoyote,hali hiyo ilzidi kumshangaza "au ndio wachuna ngozi" alijiuliza Adam kwa hofu tele.
Hayo ndio masharti ambayo mama Reshmail alitoa kwa vijana aliowapa tenda hiyo ya kumtorosha Adam pale nyumbani. Shida yake haikuwa kumtesa Adam bali kumweka mbali na mwana (Reshmail) ambaye alikuwa amempagawisha ipasavyo katika mapenzi ya jinsia moja.Suala la pesa halikuwa tatizo hata kidogo alichohitaji ni kutimiziwa alichotaka. Mkataba wa miaka mitano ndio alioingia na watu hawa kukaa na Adam bila kumruhusu kutoka nje ya jingo.Bi Gaudencia aliamini kwamba kwa kutokomea Adam mbele ya uso wa Reshmail ilikuwa fursa nzuri ya kurudisha tena uhusiano wake na Reshmail ambao ulikuwa unaelekea kufa lakini kinyume chake alikuwa ameibua chuki kubwa baina yake na mwanae “heri  wote tukose kama ni hivyo” alijiapiza mama Reshmail baada ya kuona dalili za kumshawishi Reshmail hazipo tena
       Alikuwa ni Reshmail mwingine kabisa mkasa uliomkumba ulimbadilisha sana na kuitanua akili yake sana,Eveline naye alisikitishwa na yaliyomkumba shoga yake akajitahhdi sana kuwa karibu naye kumpa moyo huku akijiepusha sana kufanya vitendo ambavyo vitamkumbusha Resh jinsi alivyoweza kukutana na Adam. Ni katika kujiepusha na kumkera rafiki yake huyo kipenzi Eveline akajikuta amefuta picha za uchi na filamu za ngono katika kompyuta yake akawa si mtu wa kutoroka shule,hakuwa tena mtu wa wanaume na hatimaye akawa Eveline wa kuigwa na wanafunzi wenzake jambo hilo liliwaduwaza sana wanafunzi pale shuleni lakini ndio hivyo Eve alikuwa amekubali mabadiliko katika maisha yake. Juhudi zao katika masomo ziliendelea kuwaweka katika nafasi nzuri ya kufanya vizuri mtihani wao wa mwisho. Hawakuyazungumzia tena yaliyopita tena walijadili mapya na yanayowanufaisha "Eveline wewe ni kama dada yangu nakupenda sana"
"Nakupenda pia Reshmail umebadili maisha yangu moja kwa moja nina maisha mazuri sasa" alijibu Eva kwa upole huku akimwangalia Reshmail aliyekuwa anaishusha chandarua yake aweze kulala. Ni kweli walitokea kupendana wawili hawa.
"Hivi Resh una mpango bado wa kusomea uhasibu mi lazima niwe mhasibu"
"Mh! unavyojiaminisha utadhani tumefaulu tayari" alijibu Resh.
"He! mi najua sisi kufaulu kwetu sio swali ni jibu,swali ni je tunaenda chuo gani na kusomea nini." alijiaminisha Eveline.
"ok! nilidhani nitasomea uhasibu lakini kwa heshima ya Adam nitasomea sheria" alijibu Reshmail kwa furaha.
"Mh! na upole wako huo na mambo ya kutoa hukumu wapi na wapi? mwenzio naangalia ankara" alisema Eva.
"Wala hata siendi kuhukumiana naenda kwa heshima tu" alisisitiza Reshmail.
"Mh! haya mheshimiwa hakimu napenda kujitetea kama ifuatavyo" Eve alitania akifuatiwa na kicheko kikubwa kutoka kwa Reshmail.
                            * * *
Maisha yaliendelea vyema sana tu japo yalikuwa maisha ya mashaka Adam aliruhusiwa kuongea na kuuliza kila kitu kasoro swali moja tu "Kwa nini niko hapa?",ndio hakuruhusiwa kuliuliza hata kwa mbali,watu wote pale hawakuwa na ubaya nae hata kidogo,hawakumtesa,hakugombezwa wala hakufanya kazi,alipewa huduma zote za msingi,aliweza kutoka nje na kwenda bustanini lakini nje ya geti hakuruhusiwa. Tayari aliyazoea maisha haya lakini kumbukumbu ya jinsi alivyochukuliwa ndani ya jumba la wakweze bila kupata msaada wowote ule "Nani atakuwa nyuma ya haya yote mlinzi alikuwa wapi? Mama Resh je?" alijiuliza sana bila kupata wa kumpa jibu.
"Hivi unaitwa dada nani vile?" Adam alimuuliza dada mmoja ambaye kila baada ya siku tatu alikuja kufanya usafi katika chumba chake.
"Naitwa Beatrice Cosmas niite Bite" alijibu huku anafuta vioo kwa dirisha la chumba cha Adam.
"Una jina zuri wewe mh!"Alisanifu Adam.
"Asante wewe ni Adam eeh!" aliongezea yule binti huku akiwa ameacha shughuli yake aliyokuwa anafanya.
"Ndio mimi ni Adam! samahani nikuulize maswali machache"
"Uliza tu lakini sitakujibu sasa hivi"
"Kwa nini?"
"We uliza yote ndo nitakwambia kwa nini"
"Hivi hapa ni wapi? kwa nani? na kwa nini nipo hapa?"
"Ndio hayo matatu tu?...sawa nitakujibu kwa sharti dogo sana yaani"
"Sharti gani hilo mi nipo tayari"alitoa uhakika Adam bila hata kulijua sharti lenyewe.
"Sikia Adam sina haja ya kuzunguka zunguka nina mwaka wa pili hapa kitu kinaitwa mwanaume katika mwili wangu ni kama ndoto sasa ni wewe wa kutii kiu yangu na mimi nitajibu maswali yako" alijieleza Bite,jambo ambalio lilikuwa zito na la kumshangaza Adam.
"Mh! au ndo mtego tena kutoka kwa Reshmail? dah! ikiwa hivyo nitaaibika kweli mimi"Alijiwazia Adam kwa mashaka makubwa kabla ya kujibu.
"Basi utakuja kunijibu baadaye!" alisema Adam.
"Haya usiku na wewe jiandae" alijibu na kuaga Bite.
Hayawi hayawi mara yakawa usiku wa saa tatu,Bite tayari ndani ya chumba cha Adam ndani ya khanga moja peke yake.
"Haya nipe nikupe hakuna longolongo hapa" alizungumza Bite.
"Subiri taratibu basi,sikiliza" alianza kujitetea Adam wakati Bite anajisogeza kitandani,Adam alikuwa amechelewa tayari joto la Bite lilipenya katika mwili wake na kumchanganya hadi kujikuta akifanya kinyume na alivyotarajia kwamba atafanikiwa kutegua mtego wa Bite badala yake alikuwa ameshafanya mapenzi na Bite. Kwa Bite ulikuwa ushindi mkubwa sana kwani tangu aletwe hapo kuwa msaidizi wa kazi za ndani ya vyumba hakuwahi kutoka nje ya jengo hilo,sio kwamba alikuwa amefungwa hapana kila kitu kilikuwepo ndani kila siku pia alikuwa ameridhika kuwa hapo.
"Hapa ni Iringa,nimejibu swali lako la kwanza tuendelee tena nikujibu swali la pili na tatu" alisema Bite kwa shauku kubwa sana.
"Hapana Bite imetosha kwa leo sijisikii vizuri,siku nyingine basi sawa!" alidanganya Adam na Bite hakuwa mbishi akambusu Adam shavuni akajiondokea zake.
Ilimchukua takribani siku tano Bite kugundua kwamba tayari ameshika ujauzito jambo ambalo halikuruhusiwa katika jumba hilo na alipewa onyo kali wakati anaingia hapo. Kwa usalama wake na Adam alifikiria suala la kutoroka lakini haya yote aliyafanya baada ya kuongea na Adam na kumweleza hali halisi. Ni katika wasaa huo alimweleza Adam chanzo ambacho kinaweza kuwa kimemsababishia yeye kuwepo pale "Umemchukulia kigogo mpenzi wake,umemendea mtoto wa kizito au umemkataa kimapenzi mtu maarafu" hizo ndizo zilikuwa baadhi ya sababu alizoorodheshewa na Bite,lakini kwake yeye aliona hakuna hata moja inayomuhusu kwani wazazi wote wawili wa Reshmail walimpenda sana hakuwa tayari kuweka hisia kwamba pengine moyoni wanamchukia.
"Usijali lakini hutakaa milele humu,huwa unafika
Muda aliyekuweka humu akiridhika unatoka.
"Nitamlea mtoto,napenda watoto hata kama usipokuwa mpenzi au mume wangu nitampenda sana na nitamwita....."
"Christian akiwa mvulana au Christina akiwa msichana" alidakia Adam ambaye kwa mbali alianza kumtamani Bite kimapenzi.
                          * * *
         Biashara za baba yake zilikuwa zinaendelea vizuri na skendo lake lilikuwa linafifia taratibu. Hadi anamaliza kidato cha sita Reshmail mapenzi kwa wazazi wake yalikuwa palepale na japo hakutaka kumwongelea Adam jena alikuwa na picha yake waliyopiga pamoja siku moja kabla ya tukio lile la kushangaza na kuumiza. Reshmail kwa ruhusa ya wazazi wa Eveline alienda nae mpaka kwao ambapo walikaa wote kwa siku tano kisha akarejea tena Arusha. Urembo wa Reshmail ulipagawisha kila mwanaume na hata baba yake ilifikia kipindi akakiri kwamba kweli pale alizaa mtoto mmoja wa kipekee na kweli alikuwa wa kipekee. Mama Resh bado alikuwa na matamanio lakini kwa ssa alimwogopa sana Reshmail tofauti na miaka mingi iliyopita.
"Baba na mama wiki ijayo nataka kwenda Mwanza kwa wazazi wa Adam" Resh alitoa hoja yake wakiwa mezani wanakula.
"Wapi? Mwanza! hawatakuelewa mwanangu utakuwa kwa maksudi kabisa unafufua shari iliyopoa tayari.
Tayari"Kwa busara tele na upole mzee Manyama alimweleza mwanae ambaye pia aliyapokea kwa nidhamu ya hali ya juu na kichwa chake kuyakubali kuwa yana maana kubwa ndani yake."Nimekuelewa baba sitaenda tena" alijibu kwa unyenyekevu sana Reshmail.
Muda mwingi wakati anasubiria matokeo aliutumia kuimba na kusikiliza muziki na mara chache sana kwenda kutembelea rafiki zake walioishi jirani naye.
                           * * * *
Matokeo ya kidato cha sita yalipotoka hayakuwa ya kushangaza sana kwa upande wake kwani alikuwa amevuna alichokipanda. Reshmail alikuwa amepata daraja la kwanza na ndivyo alivyotarajia,furaha yake iliongezeka baada ya kumwona katika orodha Eveline Maige rafiki yake kipenzi naye akiwa amepata daraja la kwanza huku wakitofautiana pointi kadhaa. Akiwa anajiandaa kumpigia simu tayari simu yake iliwakawaka na kuandika "pacha" jina ambalo alikuwa amemwandika Eve katika simu yake,badala ya kuongea wote kwa pamoja wakaanza kucheka,walicheka sana hadi simu ilipokatika. Zilikuwa ni furaha kutoka moyoni,kwa nini wasifurahi wakati ndoto zao zilikuwa zinatimia?
Tanzania Commission of Universities (T.C.U) ilipotoa uchaguzi wa kwenda vyuoni Reshmail kama alivyopenda alichaguliwa chuo kikuu cha mtakatifu Augustine Mwanza kwa masomo ya sheria huku Eveline Maige akipelekwa Mzumbe chuo kikuu kwenda kuchukua masomo ya uhasibu shahada ya juu.
"Ndugu hakimu naomba kujitetea!" Eve alimtania Resh utani wao wa shuleni siku walipokuwa wanaagana.Walikuwa wametenganishwa hatimaye lakini mawasiliano yao yalidumu

Kama alivyojiwekea kiapo chake cha kutopenda hovyohovyo ni hivyohivyo alivyoingia pale chuoni,hakuringia uzuri wake lakini hakutaka pia usumbufu unaopitiliza kutoka kwa wanaume yaani kwa kifupi alikuwa na msimamo mkali sana,ni rafiki yake (Eve) pamoja na wazazi wake ambao wangeweza kubashiri sababu hasa inayomfanya binti huyu awe hivi na si mtu mwingine pale chuoni.
Maringo yake yalifichwa na werevu wake darasani,kwani ilikuwa ni warembo wachache sana wa aina yake waliofanya vizuri kimasomo,jambo hilo lililowavutia waalimu wengi sana na wanafunzi ambao wanapenda maendeleo kimasomo. Reshmail hakuwa mtu wa mambo mengi hakunywa pombe wala kwenda kumbi za starehe usiku starehe yake ilikuwa ni kusoma na michezo.
Mnamo mwezi wa pili michezo ya FAWASCO ilipoanza michezo hiyo inayohusisha vitivo vyote pale chuoni,kwa maksudi alichaguliwa kuwa mhamasishaji kwa wasichana wajibu alioufanya vizuri ipasavyo na kikubwa zaidi akawa pia mdhamini mkubwa sana. Moyo wake wa kujitolea uliwavutia sana wanadarasa wenzake ambao baadhi walimpenda huku wengine wakidai ana maringo, msimamo wa Reshmail ulibaki palepale.
Mwaka wa pili pale chuoni ndio ulikuwa mbaya kwake. Darasa walilolitumia mwaka wa pili wanafunzi wa kitivo cha sheria,lililojulikana kama Mombasa Raha kwa mbele lilikuwa na picha kubwa sana ya Adam ambayo ilikuwa pembeni ya ubao wa kufundishia hiyo ikimaanisha kwamba kila atakapoingia darasani lazima aione,"ADAM THE GREAT" yaliandikwa maandishi haya chini ya picha kubwa ya Adam. Amani,ikatoweka kabisa moyoni mwake kumbukumbu mbaya za kumpoteza mpenzi wake Adam zikaanza kumrejea kwa kasi sana.Reshmail akaanza kujihisi yeye ndiye chanzo cha yote hayo,tofauti na waalimu wake hakuna mwanafunzi aliyemfahamu Adam zaidi ya kujua tu historia ya yaliyomkuta na wengi kuichukulia kama simulizi tu ya kusadikika. Reshmail alianza kuwa mtoro darasani na hata alipoingia badala ya kumwangalia na kumsikiliza mwalimu,mawazo yake yote yalivutwa na picha ya Adam yenye tabasamu pana mara zote aliamini inamuangalia yeye na kumlaumu kwa kumkatisha masomo yake kwa penzi la mtandaoni. "Adam stop blaming me!!(Adam usinilaumu)" alipiga kelele kwa nguvu Reshmail bila kujitambua,mwalimu alimshangaa na hakuelewa kilikuwa kimemsibu nini "Is she dreaming? (Anaota?)" aliuliza mwalimu Sijjo aliyekuwa anawafundisha somo la mawasiliano (Communication skills),darasa zima likacheka kwa fujo sana,lakini Reshmail alikuwa analia huku akitetemeka sana,kwa ghadhabu akasimama na kutoka nje. Japo ulikuwa ni mwezi mmoja tu tangu waanze masomo ya mwaka wa pili lakini
tabu na mateso aliyokuwa ameyapata yalitosha kumshawishi kuwa huenda amesoma hapo kwa miaka kumi.Wazazi wake hawakuwa na la kufanya,Eveline alibaki kumwonea huruma shoga yake huyu alijaribu mara kwa mara kumpigia simu lakini haikuwa tiba ya tatizo la Reshmail. Ni kweli Reshmail asingeweza kujilazimisha kuwa na furaha kwani ni yeye aliyemshawishi Adam awe nae kimapenzi na ni yeye huyuhuyu alimshawishi Adam aende kwao kwa ajili ya kujitambulisha na safari hiyo ikawa ya mwisho ya Adam. "Nikiwaambia waalimu wangu watanielewaje,na hata wakinielewa itakuwaje wanafunzi wenzangu wakijua siri hii? watajenga picha gani tena kuhusu mimi,mh! niepushe na hali hi bwana,kama uliweza kuniondolea mawazo haya hadi nikamaliza kidato cha sita vyema hebu baba na sasa ondoa tena na hili jaribu zito mbele  yangu na jina lako lisifiwe." aliweka ombi fupi Reshmail katika mawazo yake hayo. Lilikuwa ni jambo gumu sana kwa Reshmail alikonda sana na punde si punde maneno ya wakosaji yakaanza tena "Mh! kumbe ndio maana anakataa wanaume kumbe anaishi kwa matumaini maskini,dada mrembo kama huyu" yalisikika maneno hayo katika vijiwe vya wanafunzi pale chuoni. Ilikuwa ni kero kubwa kila alipokatiza vidole vilimwelekea yeye umaarufu wake wa awali kwamba ni mrembo ukaongezeka maradufu karibia chuo kizima lakini wakati huu ilikuwa ni sifa mbaya kwamba ana virusi vya UKIMWI hata yeye aliyasikia maneno hayo yalikuwa yakivuma kwa kasi,hakuwa na uwezo wa kuzuia tetesi hizo "Wangejua kwamba mi ni bikra na wanayoyasema yote ni uongo,hata wasingenyanyua midomo yao michafu kuropoka upuuzi huo,lakini bila Adam watajuaje?" alijiuliza Reshmail akiwa chumbani mwake katika hosteli ya Ngulelo aliyokuwa amepanga chumba alichoishi peke yake. Marafiki zake taratibu wakaanza kumtenga wakiamini ameathirika,hilo halikumuumiza kichwa kwani alilitegemea sana hasa hasa dhana ya unyanyapaa  kwa waathirika iliyokuwa inatawala chuoni hapo.
                                ***
Bite alifanikiwa kutoroka katika ngome ile kubwa aliyokuwa amehifadhiwa Adam. Kwa jinsi alivyokuwa amezoeleka pale haikumchukua muda mrefu kumshawishi mlinzi amfungulie geti atoke kidogo na ndio ikawa jumla hakwenda mbali sana na mkoa wa  Iringa bali aliweka kambi yake maeneo ya Uyole Mbeya mkoa uliopo jirani na Iringa ambapo kipesa kidogo alichoondoka nacho pale ndani alifungua kibanda chake sokoni na kupanga nyumba eneo jirani la Igawilo akianzia maisha ya kulala chini hadi aliponunua godoro.Biashara ya kuuza nyanya
na mbogamboga ilimkimu sana maisha yake kwani wazo wala tegemeo lake halikuwa kununua gari,au kujenga nyumba hapana lengo lake lilikuwa uhai pekee,na shilngi elfu moja alizozipata zilikuwa zinamtosha kabisa. Alikuwa mchangamfu na mstaarabu sana,wateja walivutika kwake kwa kasi kufaidi ukarimu wake katika biashara.Tumbo lake lilianza kukua taratibu,kina mama sokoni wakaanza kuhisi tayari Bite kapata mjanja Mbeya amemjaza mimba,lakini miezi yake ya kujifungua ndiyo ilifungua akili za waliokuwa na maswali na kugundua kwamba ile mimba alikuja nayo pale na sio kwamba aliipatia pale. Salama bin salmin Bite alijifungua mtoto wa kiume miezi tisa ilipowadia.
"Mh! baba yake atafurahi tena alimpa jina pale tu nilipomwambia nimeshika mimba" Bite kwa furaha tele aliwaambia kina mama wa pale sokoni,akiwemo jirani yake mama wawili,ni hao ndio walikuwa ndugu zake."Hongera Bite,sijui ndio unakuwa mama nani vile" Bite alihojiwa na mama wawili
 "Mwanangu anaitwa Christian" alijibu Bite huku akibusu kichanga chake hicho ambacho kilikuwa kinarusharusha miguu na mikono yake huku na huko.
        Christian alizaliwa akiwa na afya tele na hakusumbuliwa na magonjwa wakati wa ukuaji wake mwaka wa kwanza,ilikuwa furaha kubwa kwa mama yake.
                             ***
Miaka ilizidi kukatika wazo la Bi. Gaudencia kumtoa Adam katika jumba lile lilikuwepo kichwani mwake kwani udhaifu alioupata Reshmail pamoja na kashfa mbaya anazozipata pale chuoni zilimsononesha sana lakini ataanzia wapi kuificha aibu yake pale ambapo Adam,akasababisha uovu wa mama huyu uwekwe hadharani. Ni jambo hilo lililomuumiza kichwa mama huyu. Reshmail na baba yake watanielewaje kwa mabaya niliyowafanyia,nimeishusha heshima ya mume wangu aliyekuwa na heshima kubwa bungeni" alizidi kuwaza
    Huku Iringa maeneo ya Ruaha Adam alikuwa anauanza mwaka wa tatu,akiishi kama nyumbani kwake,lakini hakuridhika hata kidogo maisha hayo ya ufungwa. Miaka mitatu ilikuwa mingi sana "Mama na baba yangu wanahisi niko wapi? vipi kuhusu mpenzi wangu Reshmail,hapana imetosha nahitaji kutoka hapa,lakini lazima nijiulize nitatoka vipi hapa katika ngome hii" alijisisitiza Adam japo ulinzi madhubuti ulioongezwa kutokana na kutoroka kwa Bite katika mazingira ya kutatanisha pale ngomeni
                          ***
Mwaka wa pili uliisha hivyohivyo kimateso makali yaliyojawa na kumbukumbu mbaya na isingekuwa kuhamishwa kwa darasa la sheria mwaka wa pili kwenda katika maghorofa ya Mwanjonde chuoni hapo basi Reshmail angefeli vibaya masomo yake kutokana na msongo wa mawazo.
     Akiwa mwaka wa tatu afya yake ilirejea tele kwani hakuwa akiiona tena picha kubwa ya Adam machoni pake hali hiyo ya afya kurejea ilizusha msemo mpya tena,tofauti na mwanzo walivyosema ana Ukimwi,sasa walisema "Akikonda ana virusi,akinenepa ameanza kutumia dozi" yote hayo alituhumiwa Reshmail lakini kamwe hakuwahi kuthubutu kunyanyua mdomo wake kujibu vijembe hivyo yeye alikuwa mkimya huku akipambana na masomo hadi alipoumaliza mwaka wake wa nne vyema.
         Mnamo mwezi wa kumi na moja familia yake yote ilisafiri kuelekea jijini Mwanza kusheherekea kwa pamoja mahafali ya mtoto wao,Eveline ambaye tayari alikuwa kazini baada ya kuwa amemaliza miaka yake mitatu chuoni na kufaulu vizuri pia alijumuika katika kukamilisha furaha hii ya rafiki yake mpenzi huku akiongozana na mchumba wake Benjamin Simon. Reshmail alifurahishwa sana na ujio wa Eve kwani alizidi kudhihirisha kuwa ni kiasi gani yeye ni rafiki wa kweli.
Yalikuwa ni mahafali makubwa na ya kipekee kuliko yote yaliyowahi kutokea ambapo chuo cha Mt.Augustino kilifanya mahafali ya pamoja na matawi yake yote Tanzania,yaani Iringa,Mtwara na Tabora. Kwa ufupi yalikuwa yamefana.
Ni katika pirikapirika na pitapita za huku na huko
za sherehe hiyo ndipo Reshmail akiwa na Eveline ana kwa ana anakutana na familia ya Adam yaani baba na mama yake,aliwatambua kwa uwepo wa Rosemary yule mdogo wake Adam. Rosemary alikuwa ndio kwanza amehitimu shahada ya elimu katika chuo kikuu cha mtakatifu Augustino tawi la mtwara hivyo yeye na familia yake pia walikuwepo katika viwanja vya Raila Odinga kusheherekea mahafali yale."Mchawi...mchawi!" alianza kupiga kelele mama yake Adam wakati Reshmail akisogea taratibu katika eneo walilokuwepo kwa furaha "Uuuwii" alipiga makelele kwa sauti ya juu jambo lililovuruga usikivu katika eneo lile na watu kuanza kumwangalia yeye kama mtu aliyechanganyikiwa,Reshmail na Eve walikuwa wameganda tu na mama Adam akizidi kupiga kelele,jitihada za baba yake Adam kumtuliza mkewe hazikufua dafu,mara ghafla mama Adam akakurupuka akiwa na chupa iliyokuwa na soda ambayo haijafunguliwa bado na kwa kasi akaenda kumkabili Reshmail ambaye akili yake ni kama ilikuwa imesimama na umati uliokuwa umemkazia macho kwa kitendo cha kuitwa mchawi ulimzidishia hofu na fedheha kwake,Eve alimshika mkono Reshmail na kujaribu kumvuta watoke eneo lile lakini tayari mama Adam alishawafikia na kwa nguvu kabisa akaituliza chupa ile juu ya kichwa cha Reshmail palepale akaenda chini huku damu nyingi ikimtoka kichwani. Wanaume watatu akiwemo pia baba yake Adam walifika na kumbeba juu juu,mama Adam ambaye alionekana dhahiri kuwa bado hajaridhika na kipigo alichotoa kwa Reshmail kwani bado alikuwa anaangaza huku na huko kama palikuwa na silaha nyingine. Alikuwa kama mwendawazimu
Wengine walimbeba Rshmail ambaye joho lake la kipekee kabisa lilikuwa limechafuliwa vibaya na vumbi la uwanja wa mpirawa miguu wa Raila Odinga ambapo ndio sherehe zilifanyika. Hali ya sintofahamu ilitawala sherehe zile kwa takribani nusu saa nzima hadi Reshmail alivyoondolewa na familia yake kuelekea hospitali na mama Adam kutiwa katika nguvu ya dola
                               ***
Halikuwa jeraha kubwa sana nyuzi mbili zilipita katika kichwa chake kushona jeraha lile
“kwa nini mama mkwe wako akutende hivi” eve alimuuliza Reshmail akiwa pale kitandani
“ni haki yake hata kunipiga risasi mimi ni chanzo cha maumivu haya wanayoyapata” alijibu Resh huku akilazimisha tabasamu
“kwa hio hapa amenionea huruma sana mimi ni sawasawa na muuaji tena wa kukusudia na haki yangu ni kuuawa pia” aliendelea Reshmail huku akitoa tabasamu hafifu tena
“usiseme hivyo mamii sio wewe uliyetaka iwe hivyo ni Mungu pekee” aliongea kwa upole Eve huku akivibinyabinya vidole vya Reshmail
“mama mwambie baba afatilie mama mkwe asije kulazwa selo hata kwa saa moja hana kosa lolote” Reshmail alimwambia mama yake alipoingia katika chumba cha hospitali ya Agha khan aliyokuwaelazwa kwa ajili ya matibabu maneno hayo yalimshangaza sana mama yake aliyetegemea Reshmail atakuwa na hasira ya kutendwa vile mbele ya hadhara
         Nafsi ilikuwa inamsuta sana mama reshmail,moyo uliomba msamaha lakini mdomo ulikuwa mzito sana kufanya hivyo. Hali hiyo ilimkondesha sana na kumkosesha raha ndani kwa ndani unene wake wa asili uliyafunika yote hayo na hakuna aliyejua jambo zito alilobeba mama huyu.
      Kweli badala ya bwana na bibi Manyama kuegemea upande wa mashtaka ili mama Adam apewe adhabu la wao waliunga mkono kwamba Reshmail alikuwa na makosa mahakama ikatupilia mbali mashtaka hayo na mama Adam akawa huru,jambo hilo badala ya kurudisha undugu liliongeza chuki na uadui
“si nilikwambia ukabisha?? Kama hawajamtoa mwanetu kafara kwanini sasa wamekubali niachiwe huru??” mama Adam alimwambia mumewe jambo ambalo wakati huu hata yeye alikubaliana nalo kuwa motto wao mkubwa wa kiume(Adam) alitendwa vibaya na familia ya reshmail . kuamini kwa mzee Michael baba yake Adam ni sawa na familia nzima kuamini kabisa na sumu ya chuki ikamwingia kila mwanafamilia na kuwa aadui wakubwa wa familia ya mzee Manyama.



*       *    *       *        *    *      *       *     *    *    *
Siku mbili alizokaa pale hospitali hakuja hata mwanafunzi mmoja kutoka pale chuoni kuja kutoa pole kwa Reshmail wote waliogopa wakiamini alikuwa mshirikina . Eve hakukubaliana hata kwa mbali na shutuma hizo kwani alimwamini sana Reshmail hivyo aliendelea kuwa pale hospitalini pamoja na mchumba wake kumuuguza Reshmail ambaye alitoka siku tatu baadaye.
“baba mimi nitaenda na Eve kwake nitakaa siku tano ndio nitakuja huko” Reshmail alimpa taarifa hiyo baba yake naye hakupinga kwani amani aliyokuwa nayo Resh akiwa na Eve ilikuwa kubwa mno hali iliyowapa faraja hata wazazi wake hivyo walimruhusu bila kusita.
      Siku hiyohiyo walipanda ndege kwa gharama za mchumba wa Eveline aitwaye Benjamin Simon,kuelekea Iringa ambapo Eve alikuwa amepata ajira katika benki ya N.B.C tawi la hapo.
      Maisha yao yalikuwa mazuri sana kwani Benny alikuwa mwalimu wa shule ya sekondari hivyo katika majukumu waliweza kusaidiana na upendo wa dhati kati yao ulipendezesha zaidi nyumba yao.Reshmail alivutiwa sana na maisha hayo na kumkumbuka sana Adam wake “laiti angekuwepo tungeishi hivi siku moja “ alijiwazia Reshmail wakati akiwaangalia Eve na Benny wakiwa kwenye kochi wamebebana kwa furaha huku wakitaniana
    Ilikuwa jioni moja Reshmail na Eve wakiwa katika mizunguko ya hapa na pale mizunguko ambayo kwa namna moja au nyingine iliibua ghafla safari ya kuingia sokoni,waliingia hapo kununua matunda matunda,zilikuwa zimepita siku tano na tofauti na alivyowahaidi wazazi wake hata hakuwa amefikiria kurudi Dar maisha ya Iringa yalikuwa yamempendeza sana .
“Eveline  ona  eveline jamani angalia kale katoto!!!” Reshmail alimgusagusa begani Eveline huku akimwonyesha kikundi fulani cha watoto pale sokoni
“wewe achana hao machokoraa walionikwapua pochi langu sina hamu nao hata kidogo,kisimu changu cha mchina na shilingi elfu thelathini zikapotelea hewani looh!! Wabaya hao” aliongea kwa hasira Eve huku akisitisha zoezi la kula chungwa aliliokuwa anafanya kwa wakati ule.
“mh!! Eve jamani achaga uongo yaani katoto kama kale jamani hebu kaone kale kadogo “Reshmail alizidi kusisitiza lakini Eve alionyesha bado ana uoga na uchungu moyoni wa kuibiwa vitu vyake na watoto aliowaita machokoraa
“Reshmail shauri zako vitakuliza hivyo we endelea kusema ni vitoto………..mh!!  Resh lakini kale kadogo kazuri kweli” aliongea Eve alipokaona kale katoto ambako Reshmail alisisitiza sana.
“toto zuri jamboo!!”
“sijambo shkamoo!!” kalijibu katoto kale kwa uchangamfu sana baada ya Reshmail na Eve kukasogelea na kukasalimia.
“marahaba mtoto mzuri mbona upo hapa! Mwenyewe au hawa ni kaka zako?” Resh alimuuliza
“a  a sio kaka zangu mi namsubiri mama ameondoka na watu wameenda huko amesema anarudi nimsubiri” alijibu tena kwa sauti ya kitotototo
“umekula??” aliuliza Eve.
“looh!! Eve hujaacha tu maswali yako ya kichoyo ya uchagani  kwenu mh! Unataka aseme amekula ili umnyime au ?” Reshmail alimshushua     Eve kiutani
“mh! Limeniganda shoga,una mashushu wewe!!”  alijibu Eve kiaibuaibu  huku akimpa yule mtoto chungwa lililokwisha menywa  tayari.
“mama anarudi saa ngapi??” Reshmail alimuuliza yule mtoto tena
“sijui nimemsubiri hata hajaja amenipa chai tu akaondoka na wale wanaume wawili” alijieleza vizuri motto yule
“mh!! Mjini mjini tu katoto kanajieleza utadhani mtu mzima dah!” Eve alimnon’goneza Reshmail
“haya twende ukale eti motto mzuri!” Reshmail alimwambia yule motto naye akakubali kwa ishara ya kichwa,akiwa pekupeku akafuatana na Reshmail hadi kwenye mgahawa ulioandikwa “MAMA FRED MGAHAWA” uliokuwa pembeni kidogo ya soko kuu la Iringa.
“utamsalimia mama eeh!!” baada ya kumnunulia chakula walilipa na kumuaga
“haya mamdogo!” alijibu yule motto
“unaitwa nani vile”Eve akamuuliza
“naitwa Christian motto wa mama Bite” alijibu na wote kwenye mgahawa wakacheka




Kuifananisha na picha ya Adam,dimplez za yule mtoto zilimfananisha kabisa na Adam,achilia mbali rangi yake ya maji ya kunde na ucheshi wake.
"Eve hapana,mbona kesho naenda kumtafuta Christian ili nimjue baba yake anavyofanana,haiwezekani kufanana kwa kiasi hchi hapana "Aliongea Resh huku akiifunika album ile . Eve alikubaliana naye na siku iliyofuata majira ya saa nne,walikuwa katika hoteli ya yule mama ambapo walimwacha Christian.
"Nyie watoto ni kesi gani hyo mmetaka kuniachia jana" mama mnene kiasi mmiliki wa mgahawa wa Mama Fred aliwapokea kwa maneno hayo makali huku akifunga kanga yake vizuri kiunoni. Resh na Eve hawakuwa na jibu la kutoa walidhani amewafananisha labda "Mama ni nini tena,mbona sisi...." alijaribu kujieleza Eve huku akiishiwa maneno ya kujieleza.
"Mmenitekelezea mtoto hapa anaanza kunililia hapa usiku he! jamani mnataka mniuwe kwa presha mkurya wa watu mie" aliongea kwa ghadhabu na mshangao mkubwa sana yule mama.
"Mama sisi tumempata hapo sokoni,ndio kumleta hapa kwako kwa ajili ya kupata chakula tu mama yangu" Reshmail alinyanyua mdomo wake na kuzungumza kwa sauti iliyojaa mshangao pia.
"He! mauzauza gani haya jamani,mi nimempeleka pale kituo cha polisi usiku uleuule ndugu






**************************************

*           *        *       **     **    **        **       *

Baridi kali ya Mbeya ilikuwa imemkataa motto wa Bite (Christian) kwa hali hiyo alipotimiza miaka miwili waliondoka na kurudi tena Iringa ambapo Bite alitaka kukaa kidogo halafu aende Mwanza kuweka makazi mapya huko. Jambo la kushangaza licha ya baridi ya Iringa hali ya Christian ilianza kuwa njema kama awali jambo lililosababisha Bite aendelee kukaa katika mkoa huo.hadi anatimiza miaka mine hali yake kiafya ilikuwa njema sana na tayari Bite alikuwa amesahau suala la kwenda Mwanza.akaanzisha genge la kuuza uji na karanga mida ya jioni na mihogo ya kukaanga majira ya asubuhi. Ilikuwa biashara ndogo lakini iliyomuingizia kipato kizuri tofauti na matarajio yake.aliweza kupanga nyumba ya chumba kimoja na sebule aliyoishi na mwanae kwa furaha sana tu bila masumbufu yoyote hadi siku hiyo asubuhi alipokuwa anauza mihogo yake ambapo wanaume wawili ambao sura zao hazikuwa ngeni machoni pake walipofika eneo la biashara yake.Aliwapokea kwa furaha sana na bashasha kama wateja wengine aliozoeana nao.”Bite tukuone pembeni kidogo samahani lakini’ wawili wale walimvuta pembeni Bite
“mh! Mikopo asubuhi asubuhi hamna kwakweli mtadhalilisha hizo suti zenu” aliongea Bite kwa utani huku akiwafata walipo wawili hao
“funga biashara tunaondoka na ukithubutu kupiga kelele au kukimbia nasambaratisha ubongo wako nadhani hujawahi kufikiria kifo cha namna hiyo,hivyo basi fanya kama unavyoagizwa” aliambiwa Bite na wale wanaume huku mmoja akifunua koti lake jeusi la suti na kumwonyesha Bite kitu ambacho hakujiuliza mara mbili mbili kuwa ile ilikuwa ni Bunduki,kwa kuutambua uoga alioupata Bite,yule mwenye bunduki alimbandika kitu mfano wa kishikizo cha nguo na kumwambia “hiyo ni sound recorder nenda ukawaambie wateja wako sisi ni  ndugu zako tumekuletea taarifa za msiba nitakuwa nakusikiliza hapa,ole wako nasema ole wako usifuate maelekezo” alipewa masharti hayo ya uongo Bite ambaye laiti isingekuwa pensi yake ya jinsi ambayo huwa anavaa kwa ndani ili kuhifadhia pesa zake za mauzo basi mkojo uliopenya bila yeye kujua ungemwagika palepale hadharani na wala asingepatwa ma aibu yoyote ile.Kama alivyoagizwa aliwaeleza wateja wake wawili waliokuwa wanamalizia kuitafuna mihogo waliyokuwa wameinunua,wakampa pole za dhati . jasho lilikuwa linamtoka alitamani kutumia ishara kuwaambia kwamba yupo katika hatari lakini alipowazia mdomo wa bunduki alikaa kimya kabisa,bila kificho Bite aliiogopa sana bunduki na hakupenda kumwacha Christian katika umri ule.Tayari akili ilisharudi nyuma akatambua hasa,hao  watu alikutana nao wapi,walikuwa ni baadhi ya  wafanyakazi katika ile ngome aliyekaa miaka miwili na ni hao  waliomleta Adam pale ngomeni “nimekwisha mimi Beatrice” alijiwazia Bite huku akitetemeka.
     Baada ya kuifunga biashara yake aliwafuata akiwa na mwanae amemshikilia mkono.
“nadhani unajua hatuhitaji mtoto!!! Tunakuhitaji wewe tena sasa hivi” aligombezwa Bite na bila kujijua akajikuta akimwacha mwanae pale “Christian narudi sawa nisubirie pale sokoni sawa mwanangu! “haya mama alijibu Christian kwa furaha kwani alijua amepata fursa kubwa na ya kipekee  kwenda kucheza na watoto wenzake pale mtaani
 “ulidhani unaweza kutuzidi ujanja sisi,umepotea sisi hatupimiki hata kidogo umeumia tena  umeumia sana aliambiwa Bite na wale wanaume wakiwa kwenye gari kuelekea kwenye gari kuelekea kule katika ngome jambo hilo Bite hakulitamani hata kidogo,japo alimpata Christian kwa bahati mbaya lakini alikuwa akimpenda sana kutoka moyoni na hakuwa tayari kutenganishwa naye kwa namna yoyote ile.Alijiuliza maswali mengi sana ni nani atakayempa chakula mwanaye siku hiyo na nyingine zitakazoendelea wakati yeye hayupo,michezo ya kukimbizana aliyoipenda Chriss pia ilimtia hofu Bite na kuhisi huenda mwanae anaweza kupoteza uhai wake kwa kugongwa na gari. Funda la hasira lilimkaba kooni alitamani kufanya lolote lile wakati huo lile jambo liwe ndoto kwake, machozi yaliyotoka ndio yaliyeyusha lile fundo japo kidogo,hasira kali ilikuwa imemkaba Bite aliyekuwa amekaa siti ya nyuma na jamaa mwenye Bunduki katika koti lake lakini maskini hakuwa na la kufanya hadi gari lilipoingia ndani ya ngome ile

*             *         *     *                 *
Macho ya Reshmail yalitawaliwa na taswira ya yule mtoto Christian,zilikuwa ni siku nyingi zimepita tangu afungue album yake kumwangalia mpenzi wake (Adam) aliyeaminika kuwa tayari ni marehemu.Ni katika usiku huu alipokuwa akipitia album ya Eveline ndipo tena anakutana na picha ya Adam ambayo yeye (Adam) alimpa Eveline walipoenda Mwanza.”Eveline,Eveline,Eve……….huyu hapa ni nani???”
“we umechanganyikiwa  tena eti hebu acha mambo yake ya ajabu huyu Adam” Alijibu Eve kwa uoga.
“ na tuliyemwona leo kule sokoni ni nani??” aliuliza Reshmail
“we Reshmail jamani wanafanana Mungu wangu mbona wamefana hivyo lakini eeh!! Eve alijikuta picha ya mtoto Christian ikiumbika kichwani mwake na
                                                            
Zangu kwa sababu nimekaa naye hadi saa nne tumemsubiri huyo mama yake aje wapi!! Nikaona isiwe shari ngoja nimpeleke polisi penye usalama kuepuka balaa kumbe na nyie hamjui ni wa nani he!!” alitoa maelezo hayo yule mama na kueleweka vyema kwa Reshmail na Eveline.
“hicho kituo cha polisi umesema kipo wapi?” aliuliza Eve
“kile pale kinaonekana hata kwa hapa,lile jingo la bluu nyuma yake” alielekeza yule mama
Ndani ya dakika tano tayari Reshmail na shoga yake walikuwa mbele ya mapokezi ya kituo cha polisi Iringa mjini
,na walikuwa kwenye foleni wakisubiri zamu yao ya kuhudumiwa ifike.
“nyie ni ndugu zake? Au mmoja wenu ndio mama yake?”
“hapana sisi si ndugu zake ila……”aliishia njiani katika maongezi yake Resh baada ya kukatishwa na yule askari “ila nini? Yaani nyie wanawake wa siku hizi suala la kujali watoto wenu hamtaki kabisa kulisikia mnachojali ni urembo tu wa sura zenu”
“jamani sio kwamba kuna ndugu yake hapa kati yetu ila sisi tumemkuta jana kule sokoni ndio tumemnunulia chakula halafu tukajiondokea zetu,leo hii ndio tunapita pale kwa mama Fred yule mwenye mgahawa yeye ndiye ametupatia taarifa hiyo tukaona sio vibaya nasi tukifika kumwona huyo motto” aliongea Eve aliyeonekana kutokuwa na hofu na kituo cha polisi lakini Reshmail alikuwa ana uoga kwa mbali kama vile anatuhumiwa kwa lolote lile.
“haya yupo tumemuhifadhi na tumepeleka taarifa kwenye vyommbo vya habari wataanza kutangaza kama mama yake  bahati mbaya haya atakuja kumchukua na kama amemtelekeza akajiandae kwenda kuishi kwa watoto yatima sisi hatuna uwezo wa kuhifadhi watu hapa zaidi ya mahabusu” alijieleza askari yule huku akijipepea joto kwa kutumia kofia yake iliyochakaa
Majuma mawili yalipita bila mama wala ndugu wa motto kupatikana licha ya kituo cha redio maarufu mjini iringa cha Ebon fm kutangaza kila siku bila kukoma
“eve naenda kumchukua yule motto nafsi yangu inanishauri hivyo na ni lazima nifate ambacho nafsi yangu inaniamuru” Reshmail alimwambia Eve siku moja wakiwa wamekaa sebuleni wakiangalia habari katika luninga.Eve alikuwa amejenga tabia ya kutobishana na rafki yake huyo kwani furaha yake ilikuwa ni kumwona Reshmail akiwa na furaha tele
“lakini Resh,mama yake si atamtafuta ssana??”
“Eve yaani imetangazwa hivyo redioni na hajajitokeza leo hii mie tu kumchukua ndipo ajitokeze? Looh! Acha nae ahangaike kidogo” alijibu Reshmail kwa jeuri
“mh! Haya sikuwezi mwanasheria wangu”
Polisi hapakuwa na usumbufu ni wazi kwamba walikuwa wamechoshwa na matukio ya watoto kutelekezwa na wazazi wao pasipo sababu zilizo wazi,hivyo kitendo cha Resmail kuamua kumchukua Christian ilikuwa ahueni kwao.aliandiokishwa maelezo mafupi tu kabla ya kuruhusiwa kondoka na mtoto ambaye alikuwa dhaifu tayari kutokana na lishe duni na upweke wa kutomuona mama yake kwa siku hizo zote.
     Reshmail alikuwa ameyafurahia sana maisha ya Iringa,kampani kubwa kutoka Eveline na mchumba wake ilibeba nusu ya furaha yake huku nusu nyingine ikikamilishwa na uwepo wa Christian mikononi mwake,mara kwa mara alipenda kuwa naye karibu huku akimwita mume wako jambo lililompa faraja kubwa moyoni
”Eve jamani nitakumiss kipenzi changu lakini nitarudi tena asanteni sana kwa ukarimu wenu mlionionyesha tangu mwanzo nimeishi kwa furaha kubwa sana hapa” Reshmail aliyazungumza hayo alipokuwa anawaaga Eve na Benny usiku ambapo kesho yake alitegemea kurejea Dar-es-salaam akiwa ameandamana na Christian mtoto aliyempata katika mazingira ya kutatanisha
Kwa Christian safari ya kutoka Iringa kwenda Dar ilikuwa safari yake ya kwanza ndefu zaidi kuwahi kusafiri
Siku iloyofuata wawili hawa walikuwa ndani ya basi la ‘budget’ litokalo Mbeya kwenda Dar likipitia Iringa.
“Mama alisema baba yupo pale kwenye ile nyumba, tushuke nikamsalimie!” Chriss aliongea hayo huku akielekezea kidole chake kwenye jingo lililoonekana kwa mbali mno kutokea pale barabarani na hapakuwa na dalili ya kuishi mtu pale hivyo Reshmail akachukulia kuwa ni akili ya utoto imemtuma Chriss kuzungumza akaamua kupuuzia
“chriss alikwambia nani we muongo!!”
“alinambia mama siku moja hivi tulipita hapa ,halafu mama alinikataza kusema uongo ni dhambi” alijieleza Christian haraka haraka
“mh! Haya tutakiuja siku nyingine sawa mfalme wangu” Reshmail alimjibu Chriss ili kumlidhisha kwa aliyokuwa anasema

             **                 **                       **                **
Nyumba tulivu kabisa ya mh.Manyama ililipuka kwa furaha kwa kurejea kwa Reshmail akiwa mwenye furaha tele “umetuletea na mjukuu!!” alitania mama Resh.”mtoto wa Eve huyu anamwita mama mdogo” Resh naye akdanganya “kazuri kweli kama………………” alisita kumalizia baba yake “ni kama Adam baba usiogope kufananisha wamefanana kweli” alimtoa baba yake wasiwasi huku akimkumbatia baba yake kasha mama yake.
“mh!! Tulikuwa wapweke kweli jamani dada” msaidizi wa kazi za ndani aliyeitwa Fatuma alimwambia Reshmail huku akimkumbatia na kumbusu shavuni
“na huyo mtoto kama mwanao vile hebu kaone” aliendelea Fatuma
“sio kama wa kwangu ila ni wa kwangu humwoni alivyonifanana?” alijibu kimzaha na wote wakacheka kwa pamoja
            **          *****            *****
Hali ya sintofahamu iliwakumba wale wafanyakazi wa lile jumba (ngomeni) alipokuwa anatunzwa Adam. Mkuu wa ngome hiyo bwana Lwebe alikuwa na ghadhabu kubwa sana,kila  mbua alikuwa na ghadhabu kubwa sana,kila kitu kilikuwa shaghala baghala kila mara aliongea kwenye simu hukuakitoa vitisho vikali sana na hata kutishia kuua. Wafanyakazi hawakumwelewa lolote walizitambua hasira za bosi wao huyo ambaye mara chache anazokuwa katika hali kama hiyo humalizia hasira zake kwa kutoa roho ya mtu
“mlete Adam hapa mara moja !!” aliamrisha huku akijikuna ndevu zake kwa kutumia mdomo wa bunduki aliyokuwa nayo
“maskini Adam sijui amekosa nini” alijiuliza aliyekuwa anaenda kumwita. Bila wasiwasi wowote Adam akamfikia Lwebe D kwa ishara ya mkono akamwamrisha kumfuata,pamoja na mabaunsa wawili waliotinga suti nyeusi . lwebe hakuongea neno lolote hadi walipofika kwa nje,tayari kigiza cha saa mbili kilikuwa kimetawala
“mlete na yule mwingine wa nyumba ya chini” alitoa amri nyingine tena baada ya tano walioagizwa wakarejea na mtu mwingine
“we kinyamkera una bahati sana aliyekuleta hapa amesema haujasambaza taarifa zozote mbaya laiti kama ungethubutu ningeiondoa shingo yako sasa hivi. Nakuacha uende tena lakini tambua mtandao wangu upo popote katika nchi hii sasa ole wako uthubutu kunyanyua mdomo wako kutangaza ujinga” aliambiwa yule binti aliyeletwa pale huku akionyeshwa njia ya kutokea
“we kidume kwa jeuri ya bosi wako kujaribu kunidhurumu pesa yangu wakati wewe unakula na kulala bure hapa;lazima nimwonyeshe mimi ni nani na ni wewe utakayeumia” aliongea Lwebe huku akipuliza moshi wa sigara hewani.
                                        **********
Ilikuwa ni mwezi mmoja tangu Bite arejeshwe kwenye ile ngome lakini katika chumba kingine,hakuwa msaidizi wa kazi tena bali mtuhumiwa na hakupata fursa ya kuonana na Adam hata siku moja . siku alipotolewa nje usiku na kwa mahesabu ya miaka mitano ambayo Adam angekaa pale machale yalimcheza,alivyopewa uhuru wa kuondoka hakwenda mbali sana alifika eneo moja kwenye mtaro na kuanza kusubiria ni nini kitatokea japo hakusikia vizuri maneno lakini alisubiri hata vitendo
    Mkataba wa miaka mitano alioandikishana Bi.gaudensia na Lwebe wa Adam kuhifadhiwa pale ulikuwa umeisha tayari na miezi mitatu zaidi ilikuwa imepita,suala hilo la kuchelewesha pesa lilimkera sana Lwebe na pia ahadi za uongo kutoka kwa Gaudencia zilichochea sana hasira za Lwebe kufikia hatua ya kuamua kuzipooza kwa huyo Adam aliyehifadhiwa hapo.ni usiku huo alipoamua kwa mkono wake mwenyewe Adam duniani kama kisasi kwa Bi.Gaudensia
“paa!! Paa!!” mlio mkali wa risasi ulisikika na kumzindua Bite ambaye alikuwa amepitiwa na usingizi pale kwenye mtalo,kidogo apige kelele lakini viganja vya mkono wake vikawahi kuuziba haraka sana. Hakusikia hata chembe ya kilio na baada ya dakika kama saba akasikia milango imefungwa
Kwa ujasiri na tahadhari kubwa Bite akajisogeza hadi karibu kabisa na eneo ambalo aliamini hakika ndipo mlio wa risasi umetokea huku kichwani kwake akiwa ana jibu la “nimesahau saa yangu” iwapo atakutana au kushtukiwa na mlinzi,kwa hofu alizurura katika lile eneo dakika tatu bila kuona chochoten”au wameingia nae ndani??” alijiuliza bila kupata jibu
“koh!!  Koh!! Alishtuliwa na sauti ya kikohozi nyuma yake,mawazo yake alidhania ni mlinzi eneo lile lakini alipogeukz hakuwa mlinzi tena ni mwili wa binadamu ukiwa chini,hakutambua mara moja yule ni nani hadi macho yake yalipolizoea giza la pale “Adam!!!!!”
“we ni nani??” alijibiwa kwa sauti ya chini sana iliyokuwa inaunguruma kama mnyama anayechinjwa
“Bite mimi jamani Adam”
“ondoka watakuua hao Bite ondoka niache mi nife hapa” alijibu Adam
“hapana Adam usife,usife Adam twende tukamtafute mwanetu Chrstian anatamani sana kukuona,usife Adam tafadhali” Bite alibembeleza
    Risasi mbili zilizopenya katika paja lake la kulia zilikuwa zimemsababishia Adam kuvuja sana damu na mbele yake alichokitarajia ni kifo hakuna kinginelakini maneno ya Bite nguvu zilirejea upya kabisa tena kwa kasi”Bite ulijifungua,mtoto wangu yuko wapi? Ni wa kiume au wa kike?” alihoji maswali mfululizo Adam huku akijitutumua kusimama kwa nguvu alizokuwa amezipata
“ni stori ndefu na hapa sio mahali pake tuondoke tafadhali jitahidi kuna hatari kubwa kama unampenda mwanao jitahidi tuondoke” aliongea Bite huku akiuweka  mkono wa Adam katika bega lake na kuanza kumkongoja kutoka eneo lile huku (Adam) akitumia mguu mmoja na ule uliojeruhiwa ukiwa juu juu.kutoka pale walipokuwa hadi barabarani haukuwa umbali mrefu sana na walifanikiwa kufika,kwa giza nene lililokuwepo hawakuweza kuonekana na mtu yeyote,nguvu zilikuwa zinamwishia Adam kutokana na kuvuja damu lakini alijikaza kijasiri sana na kuendelea mbele
*********     *******     *******
Lwebe na kundi lake baada ya kumpiga risasi  mbili Adam waliamini katu asingeweza kunyanyuka kutoka katika eneo lile,na hata angeweza kuinuka hakuwa na pa kwenda hakuujua mkoa huo hata kidogo. Waliingia ndani na kupiga simu kwa Bi.Gaudensia kwamba mtu wake tayari ana risasi mbili mwilini
“msimuue jamani,tafadhali sana kesho naileta pesa yenu mapema kabisa”
“nimechoshwa na ahadi zako mheshimiwa jiandae kuchukua maiti yako siku yoyote utakayotaka utaikuta nimeihifadhi na kama na kuizika nitakusaidia” alijibu kwa ghadhabu kasha akakata simu
Bi Gaudencia akapiga tena
“nakusikiliza”
“basi nielewe kwa leo na hili ni ombi la mwisho tafadhali usimuue kesho asubuhi sana nakuja huko,ninaondoka huku saa nane usiku tafadhali” alibembeleza
“na iwe hivyo atalala nje leo na hata kula hadi utakapokuja
“sawa mkurugenzi” alijibu kwa unyenyekevu Gaudensia
Akini ya Bi.Gaudensia  ilifanya kazi haraka haraka akapekua kila kona katika chumba anacholala na mumewe na kwa bahati nzuri kwa akakutana na kadi ya benki ya mume wake ambayo alikuwa akifahamu vizuri kabisa namba zake za siri. Bila kupoteza muda akampigia dereva wake wa siri ambaye huwa anampeleka Iringa naye haraka haraka bila kuhoji akatii amri aliyopewa.bila Reshmail kujua Bi.Gaudensia akaondoka majira saa saba usiku,nafsi ilikuwa ikimuhukumu juu ya baya lolote litakalomkuta Adam “damu ya Adam ipo juu yangu”
“naenda kwa rafiki yangu ameugua ghafla “ mama Reshmail alimuaga mlinzi wa getini
“sawa bosi” alijibu mzee yule wa makamo huku akifunga geti baada ya mama kuwa ametoka nje
Kwa kasi ya ajabu gari iliondoka jijini Dar-es-salaam kwa kuwa ilikuwa usiku sana vizingiti vya watu wa usalama pamoja na foleni havikuwepo sana hivyo dereva alikimbiza gari kwa  kadri ya uwezo wake. Breki ya kwanza ilikuwa ni katika benki ya C.R.D.B maeneo ya Ubungo ambapo mama Reshmail alishuka na kuvuta pesa kutoka katika akaunti ya akiba ya mzee Manyama
Badala ya masaa matano kwa gari binafsi kufika Iringa walitumia masaa matatu pekee
“mh!! Huku napo kijijini kweli huyo nae sijui ni mgonjwa sasa usiku huu atapata wapi lifti ya gari” mama Reshmail alimwambia dereva wake alipoona watu wawili wakisimamisha gari
“ah!! Ndo maisha ya Tanzania yalivyo” alijibu dereva huku akiongeza zaidi mwendo wa gari hadi wakaifikia ngome ya vigogo waliyokuwa wakiifuata

****     ****    *****
Magari makubwa ya mizigo yatokayo Morogoro kwenda Zambia na Malawi ndiyo yaliyotoa msaada kwa Bite na Adam ambapo Bite alijitambulisha kama mke wa Adam na kwamba wamevamiwa na majambazi na mumewe (Adam) amepigwa risasi. Laiti kama madereva wangekuwa watanzania kwa jinsi walivyo waoga katu wasingewapandisha wawili hawa lakini wakongomani wale ambao vita kwao ni jambo la kawaida waliwachukua Adam na Bite hadi Iringa mjini walipowaacha jirani kabisa na hospitali ya rufaa.
“bila RB hatupokei mgonjwa wa aina hii” alisema muuguzi wa kike wa hospitali ile wakati Bite anajieleza.ni kweli yule muuguzi(nesi) alikuwa na haki zote za kupingana na ujio ule kwani hali aliyokuwa nayo Adam ilihitaji taarifa za polisi kwanza
“haa!!! Mama Christian,ni wewe hata siamini au nakufananisha?” wakati Bite akijiegemeza kwenye ukuta huku akiwa amekata tama alishangaa kutambulika kwake na nesi yule
“Mungu wangu mama wawili jamani!!!” baada ya kumkazia macho naye Bite akamtambua yule nesi kuwa waliwahi kufanya nae biashara katika soko la Uyole Mbeya na pia alikuwa jirani yake pale alipokuwa anaishi,ulikuwa mshangao mkubwa sana
“ehe!! Kulikoni tena ndugu yangu yamekukuta yapi tena mwenzangu?” alihoji nesi huku akiwa amechangamka sana safari hii
“ni makubwa sana,lakini ningeupata msaada wako kwanza kwa mume wangu ndio tungeongea vizuri shoga” alijibu Bite akiwa na matumaini tele
“ondoa shaka shoga huduma mnaipata sasa hivi tena huduma bora,daktari tunaheshimiana naye sana na pia ni shemeji yangu” nesi aliongea hayo huku wakisaidiana kumwingiza Adam ndani ya chumba cha wagonjwa,hapakuwa na maswali mengi,undugu ulitawala pale. Adam akafanyiwa upasuaji mdogo wa kuondoa risasi katika ambao haukuchukua hata hata nusu saa damu na maji pia vikaongezwa katika mwili wake uliokuwa dhaifu sana.kufikia majira ya saa kumi na moja alfajiri Adam alikuwa amepata nafuu kubwa na aliweza kutembea japo kwa kuchechemea
“shoga nikueleze wazi tu kwamba sisi pa kufikia hapa Iringa mimi na mume wangu hatuna! Tangu niondoke ghafla niliacha sijalipa kodi nina uhakika chumba sio changu tena kwa hiyo pa kwenda hatujui” Bite alimweleza hayo mama wawili baada ya kuwa amemsogeza pembeni ili mtu mwingine asiweze kusikia
“ondoa shaka Bite miim kwangu pana nyumba kubwa tu!! Nimejengewa na mnyakyusa mmoja,nimemweka kwenye kiganja kwangu mimi hasikii,haoni wala hasemi,ni kaka yake na huyu daktari we mwenyewe si umeona alivyowashughulikia haraka” kwa sauti ya chini kabisa nesi alijibu
     Wote watatu katika teksi wakaongozana hadi nyumbani kwa nesi ni kweli nesi hakuwa na chembe ya utani hata kidogo  nyumba ile ilikuwa kubwa sana na haikuwa haki kukaliwa na watu wawili pekee vilikuwa ni vyumba sita pamoja na sebule
“karibuni! Karibuni sana! Nesi aliwakaribisha walipofika nyumbani kwake.
“asante sana ndugu yangu ama kweli ishi na watu uvae viatu” alisema Bite kwa upole sana
“usijali Bite tumeishi vizuri,hatukuwahi kugombana hata siku moja,tumetwishana matenga ya nyanya kwa nini sasa nishindwe kukutendea wema!!!” nesi alimtoa hofu Bite
Chumba walichopewa kilikuwa kikubwa cha kuwatosha kabisa,kitanda cha tano kwa sita kilikuwa saizi yao kabisa. Adam alishangazwa sana na wema huo wa nesi lakini mshango wake uliongezeka maradufu baada ya kukutana na mume wa nesi siku ambayo walikuwa wakitambulishwa kwake kama shemeji zake yaani ndugu zake Bite.mzee huyu wa kinyakyusa aliyeitwa Gwakisa ni kama heshima ilipitiliza na kuwa kama anawanyenyekea wawili hawa. Adam alihudumiwa na yule daktari kana kwamba alikuwa ni mgonjwa wa kisukari au alikuwa ni mtoto wa mfalme,Adam alipata farijiko kubwa sana kuishi pale
Bite kama kawaida alikuwa mwanamke wa kujituma  sana,ndani ya wiki moja tayari alikuwa amepata kazi ya ndani katika nyumba nzuri waliyoishi wanafamilia watatu,mwanaume na mke pamoja na mtoto wa kama miaka mitatu wa kike aliyekuwa anasoma shule ya awali

*****    ******     ******     ******
“bite mama!!”
“bee mama”
“mpeleke mtoto shule halafu baadaye mpeleke pale zahanati akapimwe jana usiku amekohoa sana” ilikuwa sauti ya Eveline akimpa maelekezo Bite ambaye alikuwa mfanyakazi wake mpya na wa kwanza wa ndani ya nyumba yake na mchumba wake. Ratiba ya Bite ilikuwa ni kazi kuanzia asubuhi ya saa mbili ambapo alikuwa akimpeleka Loyce {mtoto wa kaka yake Benny} shuleni na kisha akirejea anaandaa chakula cha mchana kwa siku ambayo Benny hurudi nyumbani mchana  na baada ya hapo humfuata Loyce shuleni,kisha maandalizi ya chakula cha jioni na majira ya saa kumi na mbili huaga na kuondoka,ilikuwa kazi ambayo haikumtoa jasho Bite na malipo ya shilingi laki moja kila mwezi yalimtosheleza kabisa kupanga chumba kidogo walicholipia shilingi 15000 kwa mwezi
“tunashukuru sana kwa ukarimu wenu bwana na bibi Gwakisa Mungu awazidishie baraka katika kazi zenu” alitoa shukrani za dhati Adam kwa niaba ya mke wake wa bandia (Bite).uchangamfu wake na wingi wa vituko ulifanya nyumba ya Gwakisa iwe iwe yenye shangwe na tabasamu kila siku,kitendo chake cha kuaga pale kilimsononesha Gwakisa na mkewe lakini hawakuwa na jinsi,kutoka mfukoni mwake aliwakabidhi shilingi laki mbili za kuanzia maisha yao huko waendako
Tayari Adam alianza kumpenda kwa dhati Bite uchapakazi wake na jinsi alivyomwokoa kutoka katika kifo ulichangia sana lakini kiunganishi cha mtoto Christian ndio ilikuwa chachu kubwa ya mapenzi yao.walivyohama katika nyumba yao ya kupanga walianza rasmi kuishi maisha ya mke na mume Adam hakuwa na amani hata kidogo na familia ya Reshmail hasa baada ya kukuta katika nyumba  hiyo ndogo waliyohamia magazeti yaliyobandikwa kama mapambo likisema “imani za kishirikina zamwondoa mheshimiwa Manyama bungeni” alitamani sana kuisoma habari hiyo kiundani iliyotoka takribani miaka mitano iliyopita lakini ilikuwa imeandikwa inaendelea ukurasa wa pili anbao haukuwepo pale ukutani
“au walikuwa wanataka kunitoa kafara? Mungu wangu!! Niliwakosea nini mimi” alijiuliza Adam wakati wakiingiza yao ya Rambo ndani ya chumba hicho kimoja kilichotenganishwa na pazia kufanya sebule na chumba
Hisi hizo mbaya zikamfanya Adam aamue kuanzisha rasmi uhusiano na mwanamke ambaye amezaa naye mtoto pia aliyeokoa maisha yake bila kutarajia mwanamke ambaye hajawahi kumkwaza,mwanamke mpiganaji anayempa furaha tele kila siku
“Bite nataka uwe mke wangu”
“Mh!! Niwe  mkeo mara ngapi mimi mkeo tayari jamani” alijibu Bite huku akichezea ndevu za Adam ikiwa ni siku ya pili tu tangia wahamie katika makazi hayo mapya
“una utani wewe mbona ulikuwa hujaniambia wala sijawahi kusikia ukiniita mume wako?
“sio lazima nikwambie tayari nina mtoto wako halafu humu ndani kuna kitanda kimoja tena kidogo tu,ulidhani chako mwenyewe!!!” aliuliza Bite kisha wote wakacheka huku wakikumbatiana na kuangukia kitandani

****              *******
Maisha ya Reshmail jijini Dar-es-salaam yalikuwa yamebadilika sana akiwa anasubiri wakati baba yake akimtafutia kazi itakayompendeza alifurahia mara zote na Christian huku akiwa amewabadili watu wote wanaomfahamu kwa ukaribu kutokea kumwita Reshmail na sasa walimwita mama Christian na alikuwa amejivika pete ya ndoa  katika kidole chake cha shahada ikwa na jina Adam na nyingine ndogo akiwa amemvisha Christian ikiwa imeandikwa Reshmail.
Hakuwa mtu wa kulialia tena wala msongo wa mawazo haukumsumbua tena aliamini nafasi ya Adam ilikuwa imezibwa vyema na Christian ambaye alikuwa Adam mpya kwake. Walilala wote,walicheza wote na kusimuliana mambo mbalimbali.alipoenda kusalimia rafiki zake walienda wote Christian mkono wa kulia. Harakaharaka Christian alijikuta akimpenda mno Reshmail kuliko hata ilivyokuwa kwa mama yake mzazi,maisha ya kifahari ya kwao Reshmail yalimfanya Christian anawiri sana ungewakuta wakicheza bustanini kama vile wanalingana umri walibembea pamoja na kupigana kiuongouongo,kwa ufupi waliishi maisha ya kusisimua kwa kila aliyewaona. Akiugua Reshmail ni Christian atamuuguza kwa kukaa pembeni yake bila kutoka nje hadi apone hivyo hivyo kwa Reshmail abaye alimwogesha na kumlisha. Wakati huo Reshmail ndio alikuwa mwalimu wa Christian akimfundisha kusoma na kuandika jambo ambalo hata baba yake alilipenda na Christian alikuwa mtu anayeelewa haraka akifundishwa ,reshmail alifurahia sana.
Baada ya kukaa na Christian mwezi sita reshmail kwa mara nyingine Iringa kwa rafiki yake jambo kubwa lililompeleka huko ni harusi ya rafiki yahe huyo ambapo alitarajiwa kuwa matron wa kipenzi chake hicho.
“shoga shughuli kesho kutwa hata haujaonekana jamani au ndio mambo yetu yale haja ya kufanyiwa make up….”aliuliza kiutsni .Eve katika simu alipokuwa anaongea na Reshmail.
“Kesho asubuhi na mapema nakujua ,mume wangu alikuwa na mafua ndio tatizo si unajua tena.”alijibu Reshmail.
Haya mume huyo anavyoringiwa shauriro “alijibu Eve .Christian alikuwa amependekezwa kuwa bwana harusi  mdogo pamoja na Loyce (mtoto wa kaka yake Benny).
“He unatoka mume wangu asiuze sura,na jinsi alivyoandaliwa huku Dar es salaam ,utachoka mwenyewe na simtoi  mpaka siku ya shughuli,atakayeruhusiwa kumuona ni bibi harusi mdogo(Loyce) peke yake wakati wa kujifunza,sitaki mwingine amuone mpaka siku yenyewe”alijibu Reshmail kwa furaha.
“Haya umeshindwa ambao hatuna waume tunalo,alijibu  Eve kisha wakaagana.
Asubuhi ya siku iliyofuata majira ya saa nne asubuhi tayari Reshmail,Christian,mpambaji pamoja na dereva walikuwa ndani ya gari la baba yake (Resh)taratibu safari ya Iringa ikaanza.
“Usitupeleke kwa kasi sawa eeh,alitoa malekezo Reshmail na kukubaliwa na dereva kwa sababu hawakuwa na haraka yeyote ila mbele yao yalikuwa bado masaa mengi  sana kabla ya harusi kufanyika.
Kwa mwendo wa kinyonga kabisa gar lilifika mbele ya nyumba ya Eve majira ya saa nne usiku na hakuna aliyekuwa ameschoka sana.Shamrashamra zilikuwa kubwa sana maeneo ya pale kwa Eve kelele zilizidi alipofika Reshmail, na kama alivyoaahidi kweli alishuka yeye peke yake kutoka katika gari akifuatiwa na dereva,urembo wake utadhani alikuwa amepembwa tayari kuingia ukumbini.
“Shoga  tabia gain hiyo kupendeza kuliko bibi harusi?”aliuliza eve kiutani baada ya Reshmail kuingia katika chumba ambacho Eve alikuwa amehifadhiwa akiwa na wapambaji wake.
“Hebu acha utani wako,kila mara unadhani  tuko shuleni?mwone,”alijibu Reshmail,Eve akajiziba mdomo kwa aibu huku akiwatazama wapambaji wake waliokuwa wamejizuia kucheka lakini uvumulivu ukawashinda wakacheka kwa nguvu.
Chumba kile kikageuka kijiwa cha story kati ya Reshmail na Eve ,stori zingine zilikuwa juu ya mume wa Reshmail (Christian),shoga hadi pete?
“Sina utani mie mbona”?alijibu Resh huku wapambaji wakiwa hawajui hata kinachoongelewa.
“Mama kuna mtu anataka kukuona,ilikuwa ni sauti ya kike ikimueleza Eve.
“Heh!!ushazaa na wewe?”aliuliza kiutani Reshmail.Mh!!niringe huyu ni msaidizi wangu tu wa kazi anaitwa Bite,nampenda naye ananipenda pia.
“Sio kama mimi na Christian “alidakia Reshmail ambaye tangu aingie chumba kilitawaliwa na vicheko.
“Bite humuwezi huyu anaitwa mam Christian ni rafiki yangu tangu utotoni.
“Nafurahi kukufahamu mama Christian hata mimi.alitaka kuondelea kuongea Bite akakatishwa na Eve.”Anayetaka kuniona nani huyo tena?,mwambie nina mgeni Bite akajiondokea bila kumalizia kauli yake.
Sherehe ilifana kuanzi kanisani lakini mambo yote yalikuwa saa mbili usiku maharusi wadogo walipokuwa wametangulia mbele wakifuatiwa na wana ndoa wenyewe(Eveline na Benjamin)huku nyuma yao Reshmail na Fredrick wakifunika kila kitu kwa pale mbele Christian aliteka macho ya watu huku kamera zimemulika yeye. Tabasamu lake pana la wakati wote lililoonyesha vishimo katika mashavu yake yote  lilisababisha watu wengine wahisi huenda sio kutoka Tanzania , suti yake iliyoendana kabisa na mwili wake na viatu vyake  pia jinsi mkono wake ulivyokuwa umemshika kiustadi Loyce (bi harusi mdogo) ulimfanya MC ashindwe kukaa kimya “nani mwenyewe harusi,wa mbele,nyuma au kati” aliuliza kwa mbwembwe
“mbeleeeeeeeee!!!.......nyumaaaaa!!!!” ndio majibu yaliyosikika kutoka kwa wengi
“hayaa wageni waalikwa wanasema maharusi wa katikati wamefunika sana” alidanganya MC aliyefahamu wazi Christian na Reshmail wameteka macho ya watu wengi pengine kuliko maharusi wenyewe.
  Picha zilipigwa kwa wingi lakini Christian hakuonyesha wasiwasi wowote “mh!! Katoto kazuri halafu kajanja hako” wanawake walikuwa wakinon’gonezana huku wakimtazama Christian anavyozidi kusonga mbele
“wamekatoa nje,baba yake ni mreno” alidakia mama aliyesifika kwa umbea pale mtaani aliyejulikana zaidi kwa jina la mama mwingi.hata hawakuhangaika kujibishana nae kwani walishamzoea
   Taratibu kabisa kwa mwendo wa kunyata jozi hizi tatu za kuvutia ziligawanyika huku jozi mbili za wakubwa zikienda katika meza kubwa kabisa na watoto wakienda katika meza yao ndogo iliyokuwa akimeremeta soda na vinywaji vingine baridi,”kusema ukweli sherehe imependeza,siongei kama  MC bali kama ndugu Kidagaa Peter Kubalunga wengi wananiita MC K.P” alichombeza Msema Chochote (MC) na kushangiliwa sana na umati mkubwa uliohudhuria sherehe hiyo

**********      ************   ********
“dah!! Umependeza kweli sitaibiwa huko na wajanja,hebu ona ona mgongo wako utadhani huna mamba ulivyopendeza,ona kifua chako mpenzi wangu hapana nitaibiwa mke mie” Adam alikuwa akimtania Bite huku akim funga zipu yake ya mgongoni
“acha wivu mwanaume wewe,kaa ndani usubirie ya kwako aniibe nani wataishia kutamani tu!!” alijibu Bite huku akimun’gunya midomo yake ili lipstick aliyopakaa ikae vizuri zaidi na kioo kikiwa mbele yake
“nakupenda sana mke wangu,tambua hilo niliamua toka moyoni mwangu na wala sijutii hata kidogo najionamwenye bahati sana” Adam kwa sauti ya chini iliyomaanisha anachokisema alimwambia Bite ambaye alitulia tuli akamtazama Adam kisha akamkumbatia na kumbusu.
“nakupenda pia nakupenda sana” Bite akamwambia Adam halafu akatoka nje na kupanda teksi iliyokuwa inamsubiri kwa nje na kuondoka,Adam hakuthubutu kutoa hata pua yake nje kwani bado alikuwa na uoga wa kurejea mikononi mwa watu wabaya
Majira ya saa tatu na nusu Bite tayari alikuwa mlangoni akionyesha kadi yake ya mwaliko kwa watu wa ulinzi kisha mwanadada kutoka kamati ya maandalizi akamwongoza Bite kuelekea katika upande ambao ndugu zake na mwanamke walikuwa wamekaa,eneo la chini ya meza ya bwana na bibi harusi mdogo.Bite alikuwa tayari kama ndugu wa damu kwa Eveline walitokea kuheshimiana sana na hawakuwahi kuingia katika malumbano makubwa sana.
    Amani ilitoweka katika meza ya bwana na bibi harusi wadogo,Christian alikuwa amekosa utulivu mara kwa mara alikuwa ananyanyua shingo yake aweze kuona kitu Fulani ambacho hakuna aliyefahamu ni nini kimemsibu
“au kanaumwa tumbo?” alijiuliza matron huku akienda kwenye ile meza kumsikiliza Chriss ana shida gain
“Chriss ni nini baba umekuwaje?” alimuuliza baada ya kumfikia
“nataka kwenda kwa mama” alijibu kwa sauti iliyojaa manun’guniko sana
“subiri kidogo mtoto mzuri nitakupeleka sawa” matron alimdanganya Chriss huku akiamini shida yake ilikuwa kwenda kwa Reshmail,kidogo Chriss alitulia japo bado hakuwa na katika hali ya uchangamfu kama awali
  Muda wa kutoa zawadi ulipofika maharusi wote katika jozi tatu walitakiwa kuwa mbele ya umati kwa ajili ya kupokea zawadi zao.Christian na Loyce waliwekewa viti wakakaa wakati Eve,Benny,Reshmail na Fredrick walisimama wima kupokea heshima hizo
“he! We mtoto vipi? Jamani huyu mtoto kulikoni” yule mwanamke aliuliza  baada ya kushikwa gauni lake na Christian alipotaka kuondoka baaba ya kutoa zawadi. Bahati mbaya muziki ulikuwa umezimwa hivyo ukumbi mzima ulishuhudia tukio hili la kushangaza
“mamaaaa!!  Mamaaaa!!” Chriss alimpigia  kelele alipotaka kuondoka
“Chriss…….Christian……Christian wanguuuu!!! Jamani ni mwanangu..ni mwanangu huyu” alipiga kelele mwanamke huyu,alikuwa ni Bite na tayari akili yake imemgundu Christian,watu wote waliamini amechanganyikiwa lakini alikuwa anasisitiza bado kwa maneno hayohayo. Hakika mbele yake alikuwepo mwanaye waliyepotezana zaidi ya nusu mwaka sasa na dalili za kumpata zilikuwa zimeanza kufifia. Mayowe yake yalivyozidi yakapoteza usikivu pale ukumbini na kila mtu kuanza kujiuliza kulikoni eneo lile
“mama mama mama,huyu ni mwanangu…..Christian jamani” Bite kwa sauti ya juu sana akaanza kumwambia Eveline ambaye alikuwa amekodoa macho kuangalia anachofanya Bite pale mbele
“kuna nini jamani” Reshmail alishindwa kujiuliza akamvagaa Eve na kumuuliza
“huyu ni Christian,mtoto wangu jamani mtoto wangu kabisa” alisisitiza Bite. Nguvu zilimwisha Reshmail japokuwa hakuzimia lakini alianguka chini,alishuhudia kila kitu lakini hakuweza kuzungumza,ulikuwa mshtuko wa hali ya juu sana haikuwa sherehe tena bali kasheshe,huku Bite na mayowe yake huku Reshmail akiwa chini. Wapiga picha hawakuwa mbali walilichukua hili tukio kikamilifu tayari kwa kuuza katika vyombo vya habari.
   Mwanamama mwenye nguo nyeusi alikuwa anapambana kupenya katika msitu mkubwa wa watu pale ukumbini,mwanzoni hakuwemo kwenye sherehe “vimama vya Kiswahili navyo,hapo umbea tu ndo amefata humu,akipigwa hapo au akikanyagwa atamlalamikia nani” mwanaume mmoja aliyekuwa amevaa suti aliwaambia wenzake huku wakimtazama mama huyo mwenye baibui iliyovaliwa kwa staili ya ninja hasa hasa kwa waumini wa dini ya uislamu anavyopambana kwa juhudi ili apenye. Watu kwa huruma wakampisha,moja kwa moja akiwa anakimbia kwa kasi alifika mbele ya ukumbi akaanza kuzubaa na mara ghafla akakimbilia alipolala Reshmail na kuanza kutikisa
“huyu maza vipi mwehu nini? Yaani mtu ameachiwa hewa impige yeye anaenda kuweka usiku tena na manguo yake” kijana mmoja aliyekuwa amevaa jinsi kwa staili ya mlegezo aliwaambia wenzake
“tulia wewe huenda ni mamake huyo” alijibiwa na wenzake
“reshmail amka amka mpenzi” alimwambia kwa sauti ya chini.

                           ****                              **     ***
Wivu wa utani utani aliouonyesha mbele ya mke wake ulukuwa unatoka moyoni mwake,Adam alihisi huko nje labda kuna mjanja anamchukulia mke wake.”ngoja nikamfumanie mtu leo” alijiwazia Adam huku akipekua pekua nguo gani anaweza kuvaa iweze kumziba sura yake asiweze kufahamika kwa urahisi mbele za watu,’baibui’ ndio jibu alilopata,harakaharaka akajitanda kwa ustadi,alifahamu vyema pesa ya mkewe ilipokuwa inahifadhiwa akajichotea kiasi kilichotosheleza kwa nauli “Mountain view” alijikumbusha jina la hotel ambayo sherehe ilikua inafanyika,ni jina alilolikariri kwenye kadi ya mwaliko.
Akiwa na baibui lake alipanda teksi ikamfikisha moja kwa moja eneo la tukio,kukuru kakara aliyoikuta pale ilimtia hofu kubwa sana aliamini lazima kuna kitu kimeharibika eneo lile hakuwaza kitu kingine bali usalama wa mkewe (Bite) moja kwa moja naye alijichanganya humo ndani n
 Tofauti ya malengo yake ya kumjulia hali mkewe,macho yake yanakutana na Reshmail akiwa sakafuni na vazi lake zuri la harusi,sura yake bado ilikuwa haijasahaulika katika  kumbukumbu za Adam.
Nguvu zilizokuwa zimemwisha Resh pale chini zilirejea kwa kasi kutokana na kusikia sauti ya kiume kutoka katika nguo za kike “mamaaaaaaaaaaa!!!!” alipiga  kelele kwa sauti ya juu huku tayari akiwa amesimama wima akijaribu kukimbia,kamera zikageukia eneo lao tena nyingi zikimmulika mwanamke mwenye baibui (Adam). Kabla hajakimbia Reshmail alidakwa mkono wake.”Adaam……Adaaaam!!!” alipiga kelele kali zaidi wakati huuu Reshmail. Adam alikuwa amejivua baibui kwa upande wa usoni,akiwa hajapewa jibu lolote reshmail palepale alifika Bite,”Adam! Umefikaje hapa mume wangu…si ulisema hauji…” Bite aliuliza
“nini? Nani? Umemwitaje? Na huyu ni…….” Hakuweza kumaliziankauli yake wakati huu,mawazo yakauzidi nguvu ubongo wake akazimia palepale.Wakati huo Chriss alikuwa analia tu hgajui kinachoendelea,Eve na Benny walikuwa wanahaha huku na huko bila kukumbuka kwamba alikuwa na shera safi kabisa tena ya gharama za juu kabisa,Benny ndio alikuwa kama tahira hajui hata pa kuanzia alikuwa ameshtuka sana. Ilikuwa kama vita vile lakini hakuna hata aliyejeruhiwa wala aliyekuwa anapigana vilikuwa si vita vya risasi bali vita vya mapenzi. Wgeni waalikwa waligeuza tukio hilo kuwa kama filamu ya kusisimua lakini waliyokuwa wameianzia katikati bila kujua ilianzia wapi na inaenda wapi.,nani nyota wa filamu na nani adui.

                                            ***
Ni katika nyumba ya Eveline.Reshmail akiwa mbele ya Beti amepiga magoti akilia kwa uchungu
“Bite wewe ni mwanamke mwenzangu nionee huruma kwa haya niliyopitia,nimeteseka sana,nimedhalilishwa kwa ajili ya Adam,ni kwa ajili yake hadi leo mimi ni bikra,kwa ajili yake familia yake imetuchukia,kwa ajili ya Adam baba yangu haeshimiki tena mtaani kwetu,Bite sitamani mwanaume yeyote yule,ukininyan’ganya Adam na Christian mimi nitakufa Bite,ni furaha gani utaipata kwa kifo changu kwa ajili ya upendo?,sitajali huyu mtoto uliyezaa nae wala sitaumizwa na ujauzito wake uliombebea,ninakuomba Bite niache na mimi nipate furaha japo kidogo tu katika siku zangu zilizobaki hapa ulimwenguni,nisaidie niweze kurudisha upendo uliogeuka chuki kati ya familia yangu na Adam.Bite uamuzi upo mikononi mwako,ukikataa utaniumiza sana na nina uhakika nitakufa na pendo langu kwa Adam” Kilio kilimzuia kuendelea kuongea,lakini nay eye mgongoni mwake alilowanishwa kwa machozi ya Bite yaliyokuwa yanatililika muda wote wakati Reshmail anaongea,kwa hali halisi alimwonea huruma lakini pia kwa dhati kabisa aliwapenda Adam na Christian.Eve na mumewe Benny walikuwa watazamaji,wenyewe hawakuwa na uwezo wa kutoa maamuzi yoyote yale. Christian alikuwa ametulia kwenye kochi,hali ya utulivu aliyokuwa nayo ilipita siku zote.
“Adam tulipokutana unapajua,yote tuliyofanya unayajua,upendo wangu kwako nadhani unautambua pia……labda sikupangwa kuwa wako milele ndio maana aliyepangwa amejitokeza wakati muafaka,asante kwa zawadi ya penzi lako,asante kwa mtoto na huu ujauzito hii ni heshima kubwa kwako milele,neno gumu ninaloweza kulisema sasa ni kuwa kwa moyo mmoja nakuruhusu uendelee na Reshmail,nayasema haya mbele ya mama yanngu Eveline” alizungumza Bite kisha akashindwa kujizuia kuangua kilio kikuu kilichoamsha hisia za kila mtu pale ndani wote wakadondosha machozi yao. Adam,Reshmail na Bite wote kwa pamoja wakakumbatiana huku machozi yao yakitua juu ya Christian aliyekuwa ktikati yao,ilikuwa ni picha ya kusisimua na kuumiza sana.

******               *****
Kilikuwa kikao kikubwa cha familia yao Reshmail,watu wote muhimu walikuwemo jasoro mama wa familia hiyo aliyesusia kikao,mzee Manyama,Reshmail,Eve,Benny,Bite,na Paskalina walikamilisha kikao hichi,Christian alikuwa bustanini akibembea.Reshmail alikuwa anatoa siri nzito nzito za kushangaza ambazo kwa namna kubwa kabisa zilitoa taswira ya mambo yaliyokuwa yamefichika kwa muda mrefu,uhusiano wa kimapenzi kati yake na mama yake mzazi ulimwacha kila mtu mdomo wazi,Reshmail aliomba msamaha kwa hilo na alieleweka na kusamehewa. Ni katika usimuliaji wa upande wa Bite kuhusu ngome ya vigogo iliyoleta fikra za mazingira ya kupotea kwa kadi yake ya benki katika mazingira ya utata mkubwa,Benny hakuongea neno kwani yeye alikuwa kama mgeni tu katika mkutano huo.Mzee Manyama alikuwa kimya akimtafakari mkewe kwa maovu aliyoifanyia familia yake,kwa mateso aliyompa Adam na kwa uvunjifu wa amani aliouleta baina ya familia hizi mbili,kwa fedheha aliyomletea na kumvunjia heshima yake bungeni na hata mtaani,akiwa mwingi wa hasira alisimama bila kuaga na kuelekea chumbani,kwa hali aliyokuwa nayo Reshmail aliamua kumfata kwa nyuma ili asije kufanya jambo baya huko anapoenda,hasira yake ilipokelewa na na mwili wa mkewe ukiwa sakafuni,tayari alikuwa maiti. “ulistahili hukumu hii” bila kushtuka alisema mzee Manyama huku akimpisha Reshmail aingie humo ndani.

***           *******                           *****
Mapema baada ya mazishi ya mama yake mzazi Reshmail akiongozana na Adam katika gari ya baba yake,dereva akiwa Adam walifunga safari ya kwenda Mwanza kwa wazazi wake (Adam).
“utabaki ndani ya gari nitatangulia mimi najua watakuwa wakali hao lakini wakikuona ndipo mzizi wa fitna utakapokuwa umekatwa” Reshmail alimpa maelekezo Adam ambaye alikubali kwa ishara ya kutikisa kichwa.
Gari ilipaki nje kidogo ya nyumba ya kina Adam,kama walivyoelewana akashuka Reshmail akiwa amependeza sana,akaifunga gari kwa kutumia rimoti aliyoshuka nayo na kwa mwendo wa kunyata akaanza kuusogelea mlango akausukuma akaingia ndani,kupitia kwenye kioo Adm lishuhudi Reshmail akitoweka machoni pake.
“umefata nini hapa we mchawi Adam hajakutosha unamtaka na Rosemary ngoja sasa….Rose!!!!” aliita mama Adam,Reshmail akiwa anatabasamu kwani alijua ni muda mfupi wote watakuwa na furaha kubwa. Akiwa bado hajaanza kuongea alishuhudia mama Adam akimfuata na kisu huku Rosemary akifika pale na mwiko mkubwa,wakati huu akili yake ilifanya kazi haraka akaanza kukimbia lakini nguo yake ndefu ilimsaliti baada ya kunasa kwenye geti la kutokea nje.
Kwa macho yake mawili Adam alishuhudia Reshmail akiwa chini huku watu wawili wakimshambulia kwa fujo,alijaribu kufungua mlango lakini ulikuwa umewekwa ‘loki’ sauti yake haikuweza kusikika nje alipigapiga vioo vya gari lakini hakuna aliyemsikia. Alishuhudia damu nyingi sana ikiruka juu. Kwa akili ya haraka haraka akakumbuka kushusha kioo akatokea dirishani
“mamaaaaaaaaaaaaaaa!!!” Adam akaita kwa nguvu palepale mama yake akageuka na kudondosha kisu alichokuwa nacho,”Adam mwanangu ni wewe!!!” alisema mama Reshmail huku aimfuata Adam ambaye hakumjali bali alifika alipokuwa Reshmail “Reshmail,Reshmail”  “ mama na dada mmemuua mke wangu jamani mamaaaa!!” alilia Adam baada yakuona hajibiwi kitu.”A.d….am!!  ninaku….fa  mume wangu….ninakufa  kwa furaha…..ni..meku..rudish…sha kwenu…naku…panda..sana” Reshmail aliongea kwa kujiumauma huku akivuja damu,raia wengine walikuwa katika harakati za kutafuta msaada lakini msaada mkubwa uliopatikana ni wa polisi waliowatia nguvuni mama Adam na mwanae Rosemary huku roho ya Reshmail ikimaliza muda wake palepale Igoma jijini Mwanza.kama usingekuwa ujasiri wa Adam basi tukio lile lingegharimu maisha yake,tayari mama mkwe amepotea,na sasa mpenzi wake Reshmail,mama na mdogo wake wakitupwa jela kwa kesi ya mauaji.
****    **** ****    *****
“mapenzi yamenipotezea muda wangu nimekuwa mfungwa miaka mitano,mapenzi yameivunja vunja familia yangu,mwanamke niliyempenda ametoweka tayari tena mbele ya macho yangu,ni heri niisome hii sheria vizuri zaidi ili ikiwezekana siku moja niwatetee ndugu zangu walioko gerezani hao pekee ndio furaha yangu,kamwe siwezi kuhangaika tena na watoto wa hapa chuoni hata siku moja sidhani kama wana maana sana kwangu nikithubutu tena huend yatakuwa makubwa zaidi ya awali,usiku mwema Mosenya.” Alimaliza simulizi yake Adam,wote tulikuwa tunatokwa machozi ya uchungu,lakini lengo langu likatimia na swali la muda mrefu likapata jawabu baada ya simulizi hii kuanza kuandikwa katika gazeti la chuo.


 
Hadithi ya Joka Jeupe 
 
Katika enzi za kale, kwenye Mlima wa Emi kulikuwa na majoka mawili yenye umri wa miaka elfu moja, moja jeupe, moja jeusi. Majoka hayo mawili yalipenda sana mandhari ya watu wanapoishi, basi yalijibadilisha kuwa wasichana wawili warembo, moja lilijipa jina la Bai Suzhen jingine liliitwa Xiao Qing. Siku moja walifika kwenye sehemu maarufu yenye mandhari nzuri, ziwa la Xihu mjini Hangzhou.
Mandhari ya ziwa la Xihu kweli ilivutia sana, walipofika kwenye daraja moja la ziwa hilo ghafla mvua ilianza kunyesha, wakakimbia mvua na kujificha chini ya mti mmoja mkubwa. Wakati huo alikuja kijana mmoja mwenye mwamvuli aliyeitwa Xuxian, ambaye alikuwa akirudi nyumbani baada ya kusafisha makaburi. Alipoona wasichana chini ya mti aliwasaidia kwa mwamvuli wake na baadaye aliwasaidia kuwapeleka nyumbani kwa mashua. Bai Suzhen alianza kumpenda kijana huyo, alipoagana na kijana huyo alimwambia kesho aje kuchukua mwamvuli wake.
Siku ya pili kijana Xuxian alifika nyumbani kwa Bai Suzhen karibu na ziwa kuchukua mwamvuli wake. Bai Suzhen alimshukuru sana na kumwuliza habari za familia yake, akafahamu kuwa alifiwa na wazazi wake mapema tokea alipokuwa mtoto na sasa anaishi kwa dada yake na kufanya kazi katika duka moja la dawa. Msichana Bai Suzhen aliomwomba aolewe naye. Hakika Xu Xian alikuwa na furaha isiyo kifani. Kwa kuongozwa na Xiao Qing walifanya sherehe ya ndoa. Baada ya ndoa walianzisha duka la dawa. Bai Suzhen alifahamu matibabu, kila siku aliwatibu wagonjwa wengi.
  Kulikuwa na sufii mmoja wa dini ya Buddha aliyekuwa anaitwa Fa Hai. Fa Hai alikuwa anajua siri ya Bai Suzhen kuwa alikuwa joka mwenye miaka elfu moja, na hakika angewadhuru watu, hivyo alidhamiria kumwokoa kijana Xu Xian.
Siku moja Fa Hai alikuja nyumbani kwa Xu Xian, alimwambia, mkewe ni zimwi. Xu Xian hakuamini. Basi Fa Hai alimwambia, kama haamini, ajaribu kumshawishi anywe pombe tarehe 5 Mei, siku ya mashindano ya mbio za mashua, na kama akinywa atarudia asili yake.
Tarehe 5 Mei ilifika, kila familia hunywa pombe kusherehekea siku hiyo. Majoka yanaogopa pombe, Bai Suzhen alitaka kwenda mlimani kukwepa, lakini alikuwa na wasiwasi kuwa mumewe Xu Xian atamshuku, alikuwa hana budi ila kubaki nyumbani akijidai anaumwa.
Ingawa Xu Xian hakuamini aliyoambiwa na sufii Fa Hai, lakini kila mmoja katika siku hiyo hunywa pombe, hivyo alimshawishi mkewe anywe pia. Mkewe Bai Suzhen alishindwa kukataa, alikunywa glasi moja, mara akaanza kuona kizunguzungu. Xu Xian alimsaidia hadi kitandani, kisha akaenda jikoni kumtengenezea supu ya kuondoa ulevi. Akaja na bakuli moja la supu kitandani, alipofungua chandarua akaona joka kubwa jeupe limelala kitandani, Xu Xian alikufa kwa mshtuko.
Joka jeupe lilipozinduka likaona mumewe amekufa kwa mshtuko, alihuzunika sana, alimwomba Xiao Qing amtunze mumewe, na yeye akatoka haraka na kwenda kwenye mlima mmoja ulioitwa Xianshan ambako kulikuwa na aina moja ya jani la dawa ambalo lingeweza kumwokoa mumewe.
Wakati huo Bai Suzhen alikuwa amepata mimba ya miezi saba. Alipofika mlima Xianshan watoto waliokuwa wananlinda mlima walipojua kuwa anataka kuiba jani la ajabu walipambana naye. Mungu wa mlima huo alipoona jinsi Bai Suzhen alivyohangaika kumwokoa mumewe alimpa jani la ajabu.
Xu Xian alifufuka, lakini bado alikuwa ameshikwa na hofu. Bai Suzhen alipatia mzungu wa kumdanganya, alitumia kitambaa kirefu cheupe na kukigeuza kuwa joka kuzunguka kwenye boriti la dari na kumwita mumewe aone. Kwa kuona joka hilo, Xu Xian aliondoa mashaka yake juu ya mkewe, na waliendelea kuishi kwa mapenzi.
Sufii Fa Hai hakukufa moyo. Siku moja alimdanganya Xu Xian kwenda kwenye hekalu lake na kumzuia asirudi nyumbani. Baadaye mkewe na Xiao Qing walikuwa kwenye hekalu wakitaka kumrudisha nyumbani, wakagombana na sufii. Wakati walipopurukushana, Bai Suzhen alisikia maumivu ya uja uzito, kwa haraka alirudi nyumbani na Xiao Qing, alipofika kwenye daraja alikumbuka jinsi alipokutana na mumewe na kuanza na mapenzi, alihuzunika sana. Xiao Qing alimlaumu Xu Xian kwa kumsikiliza sufii, alimshawishi Bai Suzhen amwache mumewe.
Kwa kusaidiwa na sufii wengine, Xu Xian alitoroka kutoka hekalu na kwenye daraja alimpata mkewe. Mkewe alimwambia ukweli wa mambo, kwamba kweli alikuwa joka. Wakati huo Xu Xian alikuwa ameelewa kwamba mapenzi ya mkewe ni ya kweli na makubwa, akamwahidi kuwa hatajali akiwa ni kitu gani, lakini ataishi naye mpaka kufa.
Baada ya kurudi nyumbani, muda mchache baadaye Bai Suzhen alizaa mtoto. Katika siku ya kutimiza mwezi mzima kwa mtoto walifurahi sana, lakini wakati huo sufii Fa Hai alikuja tena nyumbani, alimkamata Bai Suzhen na kumtia chini ya mnara wa Leifong kando ya ziwa la Xihu.
Xiao Qing alitorokea mlimani Emei, alijitahidi kuinua uhodari wake wa mapambano, mwishowe alimshinda Fa Hai, na alimwokoa Bai Suzhen.



 

 SIMULIZI YA KWELI YA KUSISIMUA NA KUSIKITISHA YA MTOTO JANETH : 



Kengele ya kutoka darasani iligongwa, wanafunzi wa shule ya msingi wakaanza kutoka madarasani huku wakifukuzana wengine wakipiga kelele ilimradi shwangwe tu.

Ilikuwa mara yangu ya kwanza kufundisha shule za hatua hiyo.

Ilikuwa ni shule ya serikali.

Jicho langu liliangukia katika sura ya msichana mdogo, nguo zake chafu. Alikuwa analia.

Alikuwa peke yake na hakuwa na yeyote wa kumbembeleza.

Mimi kama mwalimu sikutaka kujisogeza karibu naye sana. Kwanza nilikuwa mgeni.

Nikaachana naye.

Siku iliyofuata tukio kama lile likajirudia. Msichana yuleyule wakati ule uleule wa kutawanyika, alikuwa analia sana. Mwishowe aliondoka huku akiwa analia.

“Mbona mwenzenu analia?” nilimuuliza mwanafunzi mmoja.

“Huyo ni mama kulialia..” alinijibu huku anacheka.

Haikuniingia akilini hata kidogo kuwa yule binti analia bila sababu.

Siku ya tatu nikaanza kujiweka karibu naye.

Muda wa mapumziko nilimwita nikamnunulia chai, alikuwa ananiogopa na hakutaka kuniangalia machoni.

Sikumuuliza lolote juu ya tabia yake ya kulia lia kila anaporuhusiwa kurejea nyumbani.

Hata siku hiyo pia alilia vilevile. Wenzake wakawa wanamzomea.

Akili yangu iligoma kuamini kuwa binti yule analia bila sababu.

Kwanini alie wakati wa kutawanyika tu?? Hapana si bure.

Nikaendelea kujiweka karibu naye. Mkuu wa shule akafikishiwa taarifa kuwa nina mahusiano ya kimapenzi na yule mtoto.

Moyo wangu na Mungu pekee ndio walikuwa mashahidi. Nilikosa cha kujibu.

Nilijaribu kujiweka mbali naye lakini moyo ulinambia kuwa kuna jambo natakiwa kulijua.

Nikaendelea kuwa karibu naye. Hatimaye mkuu wa shule akanisimamisha kufundisha pale kwa tabia yangu ya kufanya mapenzi na mwanafunzi.

Nilijitetea lakini sikueleweka. Nikamwachia Mungu……

Licha ya kusimamishwa kazi, niliendelea kufuatilia nyendo za yule binti aliyeitwa Janeth.

Kila alipotoka shule nilimvizia njiani na kumnunulia chakula, kisha tunazungumza kidogo.

Aliponiamini kama kaka yake ndipo nikajieleza dukuduku langu.

“Janeth…” nilimuita.

“Bee kaka ….” Aliitika huku akinitazama.

“Nyumbani unaishi na wazazi.”

“Ndio naishi na mama..baba huwa anasafiri safari.”

“Mama yako ana watoto wangapi?”

“Mama yangu alikufa….alikufa nikiwa mdogo hata simkumbuki” Alijibu kwa sauti ya chini.

“Kwa hiyo unaishi na mama mdogo.”

“Ndio.”

“Unampenda mama mdogo?”

Swali hili likaikatisha furaha ya Janeth. Akaanza kulia, alilia bila kukoma, Janeth alilia kwa uchungu hadi nikajisikia vibaya. Nilimbembeleza kisha sikumuuliza tena.

Siku zikaenda bila kumuuliza chochote..

Baada ya siku kumi, ilikuwa siku ya michezo pale shuleni, hivyo hapakuwa na masomo.

Janeth alichelewa kuja shule, nilimngoja uwanjani, hadi alipofika majira ya saa nne.

Nikamwambia twende kunywa chai.

Siku hiyo nilimpeleka mbali kidogo, tukanywa chai, kisha tukakaa mahali palipokuwa wazi.

Nikaleta tena mjadala mezani.

Ni kuhusu maisha ya Janeth.

Alikataa kabisa kusema lolote, nilimshawishi sana.

“Usiogope mimi ni kaka yako.” Nilimpooza.

Janeth badala ya kusimulia akaanza kulia tena.

“Ataniua mama nikisemaaaa” alilalamika.

Nikambembeleza hatimaye akanieleza jinsi anavyonyanyaswa na mama yake.

“Mama hanipendi hata kidogo, ananipiga na kuninyima chakula, hapendi nije shule, vyombo tunavyotumia usiku hataki nivioshe usiku na hataki niwahi kuamka asubuhi, nikiamka natakiwa kufanya kazi zote, kufagia uwanja, kudeki nyumba, kuosha vyombo kisha ndipo nije shule. Baba akiwepo anajidai kunijali sana…”

Alijieleza.

“Ni hayo tu Janeth….niambie kila kitu.”

“Akijua ananiua alisema….”

“Kwani amewahi kukutesa vipi..”

Ni hapa Janeth alivyozungumza huku analia kilio ambacho hakitatoka masikioni mwangu kamwe.

Siku moja, alichelewa kuamka, ilikuwa siku ya mapumziko.

Mama yake alipomwamsha, aliitika na kupitiwa usingizi tena.

Mama aliporejea mara ya pili, alikuwa na mti mkavu, alimpiga nao kichwani na popote pale katika mwili, alipoona hiyo haitoshi akamvua nguo, akausokomeza katika sehemu za siri, aliuigiza hovyohovyo, ukuni huo ulikuwa wa moto.

Yeyote mwenye moyo wa nyama ajifikirie ukuni wa moto ukazamishwa sehemu za siri za mtoto wa darasa la sita.

Nilitokwa machozi.

Nikawahi kujifuta hakuona.

“Baba yeye alisemaje….”

“Baba ni mkali na hapendi kunisikiliza na mama aliniambia nikiambia mtu ananiua mara moja.” Alijibu kwa huzuni.

“Nikija na dada yangu tunaweza kukuona ulivyounguzwa..”

“Ndio…” alinijibu.

Sikutaka kulaza damu nikampigia simu rafiki yangu wa kike.

Nikamuuliza kama yupo kwake, alikuwepo.

Nikaongozana na Janeth.

Tukafika, Janeth akatoa nguo zote.

Ilihitaji moyo wa kiuaji sana kutazama mwili wa Janeth mara mbilimbili.

Alitisha, hakika alikuwa ameunguzwa vibaya na vidonda vilikuwa havijapona vizuri.

Dada yule alishindwa kujizuia alimlazimisha Janeth twende kwa mama yake amkabiri na kumpa kipigo. Nikamzuia.

Hata mimi nilikuwa na hasira kali. Lakini sikutaka kuiruhusu ifanye kazi.

Nikachukua kamera, nikampiga picha Janeth katika yale makovu.

Mbio mbio nikaenda polisi, kituo cha haki za watoto nikaelezea mkasa ule huku nikishindwa kujizuia machozi.

Nikawaonyesha na picha.

Tukaongozana nao hadi nyumbani kwao Janeth.

Mama yule akakamatwa bila kutarajia.

Nilitamani kumrukia nimng’ate lakini haikuruhusiwa.

Sheria ikafuata mkondo. Janeth akaanza kupokea tiba.

Yule mama akahukumiwa kwenda jela miaka sita..hadi sasa yupo jela.

Mume wake alitozwa faini kubwa kwa kosa la kutofuatilia maendeleo ya mtoto wake kiafya……..

Mimi nilirudishwa kazini, kwa heshima kubwa. Heshima ya nkumkomboa mtoto.

***Akina JANETH wapo mtaani kwako…..usiwaangalie na kuwaacha tu…hebu jaribu KUWA SAUTI YAO….hawawezi kusema…hebu sema badala yao…….wanalia kisikie kilio chao…….


KAMA UMEGUSWA NA MKASA HUU SHARE NA NDUGU JAMAA NA 
MARAFIKI ZAKO ILI WAONE 


KISA CHA KAHABA
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Kesi-ya-kukutwa-na-sare-za-polisi-yaahirishwa/-/1597296/2243412/-/xlg066/-/index.html


Nilikua mwajiriwa katika kampuni moja maarufu jijini dare s salaam , katika kuajiriwa kwangu huko nikawa msaidizi maalumu wa bosi wa kampuni ile , basi siku moja moja nilikuwa naenda kujirusha na bosi wangu .

Ukizingatia kwamba sikuwa na mume wala mchumba na kwa kweli huyu bosi ndio alikuwa mtu wa kwanza kufanya nae tendo la ndoa , hivyo nilifurahia mhemko wake na jinsi alivyokuwa ananipenda na kunijali kila kitu nilipata na zaidi .

Alifanya yote haya bila kunificha kwamba ana mke na watoto nyumbani kwake kwahiyo wakati mwingine chochote kinaweza kutokea nijiandae kwa shuguli hiyo pevu kama mke wake akishitukia dili hilo .

Tulikuwa na uhusiano na huyu bosi kwa miezi 4 hivi mpaka siku moja katika tembea tembea mitaani nikakutana na kijana mmoja mtanashati akanieleza kwamba ananipenda na kunizimia sana yaani ameshanifia

Huyu kijana alihangaika kwa mwezi mzima mpaka siku nikaja kumkubalia akawa ndio mpenzii wangu halali sasa , nilimwamini sana nay eye aliniamini sana , miezi 3 tokea kujuana na huyu kijana aliniambia kuhusu kufanya nae tendo la ndoa .

Nilifikiria sana wakati mwingine nilitaka kulia jinsi alivyokuwa ananishika na kuniomba tendo la ndoa akiwa chumbani kwangu , alijaribu kunishika sehemu kadhaa akanivua nguo nami nilimtolea nje nilimkatalia .

Basi siku moja nikamwomba tukaangalie afya zetu , kijana wa watu alikasirika sana wiki nzima hakufika nyumbani kwangu wala kunipigia simu , kumbe alitaka tufanye tendo la ndoa bila kinga ? sasa ningejuaje kuhusu afya yake ? au ananiamini nini mimi ?

Maisha yaliendelea na mambo mengine yaliendelea tu wiki ya 3 alinipigia simu akaniomba msamaha turudiane na alikubali kwenda na mimi kupata vipimo vya afya zetu kujua kwanza kabla hatujaanza mambo mengine yoyote yale .

Basi ndio hivyo majibu yaliyoka mazuri , ndio mapenzi yetu alikuwa zaidi na penzi nilimpa bila hiyana wala aibu yoyote , yeye mwenyewe alifurahia mambo yangu na kwanza alikuwa anatoroka nyumbani kwao kuja kulala kwangu wakati mwingine mwezi mzima .

Tuliendelea kwa miezi kadha na huyu kijana huku na mimi nikiwa na bosi wangu kule kazini , basi bwana siku moja , sisi officini tulitakiwa kwenda kutoa damu hospitali ya muhimbili katika maadhimisho ya siku ya afya duniani . Watu walipimwa afya zao na mimi nilipimwa , majibu yangu yalikuwa ya kutatanisha sikuamini macho yangu wala masikio yangu , nilienda hospitali ingine napo majibu yalikuwa yale yale kwamba nimeadhirika na UKIMWI .

Haya majibu yalimfikia mpaka bosi wangu nae akatambua hilo akasikitika sana nay eye alivyoenda kupimwa akakutwa hajaadhirika , basi nikajua moja kwa moja ukimwi nimepata kutoka kwa yule kijana wa mitaani na sio mtu mwingine .

Nikamwomba huyu kijana tukaangalie afya zetu kwa mara ingine tena hospitali , tukaenda kule kupima afya zetu , yeye ndio alikuwa wa kwanza kupokea majibu yake , alikutwa ameadhirika akupata mshituko wa ghafla yaani haamini .

Mshituko huo ulimpelekea aanguke chini na kuzimia watu walienda kumbeba na kumpeleka hospitali kupatiwa huduma ya kwanza basi hapo ndio magonjwa mengine yalianza kujitokeza na kujulikana sana .

Kumbe huyu kijana alikuwa na urafiki wa kimapenzi na shugamami mmoja mtaa wa pili huyu shuga mami mume wake alifariki dunia miaka 5 iliyopita kwa UKIMWI watu wanaema TB sijui , ndio huyu kijana kuona zile pesa za shuga mamy akaenda kwake .

Kijana aliumwa kwa miezi 3 hivi kisha akafariki dunia akaniacha duniani mwenyewe , kule kazini nilifukuzwa kaza na bosi wangu kisa nilitaka kumwambukiza ugonjwa wa ukimwi , lakini siku moja alinipigia simu kunieleza kwamba mke wake ameadhirika na UKIMWI pia lakini yeye anasema hajaadhirika .

Hapo ndio nilishangaa sana , kwanini mke wa aadhirike yeye asiadhirike au mke wake nae alikuwa anatoka nje ya ndoa bila mume wake kujua ? basi hiyo ni siri yao nyumbani kwao mimi hayanihusu .

Lakini ndio hivyo nilikuwa nimeshaadhirika na UKIMWI kazi nimeshafukuzwa sina cha kufanya wala kutafakari nilifikiria zaidi kuhusu ugonjwa wangu wa UKIMWI na jinsi nitakavyoweza kuishi maisha marefu kwa matumaini .

KAHABA

Baada ya kuona maisha magumu na sina lolote la kufanya mimi kama mwanamke mrembo na mwenye mvuto niliamua kutafuta njia rahisi zaidi ya kujipatia kipitano nilifikiria njia nyingi sana ambazo zingeweza kunipatia angalau mlo na mavazi katika siku zangu za maisha zilizobakia baada ya kugundulika nina virusi vya ukimwi

Nikaanza kutafuta sehemu ambazo naweza kuuza mwili wangu kwa pesa za chapchap niweze kuendeleza maisha yangu ya kila siku , nilikuwa na ramani yangu kwanza pale OHIO , JOLLY , MACHENI , BILLS NA LATAVERNA hizo ni sehemu 5 kuu za starehe jijini dare s salaam kwahiyo huko naweza kufanya kazi za kujiuza kwa wiki nzima kila siku bila kuchoka .

Ohio ilikuwa nzuri ila tatizo lake ni kwamba kila anayepita pale anakujua halafu unatakiwa uonyeshe maungo yako hazarani mimi sikuzoea tabia hizo na sikuwa na mhemko huo kwahiyo nilivaa miwani yangu na kuacha mapaja nje tu waangalie wenyewe kama wanapenda watakuja . Kule macheni tatizo lake ni mashoga wengi sana , yaani mwanaume anaweza akaja kutafuta Malaya akakuchanganya wewe ni shoga , wale mashoga wanaojiuza hawana tofauti na sisi wanawake tunaojiuza wakati Fulani ulitokea ugomvi mkubwa watu waliamulia tulimgombea mwanaume .

Billa nako kuzuri ila vijana wengi sana halafu hawana pesa , na vitoto vidogo vingi , nilikuwa naogopa matatizo na vijana wa kule sikupenda kufanya mchezo na watoto wadogo waliokuwa wananitaka hata kwa dau gani nilingoja wanaume wenye pesa zao tu sio zaidi .

Basi nilianza safari za kuelekea jolly club kwa ajili ya kujiuza mwili wangu nipate angalau chochote cha kula na kufanya katika maisha yangu , pale jolly club nilikutana na dada mmoja anaitwa Aisha , huyu dada nae ni kahaba mzoefu akaanza kunionyesha mambo kadhaa wa kadha kuhusu biashara ya ukahaba na kadhalika . Hapa ndio nilijufunza kwamba sio makahaba wote ni masikini au hawajiwezi kuna wengine wanajiweza na wanazo fedha ila wanapenda kufanya ukahaba yaani wamechoka na dunia wengine walikuwa na wanaume wao wakaachika wakaamua kuja huku kwenda na mwanaume wowote yule anayekuja .

Wengine wana matatizo katika ndoa zao kupigwa na kadhalika wanaamua kuja huku kujiuza au kukaa huku ili kuepuka matatizo katika ndoa zao au mahusiano yao , wengine ndio kama hivyo waume zao hawana nguvu za kutosha kufanya nao tendo la ndoa wanaamua kuwa makahaba kila mtu na lake na mambo yake pia .

Wengine wanafanya huu ukabaha kwa ajili ya kupeleleza yaani ni wapelelezi wa polisi au watu Fulani katika serikali wako katika mitaa hii kuzuga tu , ili wafanikishe kazi zao za uchunguzi kama polisi wa usalama sehemu walizoko .

Mwisho wa yote siku hizi kuna vita kubwa katika biashara hii ya ukabaha mjini dare s salaam , mfano kule jolly kuna wazungu na wahindi wanakuja kufanya biashara ya ukahaba kwahiyo wewe mwamfrika unakazi ngumu kuwapita wale wazungu na wahindi au wachina .

Siku hizi wanaume wengi wanapenda kitu kinaitwa JICHO yaani kufanya mapenzi kinyume na maumbile , hii nayo ni soko kuu , mfano mwingine anaweza kuja kwako anataka jicho na wewe hutoi jicho maana yake unakosa soko suluhicho ni kujitoa mhanga na kufanya mapenzi kwa kuwa mteja ni mfalme .

Mbaya zaidi kuna wanaume wengine wanakuja wanaweza kukuchukua uende nao kufanya ngono kumbe wanakupiga filamu za ngono wakati unafanya kitendo hicho haswa wazungu wengine wanakupa ufanye mapenzi na mbwa wao au wanyama wao wengine mambo yanaenda hivyo .

Biashata hii ya ukahaba ilinichanganyia sana kwa miaka 2 niliyoifanya na kwa kweli hakuna aliyenijua kama nimeadhirika na ugonjwa wa ukimwi nilikuwa najitunza na kutuza siri zangu hizi kuu na sikupenda kuzoeana na watu sana hadi waniulize hivyo

Siwezi kuhesabu ni watu wangapi nimefanya nao ngono lakini ni zaidi ya 300 siku zingine nafanya kazi na watu zaidi ya 3 kwa siku moja kwahiyo mambo yanaendelea halafu wengi hawakupenda kutumia mipira ya kiume yaani kondo walipenda kuja hivi hivi tu bila kinga chochote kile

Na mimi nilikuwa nimeshaadhirika nilichokuwa natafuta ni fedha za kuendeleza maisha yangu kwahiyo hata kama nikifanya ngono zembe bila kinga mimi hainiumi sana kwa kuwwa nilishajua hali yangu sikuweza kuitengua siku wa chochote cha kufanya zaidi ya hichi .

Hii ilikuwa ni kulipiza kisasi kwa maasi ambayo yule kijana alinifanyia kuniambukiza UKIMWI kwa makusudi huku akijua kabisa ameadhirika siku nyingi ,kwakuwa yeye ameamua kuniuwa mimi basi na mimi nauwa wengi zaidi na sijali kuhusu dhambi hizi nilizozifanya na sijutii kabisa .

MAISHA YA MTAANI

Huku mitaani waliniita majina kama JLo wakati mwingine salma hayek yaani wale waigizaji maarufu duniani kwa urembo nilio nao na mvuto wake , hakuna hata mmoja aliyekuwa na mawazo kama nimeadhirika au la kwa maana yule kijana niliyekuwa nae kama mpenzi alikufa kifo cha ghafla watu walisema amekufa kwa pressure .

Mitaani napo nilikamua kinoma , waume za watu walikuja mpaka mlangoni kwangu na magari yao , wananipakia na kunipeleka katika kumbi za starehe na sehemu nyingine nyingi sana wengine walinihonga mali na mambo kibao kisa wamenipenda wanataka ngono

Na kwa uhakika hawa wanaume niliwapanga sawia kabisa na hakuna aliyeweza kutambua mimi nina wanaume wangapi na wanaishi wapi wengi walijua ni washirika wangu katika kazi zangu na mambo yangu mengine kwanza sikupenda kuongea na mwanaume wowote chumbani kwangu wote nilikuwa nawaambia tukutane mbali kidogo na nyumbani haswa kati katika ya jiji .

Katika hawa wateja wangu kulikuwa na kijana mmoja anayeitwa juma huyu juma alikuwa na rafiki yake mmoja anayeitwa Shy , kijana mwembamba mwenye umbo la wastani , hana ndevu halafu ni mcheshi sana , alifanikiwa kuiteka moyo wangu , sasa nilitaka kumwambia mara kibao kwamba nimemzimia

Tatizo ni kwamba anayekuja kunichukuwa pale ni juma , juma huja pale kwa kusindikizwa na Shy , basi juma akanitambulisha katika website moja inayoitwa darhotwire www.darhotwire.com , nyumbani nikienda kupumzika nilipenda kushinda katika tovuti hii kuchat na marafiki na watu wengine .

Huyu shy nae nilimkuta katika site hii usiku wa manane anachat na jamaa zake , ila siku moja nilikutana na kijana mwingine anayeitwa politeman , huyu ndio alinichanganya kabisa , kwanza jina lake na jinsi aliyokuwa anaongea kweli nilizimia mwenyewe bado nikawa na siri kubwa moyoni je hivi tukifanya ngono inakuwaje ?

Maisha yaliendelea tu , basi nikimpenda politeman , huyu kijana akawa anakuja mpaka nyumbani kwangu wakati mwingine na huwa nampa computer yangu aitumie tukaenda zaidi nilimshitukia kumbe huyu polite ana urafiki wa kimapenzi na dada mwingine anayeitwa salma siku moja walipanga kwenda kufanya mapenzi lakini polite akakataa ?

Sikuamini macho yangu wala masikio siku nyingi kama naota kumbe polite alikuwa na urafiki na dada mmoja anaitwa Maria Chipz ?? Sikuamini , nilimuheshimu sana maria na sikutegemea kama anaweza kufanya hivyo hata siku moja , muda ukaenda kumbe kuna dada mwingine anaitwa REHEMA naye alikuwa anampenda Politeman Miss upanga Naye anampenda Politeman we acha tu

Nikamwaga chini sikupenda tabia zake za kitoto kitoto anazowafanyia hao kina dada wengine ingawa nilifanya nae mapenzi kama mara 4 hivi na mara zote hatukutumia kinga na nilikuwa nimeadhirika ila ni siri yangu , polite hajui na wengine wote hawajui lakini ndio maisha hayo

Haya ndio hivyo , nami sasa hivi nakaribia kufariki dunia niko zangu kitandani hapa hospitali ya Amana mkoani dar es salaam , kweli maisha ni safari ishi upendavyo na sio watakavyo , mwisho wa yote dunia sio hadaa wala dunia haikuchukii au haitaki kukufanyia chochote kibaya

Bali watu ndio hadaa , hata kama ni ndugu yako rafiki yako , hakikisha humpi nafasi akutawale aweze kukumiliki wewe na kukuamrisha chochote kile anachotaka yeye , kama ukifanya hivyo ndio utaishia kubaya kama mimi

Bosi wangu alinimiliki sana nikampa penzi , kijana wa mitaani nae alinimiliki mpaka sasa nimeaona faida zake na hasara zake

Wacha ningoje siku zangu nife nizikwe niende ahera Kwaheri .



NDOA YANGU INANITESA

Nilikuwa nikifanya kazi katika kampuni moja ya usafirishaji wa madini kutoka Tanzania kupeleka Bang kok nchini Thailand. Kampuni yetu ikiwa ya mtu binafsi na ilikuwa Mkoani Arusha. Mimi Sweedy Kachenje ndiye niliyekuwa idara ya usafirishaji, nikiwa afisa mauzo.

Katika maisha yangu yote nilitegemea sana na nilihitaji kuwa na mwenzi wa kuishi naye, kama vile familia nyingine bora ambazo kila siku zina furaha na ridhaa. Kwa kila mmoja kuwa mwanandani wa mwenzake. Pia nilimuomba mungu kwa kila hali si kanisani na hata nikiwa katika mapumziko yangu, anipatie mwanamke ambaye angenifaa katika maisha yangu.Kila siku palipokucha,niliamka nikiwa na wazo la kumpata nimpendaye na anipendaye.Niliamini hivyo japo sikuwa na uhakika kama kweli ningepata mtu kama huyo maishani mwangu.

Siku zote nilijibidisha kuwa mfano bora ili niweze kupata mchumba, nilikuwa mtiifu, nikiwa heshimu wenzangu na kushirikiana nao vema kujenga Taifa.Kujaribu kuwa na marafiki wengi wa jinsia tofauti. Nilijitahidi nikihisi pengine wale marafiki wangenifaa kumbahatisha wa ubani wangu. Pamoja na yote hayo sikuweza kubahatika kupata niliyempenda kutoka moyoni, na aliyenipenda. Nilizidi kumuomba Mungu anishushie neema ya kumpata wa ubani wangu. Ikafikia wakati nikaomba ushauri, lakini wale niliowaomba ushauri walionekana kuwa fukara wa mawazo.Walinishauri wakisema kuoa ni kuoa.Eti mwanamke ningemfunza kama angekuwa na tabia mbaya.Nikafikiri mara mia mia ushauri wao nikaona haukuwa na maana zaidi ya upofu.

“Bw. Kachenje inamaana uwingi wa wanawake ulimwenguni umekosa umpendaye?”Lilikuwa swali nililoulizwa na rafiki yangu.Hatahivyo nilishinda kumjibu na hatimaye nikamdharau.

“Inamaana kuchagua mke wa kuishinae ni sawa na kuokota fungu la samaki sokoni ama vipi?”Nilijiuliza bila kujijibu kwa wakati huo.

Nilishindwa kuokota mke ilimradi mke kama vile mtu anavyookota nyanya sokoni na kulipa pesa, nafikiri hata anayeokota nyanya nae huchagua. Japo kuna usemi usemao mchagua nazi hupata koroma usemi huo niliupinga na kuutupilia mbali. Niliamini usemi wa kuoa ni kuoa pengine ningefanya hivyo basi ndoa yangu isinge kuwa na ladha ya unyumba na isingedumu maishani.

Nilijawa na imani kuwa mke mwema hupewa na Mungu, niliishi kwa matumaini ya Mungu na nilitegemea msaada mkubwa kutoka kwake. Wazazi wangu Mungu aliwapa baraka walikuwa hai wakinisubiri nioe wamuone mkwe na wajukuu wao kabla ya kufa. Kwa bahati mbaya sikuweza kupewa upeo wa kuona mchumba mwema ambaye angekuwa mke wangu, japo nilikuwa na kazi nzuri na nafasi yangu kazini ilinifanya nionekane maridadi saa zote.

Watu wengi walioniona walinishangaa sana, kwani sikuwahi kuonekana na mwanamke yoyote niliyeongozana naye katika maisha yangu. Si kwamba nilikuwa na hitilafu yoyote mwilini!. Hapana nilikuwa mwanaume rijali, na sikupenda kujihusisha na ngono,kwani magonjwa yamezagaa kama inzi kwenye mzoga.Licha ya magonjwa, ni dhambi kubwa kuzini nje ya ndoa.Nilitambua kwamba jambo hilo halimfurahishi muumba hata kidogo.Siku zote nilikuwa nikijilaumu,ikafikia wakati nikitaka kuokota mwanamke hata baa, moyo ukasita ukinitaka niwe na subira zaidi.Lakini subira gani huumiza matumbo. Je subira hii itazaa matunda ama nikunizidishia bala uzeeni?.Nikayatupilia mbali mawazo potofu. Nilihitaji kuwa na subira nikihisi pengine ningempata atakaye nipenda na mimi kumpenda.

Umri wangu ulisogea kufikia miaka arobaini. Hali ambayo iliwaogopesha sana wazazi wangu, waliokuwa wazee wa kujikongoja. Nilizaliwa mtoto pekee wa kiume na dada zangu watatu.

Wazazi wangu walichoka na maneno yangu. “Bado umri wa kuona. Nitaoa Mungu akipenda, mke mwema hupewa na Mungu” Miaka yote huwa nilikuwa najitetea hivyo .

Ulifika wakati baba na mama walitaka kuniachia laana baada ya kuwadanganya zaidi ya miaka kumi toka nipate pesa na kuwajengea nyumba. Walitaka wawaone wajukuu wao kabla ya kufariki, walijua umri walio kuwa nao,wasingeishi miaka mitano ama saba mbeleni wangepoteza maisha.

Kwa kuwaridhisha na kukwepa radhi za wazazi niliwaomba wanitafutie Mke. Niliamini mke ambaye ningepewa na wazazi angenifaa maishani. “Baba akimpenda binti, hata mimi sina budi kumpenda” nilijisemea mwenyewe baada ya kuwapa kazi ya kunichagulia msichana mwenye sifa zote zile mwanamke anatakiwa kuwa nazo. Ni miongoni mwa nidhamu kwa mume. Nilikuwa na furaha kidogo, kwani nilijiona niliyejaa Ukungu wa kutopendwa na kutopenda.

Kwa ujumla sikujua ilikuwa ni mitihani ya Mungu kwani mimi ni miongoni mwa vijana waliokuwa wakicheka vijana waliochaguliwa wachumba na wazazi wao, hakuna kitendo nilichokichukia kama kuchaguliwa msichana na wazazi. Nilikuwa na imani ya kijana akichaguliwa mke basi hata ndoa ingejaa migogoro isiyoisha na pengine ikavunjika.

**********


Kampuni yetu iliitwa JOPHU MINING TRANSPORT CO LTD, mwenye Kampuni yetu, alijulikana kwa jina la Mzee Jophu Kundy . Ndiye alikuwa Mkurugenzi na mmiliki wa Kampuni.

Kipindi cha miaka ya sabini kulikuwa hakuna gonjwa la Ukimwi, kama lilikuwepo basi ilikuwa halijajulikana kama sasa. Nilikuwa nikienda Nchi Thailand kila wiki kuuza madini aina ya Tanzanite. Siku zote nilikuwa na urafiki wa karibu na mmiliki wetu Mzee Jophu. Hakuna hata mtu mmoja aliyethubutu kuongea na mzee Jophu aliyeonekana mwenye uso wa ukali saa zote. Haikuwahi kupita siku bila mzee Jophu kuita “Sweedy njoo” nk.Alikuwa kazoea jina langu , pia alinipenda kama mwanae.

Siku moja niliondoka katika uwanja wa Kia (Kilimanjaro International Airport) nikielekea Nchini Thailand, Bang kok.Vaaa yangu toshani kielelezo kwa mtu asiyenifahamu,kusema mimi ni mtu mwenye pesa za kunifanya niitwe tajiri. Nilivaa suti ya kijivu,chini nilivalia viatu vya mchongoko,vijana wa sasa huviita ‘Mkuki moyoni’,mkono wa kushoto nilishikilia ‘breefcase’lililojaa madini ya Tanzanite.Pia nilivalia miwani ya jua,iliyosababisha vigumu kuona macho yangu.

Nilikuwa nimebeba madini gram 5000gm. Sawa sawa na kilo tano Kg 5. Kilo mbili ilikuwa ni rangi ya blue colour A na kilo tatu (3kg) yalikuwa ni rangi ya mkojo, kwa wale wakazi wa Mererani wanajua vizuri wakiona na rangi ya coke ile maji ya kunywa ilikuwa (gm 50).

Ndege iliacha aridhi ya Tanzania mnamo saa nne unusu asubuhi, ambako ilichanja mawimbi angani saa mbili na sekunde ya kumi iltua uwanja wa kimataifa Bang kok.Nilifanikiwa kushuka salama nikiwa mtu wa tano. Sikuweza kwenda kwenye soko siku hiyo, nilielekea kwenye maegesho ya gari za kukodi amabako nilikodi gari.

“Halo.kutoka hapa hadi Care lodge ni kiasi gani cha pesa?”

“Dola tano.Karibu”

“Sikuweza kubishana sana kwani niliamini kauli ya ‘nipunguzie bwana’ ni huku kwetu.Alinifungulia mlango wa mbele, nilivuta mguu wangu wa kulia na kuingia ndani mlango wa mbele kulia mwa dereva.Gari hilo lilikuwa ‘Left hand’.Nilienda moja kwa moja kwenye hoteli iliyoitwa CARE LODRGE .Dereva alitumia kama dakika nne kuingia lango la hoteli hiyo.Nilipofika, nilimlipa ujira wake, nikaelekea ofisi za kupokelea wageni(Mapokezi). Sikutaka kwenda kufanya biashara kwa wakati huo. Niliamua kujipumzisha kutokana na uchovu wa safari, jambo la kushangaza nilichokiona mbele ya macho yangu sikuweza kuamini macho yangu kama yalikuwa sawa sawa ama vipi, nilijaribu kupikicha macho pengine ni ule ukungu wa kutokuwahi kupenda. Lakini cha ajabu moyo wangu ulisimama kama sekunde kadhaa, kisha ukaendelea mapigo yake yakawa ya taratibu mno, ambayo sikuweza hata kuyasikia. Nilihisi jasho jepesi likitiririka, kwanza nilijitazama kisha nikamtazama mtu huyo, hata hivyo sikuamini kwamba kwa uzuri wake kamwe ningependwa mtu mweusi tena Mtanzania?.

Niliona mwanadada mmoja aliyekuwa amekaa karibu na muhudumu wa mapokezi katika hoteli hiyo, msichana huyo alikuwa Mzungu si mzungu, muhindi si muhindi, mwarabu si mwarabu hata kwenye weusi hakuwepo. Baada ya dakika tano, nikiwa nimemtumbulia jicho la matamanio, alinisalimia .

“Kaka habari yako”

“Nzuri, sijui nyie”nilijibu salamu kwa wote,nikiwa bado sijabandua jicho usoni mwake.Sikushughulika na huyu mwingine,macho yangu tayari yalishapata chakula.Nilimtizama hamu haikuniisha nikatabani abaki pale pale macho yangu ya shibe.

“Mimi mzima”aliitikia msichana huyo na aliyefuata ni wamapokezi.

“Hata mimi mzima pia” walinisalimia.

Sikupenda kukaa na ule mzigo wenye thamani kubwa niliandikisha jina langu na kuchukua chumba namba kumi.Kila nilipotaka kuondoka kuelekea chumba nilicholipia ,nilisita na kubakia mdomo wazi,mwili ulibweteka nikitamani kufahamiana zaidi na mwanadada yule.Niliamua kujilazimiza kuondoka ingawa nafisi ilitukutika,nilipofungua mlango wangu,niligeuka kumtizama yule mlimbwendekama vile nikihakikisha kama atakuwa pale.Nilimuona nae akinitizama.

“Mtoto mtoto,Duu!.Tembea uone mengi”Niliongea akilini nikiwa nafungua mlango,katika kuzungusha funguo mlango ukatii sheria ,ukanipa nafasi ya kuingia.Nilihifadhi Breefcase yangu haraka na kufungua mlango kutoka nje.Nilikuwa nimeshikilia funguo,nikajikuta nikiziachia bila kujijua.Yote ni baada ya kumwona yule binti akiwa ametoka chumba kilichokuwa mkabala na changu.

“Kumbe chumba nilichochukua kilikuwa karibu na chumba cha Binti yule niliyesalimiana nae muda mfupi tangu nifike pale.”Nilijisemea moyoni kiwa nimeacha mdomo wazi ,nikimtizama ,alikuwa kajifunga taulo nyepesi kabisa.Tayari kwa sasa alikuwa kanipa mgongo,kila alipovuta hatua , makalio yake yalitikisikia kama mawimbi ya maji baharini.Miguu yake minene iliyobeba umbile la wastani lilijivuta kwa madaha.Nilijikuta nikimtizama hadi alipoishia.

Kwa kweli nilimpenda na niliamini angenifaa kuwa mwezi wangu na pambo la ndani. Hata hivyo niliumia moyoni je kama akinikubali nitafanya nini kama baba na mama watakuwa wamenipatia mchumba wa kumuoa?.Wazo hilo lilinijia na nikaamua kulitupilia mbali. Lakini ngoja nisiumize kichwa sijui nitakubaliwa au laa! Kwani nitese nafsi yangu? Nilizidi kuwaza wakati namalizia kufunga chumba. Pasipo kutegemea mara nambona tena akiwa kashikilia mafuta ya lotion. Safari hii alikuwa anakuja kwa mbele,niliweza kufaidi kuisawiri sura yake vema, ilioonyesha umahiri wa muumba.Tembe yake ungeweza kudhania kachoka vile,lakini hapana ukweli halisi.Ule ndio mwendo wake halisi,ikafikia hatua nikadhani hakanyagi chini, kwa jinsi alivyotembea utafikiri anaionea aridhi huruma. Nikajikuta moyo ukinipasuka “paaa” nikiwa na mshangaa nae alinitolea tabasamu nono! lililoshamiri usoni mwake.Tena likiwa limeambatana na mwanya mzuri.Nilishikwa na butwaa kama dakika kadhaa, nikajikuta ubongo ukifa ganzi. Tulibaki macho pima, hapo nilijua dhahiri kama kunapimana hivi.Nikajitizama na kumtizama kwa mara ya pili. Mapigo y a moyo yakaanza kupungua.Hata hivyo nilishindwa kuvumilia yote niliyoyaona kwa safari hii.

“Samahani dada naweza kujua jina lako”alikuwa kesha nikaribia.

“Yaa!. Jina langu ni Jeniffer John”

“Sawa . Ahsante unajina zuri. Naitwa Sweedy Kachenje” nilijitambulisha nikilamba midomo yangu kuua aibu flani iliyochomoza kama mshale wa sekunde na kupotea.

Tuliongea mengi na Jeniffer nae hakuwa mvivu wa kujibu maswali na chochote nilichomuelezea, niliamini ndoto yangu ilitimia, yule mwanamke niliyempata angeweza kufunika pengo kubwa maishani mwangu. Hata hivyo katika mazungumzo yetu alinitamkia kwa kinywa chake kuwa nae ananipenda sana, kuliko hata mimi ninavyompenda. Ni binti aliyeukonga moyo wangu na kuuteka kila sehemu ya viungo vya mwili wangu, “Kweli subira huvuta heri” niliongea kimya kimya kwenye mtiririko wa mawazo.

Jennifer alikuwa ni mchanganyiko wa Mzungu na mwafrika (chotara) na ni msichana aliyetoka Bara la Africa kama mimi, tofauti ni kwamba yeye alitokea Africa ya kusini, na mimi nilitokea Tanzania. Wala hakujali Nchi niliyotoka kuwa ilikuwa ya kimaskini, inamaana alinipenda na umasikini wangu. Tuliongea na kujikuta mawazo yetu yakiwa sawa, kwa kutaka kunionyesha upendo alikubali ombi langu la kutaka anisindikize kuupitisha usiku uliojaa raha za kila aina. Alidiriki kuacha chumba chake na kuja kulala na mimi, nilimgusia suala la ndoa nalo alilikubali alikuwa tayari kubadili uraia kuwa Mtanzania. Lakini kama angekuwa Mtanzania aliyekuwa Afrika ya Kusini umwambie arudi aolewe Tanzania, angeruka hata futi mia.

Kwa upande wa mapenzi nilikoga na penzi motomoto, hakuwa mvivu wa kujishughulisha, tulisaidiana kupitisha usiku huo mwanana uliojaa mahaba ya kila aina, si mlimani tulipanda vichochoroni tulipita kwa nia imara ya kumridhisha Jeniffer aliyeonekana mgeni kwenye ulimwengu huo. Asubuhi kulipopambazuka nilimuaga Jennifer na kuelekea soko la madini ya Tanzanite, lililoitwa King Life. Kabla ya kuondoka nilimuachia namba ya simu email address yangu kwa mawasiliano. Na niliamua kufanya hivyo ili kuwahi na kuwaeleza wazazi habari mpya, wasihangaike kunitafutia mchumba kwani nilishampata mrembo. Nilifanikiwa kuuza madini yote kwa bei nzuri na kurudi Tanzania.

************


Nilipofika kazini, nilikabidhi pesa kwa Tajiri yangu Mzee Jophu tukiwa katika maongezi ya mabadiliko ya kibiashara. Tulisikia mlango ukigongwa kwa nje, bila kujali wala kujua ni nani mtu huyo, Mzee Jophu aliamuru aingie, Aliingia na alikuwa sekretari wa Mzee Jophu.

“Boss, samahani kuna wageni wa Sweedy wanamuhitaji” sekretari aliongea akijikanyaga kanyaga na kuuma vidole.Alionekana kumuogopa sana bosi wake.

“Sawa waambie wasubiri kidogo” Mzee Jophu alijibu kwa kifupi na kuendelea na mazungumzo nami.

Tuliongea na kumaliza, Mzee Jophu alikuwa wa kwanza kutoka kinyume na mashariti yake, tuliongozana kujua nani alikuwa ananiita. Kwenye viti vya mapokezi ya wageni, nilimuona baba na mama, mama mwingine wa makamo ambaye simfahamu, pembeni ya yule mama nisiye mfahamu nilimuona binti mwingine mrembo. Kwa haraka ubongo ulifanya kazi yake kwa bidii na kukumbuka kuwa niliwapa kazi wazazi wangu kunitafutia mchumba baada ya kuzunguka kila kona ya dunia bila mafanikio. Kumbukumbu hiyo iliutesa moyo wangu kwani nilishapata mchumba mwingine, tena mzuri kuliko yule niliyeletewa na wazazi, japo nae alikuwa mzuri lakini kamwe asingefurukuta kwa Jennifer.Ndivyo nilivyo hisi moyoni na wasiwasi ukawa umejidhatiti akilini.

“Baba shikamoo, mama shikamoo!, Mama shikamoo!, Dada habari yako! Niliwasalimia wote nikipita kwa mstari huku nikiwashika mikono. Pia mzee Jophu naye alifanya hivyo hivyo nilivyofanya mimi. Lakini cha ajabu aliposhikana mkono na binti yule akabaki amemshika muda mrefu, macho ya upendo yakiwa yanatambaa usoni mwake. Nilishtuka pale yule binti alipovuta kujinasua mikononi mwa Mzee Jophu.

Baba hakupenda kufanya mambo kwa siri, alizungumza yote mbele ya mzee Jophu mama na yule mama mwingine na binti yule.

“Mwanangu unayemuona pembeni ya mama yako ni mama mkweo na msichana unae muona hapo ni mkeo kazi uliyotutuma tumeikamilisha. Sidhani kuna la ziada zaidi ya kuhitimisha ndoa kanisani” Baba alizungumza na alitegemea kuona furaha, lakini furaha yangu ilifunikwa na uzuri wa Jennifer niliyeonja penzi lake Nchini Thailand.

“Mbona huongei wala huonyeshi furaha” Baba aliniuliza kwa mshangao.

“Baba ningeomba tuzungumze faragha kidogo. Kuna mambo mengine hayafai kuzungumza mbele ya mama na watu wengine, nilipoongea hivyo baba alikiri na kujikuta akitikisa kichwa kuafiki yale niliyoyasema.

Tuliondoka eneo lile na kulizunguka nyuma ya jengo la kazini. “Baba nimekuita mazungumzo ya pembeni nina jipya lililojitokeza”

“Jipya lipi zaidi ya hili nililo kuletea? Baba alizidi kunikazia macho ya ukali.

“Ndio hilo ni jipya ulilolileta wewe nashukuru. Lakini hata mimi nina jipya nililopata nikiwa Nchini Thailand kikazi”Baba alionekana mwenye furaha iliyotoka moyoni, alihisi pengine nimemletea zawadi, kumbe asijue ni ujumbe wa kumkataa binti walionitafutia.

“Umeniletea suti nini mwanangu Sweedy?” Baba aliuliza huku akiwa ametoa tabasamu zito la kupokea zawadi.

“Hapana baba, ila ninaomba radhi kwa usumbufu.”

“Usumbufu gani?. Sema”

“Nimewasumbua kunitafuti mchumba. Baba nikiwa Bangkok Nchini Thailand nimebahatika kupata mchumba ninayetegemea kufunga naye ndoa.”

“Eti nini”? usinichezee naona unataka radhi ya wazazi, hatuelewi kila kitu tumemaliza. Mahari tumeshalipa tunachosubiri ni ndoa tu. Halina mjadala” Baba aliongea kwa ukali, mishipa ya shingoni ilimtoka, ghafla macho yake yalibadilika rangi na kuwa mekundu.

“Naomba uniambie sasa hivi. Unamuoa yule binti au laa! Sitaki uniambie nikupe muda” Baba alizidi kufoka kwa sauti. Sauti yake ilienda mpaka alipokuwa mama na mama wa yule binti na binti. “Baba nisamehe sauti hiyo inasafiri naomba yaishe”Mara anakuja mama akikimbia huku kanga zikimdondoka alikwapua kanga na kufika pale nilipokuwa na baba.

“Baba Sweedy kuna nini? Mama aliuliza kwa kudadisi .

“Mwanao anataka kututia aibu.”Baba alisema akinikazia jicho la ghadhabu.

“Aibu gani tena?”Mama akauliza akiwa anamtumbulia macho Baba.

“Mwanao hataki tena kuoa.Anasema binti tuliyemtafutia hajampenda.Na ameshapata mchumba huko alikotoka” Baba aliongea kwa sauti ya taratibu iliyojaa uchungu.

“Hakuna pingamizi lazima aoe la sivyo atazunguka hii dunia wakumwoa hatamuona. Hata huyo anayesema amempata pia atamkataa. Kama sisi sio…… nilimkatisha mama aliyekuwa anaongea kama kuniachia radhi.

“Mama sasa naona mnaniachia laana, basi nitamuoa binti huyo.” Muda mfupi niliona maneno hayo yalirudisha furaha zao. Hawakupenda nichelewe kuoa, mipango ya harusi ilifanyika na tarehe ya harusi ilipangwa.

Wiki tatu kabla ya kusafiri kwenda nchini Thailand. Nilipokubali wazazi wote walirudi kule tulipowaacha mama wa binti, binti mwenyewe ambaye ndiye mke wangu mtarajiwa na mzee Jophu. Lakini tukiwa katika mazungumzo mimi na wazazi wangu, huku nyuma Mzee Jophu alikuwa akiongea na mama wa binti aliongea kuwa anamuhitaji yule binti amuoe yeye na sio mimi tena mambo hayo yalifanyika haraka na kwa siri, si tu kwa maneno bali Mzee Jophu alimpatia hela nyingi kuliko zile za wazazi wangu walizolipa.

“Mama kamata laki tano hizi ni zako bado nitakuongeza” kwa shida ya mwanamama yule alizipokea na kuziweka kibindoni kwa haraka huku akimuahidi kuvunja ndoa isifungwe, aliniamini angetumia njia yoyote ya kukwamisha ndoa. Ni mambo ya kusikitisha, mzee Jophu pamoja na kuwa baba wa familia ya watoto watatu, bado alihitaji mke wa pembeni aliamini kwa pesa zake nisingeweza kufurukuta “Pesa inazungumza. Pesa ni kila kitu.Haki pasipo haki kwa tajiri ni haki” mzee Jophu alizidi kuzungumza.

Tuliporudi pale nilishangaa kumuona Mzee Jophu akiwa na hasira alikunja ndita aliponiona tofauti na mwanzoni. Nilijiuliza nina kosa gani, kama ni mazungumzo yetu yalikuwa mazuri nimemfanya nini boss mbona ananitupia jicho la ukali, nilishindwa kujua kilichoendelea kwa wakati huo.Mama mkwe mtarajiwa nae alipindua midomo yake na kuibetua kama iliyoteguka jicho la dharau lilinitizama kuanzia chini ya unyayo hadi juu ya nywele, kisha kabla ya yote nilisikia akisema “Kijana wenu hana hadhi ya kumuoa mwanangu. Kwa jinsi ninavyomuona” nilistaajabu kusikia sauti iliyoambatana na kusonywa.

“Kwa nini mama Getu?. Amefanya nini mwanangu?” Mama alimuliza kwa sauti ya chini.

“Mwanao hana nidhamu. Uso wake umetawaliwa na dharau. Hawezi kumuoa mwanngu” aliongea kama kawaida alinitupia macho ya kunitazama kama mtu aliyejinyea japo maneno yake niliona na niliyasikia yakinichoma moyoni mwangu. Nilikabwa na fundo kali la ghadhabu nikaamua kumuheshimu tu, kama si heshima basi ningeropoka neno lolote baya nae limkere moyoni. Mzee Jophu alikuwa kimya pembeni , macho yakipepesa kwa kuibia na furaha iliyojificha ilionekana usoni mwake, lakini sikuweza kugundua kwanini mama yule alibadilika yeye na Mzee Jophu.

Mama na baba walimuomba radhi awasamehe kuzaa mtoto asiye na nidhamu na anisamehe, walijua pengine hasira ile ni kile kitendo cha mimi kumuambia baba siko tayari kumuoa mwanae kwani nilipata mchumba Thailand. Lakini mama mkwe mtarajiwa msimamo wake ulikuwa pale pale, hakutaka nimuoe mwanae, na alitaka arudishe mahari, kwa kile kitendo cha kusema

“Mtoto wenu hana nidhamu” hata alipoulizwa nidhamu gani alishindwa na kubaki akisema.

“Sitaki nasema basi. Chukueni hela zenu na ng’ombe zenu nne, sikotayari kumuozesha mwanangu” Aliendelea kuwa na msimamo wake. Kwa maneno ya mama yule yalikuwa ni furaha kwangu, kwani ningemkosa basi ningeenda kumuoa Jennifer na kwa upande mwingine yalinikera sana, hasa alipozidi kusema sina hadhi ya kumuoa mwanae. Eti nina dharau, nilishindwa kumuelewa alikuwa na maana gani?.

Baba na mama yangu walinivuta pembeni na kuzungumza kama dakika takribani tatu, kisha wakarudi na kuomba waondoke wakayazungumze nyumbani. Waliondoka wote, baba, mama, mama Getruda na Getruda. Hawakutaka kuyazungumza pale kwani ilikuwa sio sehemu yake. Tulibaki mimi na mzee Jophu, lakini sikumuona akiwa na furaha kama nilivyomzoea, hakutaka kuongea na mimi.

“Boss mbona unaonekana una hasira nini hasa nilichokukosea. Nimeona umebadilika” kimya kilitanda sikupata jibu lolote zaidi ya kunitazama na kuondoka zake.

Kesho asubuhi nilipowasili kazini, nilifanya kazi vizuri kama kawaida nikiwa naongea na baba na mama kwenye simu. Mara Boss Mzee Jophu anaingia na wakati huo nilimaliza maongezi na kukata simu, nilipomsalimia hakuitikia salamu yangu, bali alinitupia barua mezani, na kusema “Sina shida na salamu yako. Barua hiyo na unijibu haraka iwezekanavyo.Nakupa nusu saa” aliondoka na kufunga mlango kwa kishindo kikubwa.

Nilishindwa kumuelewa, lakini kwa matendo yake nilihisi na kuamini barua ile ilikuwa ya kufukuzwa kazi, lakini nilishindwa kuelewa kosa hasa lilikuwa lipi?. Homa ya kufukuzwa kazi ikaniingia, nilishindwa kuisoma ile barua, niliinamisha kichwa nikiwaza.

“Hivi kama nitakuwa nimefukuzwa kazi nitaenda wapi? Nitamuonaje Jennifer tena? Nauli sina ya kwenda Bangkok” Ghafla mawazo yakanijia nilikumbuka kuwa boss alinipa muda wa nusu saa kuijibu barua yake. Ndipo nilipoanza kuifungua barua huku mikono na vidole vyote kwa pamoja vikitetemeka kama mgonjwa wa degedege. Nilifanikiwa kufungua Barua. Kitu cha kwanza kukutana nacho ni maneno yaliyoandikwa kwa herufi kubwa.

YAH: UPIMAJI WA AFYA KWA AFISA MAUZO, JOPHU MINING TRANSPORT CO.LTD.

Moyo wangu ulipasuka kwa furaha “nilihisi ni ridandasi kumbe ni kupima afya hilo halina shida. Ngoja niendelee kusoma” nilijisemea kimoyomoyo.

HUSIKA NA KICHWA CHA HABARI HAPO JUU, TUMEPATA BARUA KUWA WAFANYAKAZI WA KAMPUNI YETU WANAHITAJIKA KUPIMA AFYA ZAO, HASA UKIMWI NA AFISA MAUZO AWE WA KWANZA . BODI ILIPANGA KIKAO CHA SIRI.

MKURUGENZI WA KAMPUNI

JOPHU KUNDY.

Nilimaliza kusoma barua, lakini hata hivyo moyoni nilijiuliza “Kwanini Mzee Jophu na msalimia haniitikii, halafu akanipa barua ya kwenda kupima afya yangu, au anahisi nina virusi nini?. Ama anataka kunitafutia kosa ili anifukuze kazi nini?. Kwanini ananikasirikia, ni kwa vile wazazi wangu wamekuja kuongelea maswala ya kuoa hapa kazini au ni nini?.” Nilizidi kutumbukia kwenye kisima cha mawazo kem kem, bila kupata jibu muafaka. Kwa ujumla nilishindwa kuelewa wazo halisi la Boss kunitaka nikapime afya yangu, na nikiwa mtu wa kwanza kazini kupima virusi na kwa nini alinikasirikia. Muda niliopewa na Mzee Jophu ulitimia, hakupenda kupoteza muda, aliingia ofisini kwangu na kuniuliza,

“Sweedy umeisoma barua niliyokupatia?. Naomba majibu. Utaenda kupima au hutakwenda?”

“Nitakwenda boss, lakini kwani ni lazima kupima?”

“Ndio, ni lazima hasa wewe” Mzee Jophu alinijibu kwa uhakika.

“Kwa nini mimi iwe lazima, asiwe mfanyakazi mwingine. Boss unanitisha sana hasa unaposema ni lazima mimi, na cha kushangaza boss hutaki kuitikia salamu zangu. Nimekukosea nini, naomba uniambie, ndipo nami nikujibu kuhusu jibu la kupima” Niliongea nikilalamika kidhaifu kwa boss, niliogopa mabadiliko ya boss.

“Ok, usihofu kuhusu kutoitikia salamu yako. Nilijaribu kukutingisha tu unajua Sweedy mimi na wewe dam dam. Pia watu wanatufananisha kama mtu na mdogo wake, wengine wanajua dhahiri kuwa wewe ni mdogo wangu wa toka nitoke. Nilikuwa nakupima imani yako, hivi wewe hushangai toka nikuajiri kazi hatujawahi kukasirikiana iwe sasa? Wewe ndiye ninaye kuamini katika kampuni yangu, hata nikifa leo, wewe ndiye utakaye shikilia mali mpaka watoto wangu watakapokomaa kiakili. Umenielewa Sweedy? Ondoa shaka yale yote ni matani.” Mzee Jophu aliamua kuficha ukweli uliopo moyoni mwake, alinichukia mno! kwa muda mfupi tu toka amuone Getruda, binti mrembo, hakutaka nijue nini kilichotaka kuendelea, alizidi kunifumba kwa maneno ya uwongo na kunifanya nimuamini kuliko siku za nyuma.

Nilipandisha pumzi na kushusha kwa nguvu “oophhhh!” “Ni kweli boss lakini ilinifanya niwe na alama ya kuuliza ndani ya ubongo wangu, hata hivyo sikuamini kuwa ni wewe ulinibadilikia kiasi hicho. Kuhusu kupima nani kakupa wazo hili?”.

“Ok, swali zuri, nilipata barua kutoka mamlaka ya Uhamiaji, kwamba si ruhusa mtu kutoka nje ya Nchi bila kupima afya, hivyo wewe kama Afisa mauzo bila kupima hutaenda Nchini Thailand lakini utakapopima utaendelea na kazi yako kama kawaida.”

“Hakuna shida boss mimi nitapima virusi najiamini sina kitu, mimi sio mkware” Nilimjibu. Furaha yangu nikutaka kwenda nchini Thailand nikaonane na Jennifer .

“Kesho asubuhi watakuja Daktari kukutoa damu. Hutaenda huko hospitalini, cheo chako kinakulinda na sitaki uhangaike. Watakuja na kukupima na wiki ya tatu utaenda Nchini Thailand kama hutakuwa na virusi. Sio sheria yangu hapana ni serikali”Akasema Boss akizunguka zunguka pale ofisini.Alionekana mwenye furahabaada yakukubali kuopimwa.

“Nitakuongezea mshaharaasilimia hamsini wa mwanzoni”Alizidi kunipa motisha.

“Nitafurahi Bossi” .

Tukiwa kwenye maongezi nilisikia simu ikiita. Nilipoitoa mfukoni niliona namba za baba juu ya kio cha simu. Niliipokea na kuanza kuongea .

“Shikamoo baba.Mama hajambo?”

“Marahaba!. Wote wazima wanakusalimu. Jiandae kwa harusi yule mama amekubali umuoe mwanae. Ni baada ya kwenda kwenye mila na desturi, amepewa faini ya kutaka kurudisha mahari. Umenielewa mwanangu?”

“Ndio baba. Kweli amekubali nimuoe mwanae?. Hata siamini nitajitahidi kukusanya mchango wa harusi”

“Sawa jitahidi mwanangu” Tulimaliza maongezi na kukata simu.

Nilipomtizama Mzee Jophu alinitupia macho ya lawama, lakini hata hivyo nilichukulia usemi wa kupima imani kumbe yeye maneno ya yule mama kukubali nimuoe mwanae yalimuumiza roho sana, na alikiri kumuua mama Getruda kwa kumsaliti na kumchukulia laki zake tano, lakini kwa upande wa mama Getruda hakula wala hakuzitumia hata senti tano yoyote, alipanga kumrudishia baada ya kushindwa kuzuia ndoa isifanyike.

*************

Kesho yake ilikuwa siku ya mimi kupimwa afya ikiwemo na kupimwa virusi vya Ukimwi, sikuwa na wasiwasi nilisubiri waje kunipima kwani nilijiamini sikuwa na virusi, japo nilifanya mapenzi na Jennifer kule Thailand bila kutumia kinga yoyote.Na hata mapenzi niliyofanya yenyewe yalimfurahisha na kumridhisha Jennifer na kukiri mimi ni miongoni mwa wanaume wanaojua mapenzi. Sikupenda Jennifer anidharau kwa upande wa kutomridhisha kimapenzi.

Waliingia Daktari waliovaa magwanda meupe wakiwa na vipimo vyao. Waliongozana moja kwa moja ofisini kwangu, cha ajabu baada ya kusalimiana nao walitaka nivue nguo nibaki na kaptula, jambo hilo nilipinga.

“Kama kunipima damu ninatolewa damu kwenye mkono sio karibu na uume wangu. Nyie ni daktari kweli?”

“Ndio sisi ni daktari unataka vitambulisho?”.

“Sina shida na vitambulisho vyenu. Nyie chukueni damu mkaipime, mkileta majibu mabaya nitarudia hospitali nyingine niliwaeleza waziwazi bila kuwaficha kitu.”Nikiwa nimeketi kitini,wao walikuwa wamesimama.

Haraka haraka daktari mmoja alitoa sindano iliyokuwa na kitu kama maji, sijui ilikuwa sumu au ilikuwa nini!. Maji hiyo ilikuwa ndani ya bomba la sindano. Kama cc 200. Sikuweza kuona nilikuwa nimegeuka kwa upande mwingine ili nisione sindano inavyopenya na kuingia kwenye nyama za mwili wangu. Kwa kifupi nilikuwa muoga wa sindano japo nilikuwa mtu mzima.

Wakati sindano ipo kwenye mshipa wa damu nilisikia kitu kama maji yenye uchungu wa dawa, nilipata maumivu makali nilipogeuka ndipo niliona akigandamiza bomba la sindano kwa haraka ili nisione kitu, lakini niliona kitu kilichoingizwa kwenye mshipa wa damu. Nilishindwa kujua kilikuwa ni kitu cha kuniletea matatizo ama kunijenga ndani ya mwili wangu.

“Dakitari wewe unanipiga sindano au umekuja kunitoa damu ili upime Virusi vya Ukimwi?. Iweje unipige sindano?”. Nilimuuliza daktari kwa hasira baada ya kusikia ile sindano mwili mzima, nilihisi kizunguzungu mwili ukakosa nguvu. Tofauti na kabla ya kuingiza sindano yao, halafu walikuwa bado hawajatoa damu.

“Usijali Sweedy sijakupiga sindano, nataka kutoa damu” alisema huku akivuta damu kwenye bomba la sindano. Na muda mfupi waliniaga, alionekana nesi mmoja kati ya wale waliokuja kunitoa damu mwenye majonzi. Alinitazama kama mtu aliyenionea huruma sana, machozi yalimlenga lenga lakini hakutaka niyaone aligeuka upande wa pili na kujifuta na kitambaa alichokuwa nacho mkononi. Nahisi alikuwa anajua kila kitu kilichotendeka kwa muda ule na sura yake ilikuwa sio ngeni machoni mwangu, lakini nilishindwa kumkumbuka vizuri. Alijua mipango yangu yote hasa ile ya kufunga pingu za maisha. Alijaribu kuwa wa mwisho kuniaga.

Nilisikia akiniambia “Pole sana Sweedy, moyo unaniuma Mungu akubariki maishani. Nenda kanywe maziwa mengi yatakusaidia”. Nesi huyo aliondoka taratibu, huku akigeuka nyuma na kunitazama kwa macho ya huruma. Nilishindwa kumjibu, nilibaki nikiyaganga maumivu ya sindano niliyochomwa mara ya kwanza, ambayo sikuweza kuielewa ilikuwa ya nini mwilini mwangu.

Robo saa baada ya wale daktari kuondoka mkono niliopigwa sindano na kutolewa damu nilihisi unakufa ganzi, kila nilipotafakari yale maneno ya yule nesi na kilio chake nilishindwa kumuelewa zaidi ya kujilaumu kwa nini nimekubali kupimwa pengine wamenipiga sindano yenye sumu ambayo itanidhuru. Kwa upande mwingine sikuamini niliona yule nesi alinipenda bure, na Mzee Jophu asingeweza kuwatuma watu wanipige sindano yenye sumu . Nilimuamini sana tajiri yangu.

****************

Wiki tatu zilitimia na siku ile ya harusi iliwadia. Kila mtu aliisubiri kwa hamu sana siku hiyo hasa wazazi wangu kwani walijisikia furaha kwa mtoto wao wa kiume pekee kufunga pingu za maisha. Nadhani moyoni mwao walijisemea, sasa ule wakati wa kuwaona wajukuu toka kwa mtoto wetu Sweedy umewadia. Mzee Jophu ndiye alikuwa mtu wa kwanza kwa watu walionichangia mchango mkubwa katika kuifanikisha harusi yangu. Sherehe ilipendeza sana, watu walikula na kunywa hadi wakasaza. Namshukuru Mungu sikupata lawama yoyote ya kuhusu sherehe yangu.

Getruda ambaye ndiye ubavu wangu sasa aligubikwa na furaha isiyo kifani. Sherehe iliyopendeza kwa shamrashamra na vifijo, DJ alitumbuiza kwa muziki wa taratibu wa wapendanao hasa kibao kilichopigwa na mwanamuziki Bob rudala nadhani msomaji unaupatapata ule wimbo vilivyo . Utajisikia vipi ukipigwa siku ya harusi yako? “NIMEKUCHAGUA WEWE” nakumbuka baadhi ya maneno yake, “Nimekuchagua wewe uwe wangu, wangu wa maisha wa kufa na kuzikana”msomaji sitaki nikumalizie uhondo tafuta wako na wewe awe wa maisha ili ujiepushe na mengi hasa janga la Ukimwi. MC au Msema chochote watu wa mjini wanavyoita alikuwa anaitwa MR.Kicheche ni kicheche kweli si mchezo ukumbi haukuruhusiwa kukaa kimya siku hiyo watu wote walikuwa wakicheka na kutabasamu kwa wale wasio na bandama. Kwa ufupi sherehe ilipendaza mno, hatukuwa matajiri lakini watu wailiridhika na kila idara ya sherehe.

Sherehe ilipoisha, tulichukuliwa na gari maalumu siku hiyo kwa bwana na bibi harusi na tukaelekea kwenye hotel moja iliyoitwa NGORONGORO HOTEL kujipumzisha. Tulipofika tulikwisha andaliwa kila kitu, chumba kilinukia harufu nzuri za manukato, choo na bafu ndani kwa ndani ilipendeza kwa kweli. Washenga waliondoka tukabaki mimi na mke wangu Getruda Kimario.

Nilikuwa na shauku kubwa ya kukabiliana na binti ambaye alikuwa kigoli, ambaye hakuwahi kuguswa, nilitamani kupata ukweli wa maneno ya baba aliyenieleza kuwa mke niliyeoa alikuwa bikira, na mimi nilitamani kumtoa mwenyewe yaani kama ni gari lilikuwa jipya ‘New model’ na sio mtumba.

Tuliongozana bibi mbele bwana nyuma, wote tukiwa tumefunga taulo tuliingia bafuni na kuanza kuoga. Kweli uzuri wa mke wangu niliufananisha na lulu au tunda Apple. Alikuwa na umbo dogo lenye figa, ambalo lilinifanya nimtamani zaidi na zaidi. Si kifuani, usoni na umbo lote lilinivutia sana. Nilimuogesha nae aliniogesha, tulipomaliza tulijifuta na taulo na kuelekea chumbani.

Tulijitupa kitandani, “Samahani mpenzi nikumbatie, nahisi baridi…nahitaji…..” Ilikuwa sauti ya Getruda iliyojaa mahaba na iliyonisisimua mwili na kuhisi joto .

“Usihofu kila kitu kitakuwa shwari, nitakupa kila kitu unachokitaka” nilimjibu kwa sauti nzito iliyomuingiza kwenye ulimwengu wa mahaba.

“Lakini mpenzi unajua nakupenda sana” Getruda aliongea macho ya udadisi yakiwa yametuwa usoni mwangu.

“Naamini unanipenda mke wangu ndio maana ukaamua tuoane, lakini nahisi mimi ndiye nimezimika kwako zaidi” nilimweleza na hapo hapo tulikumbatiana na mabusu motomoto yalishamiri, si mashavuni, mdomoni na kwenye paji la uso kote tulipeana mabusu ya upendo.

Niliyasikia mapigo ya moyo wake yakienda kwa kasi jasho jepesi lilimchuruzika taratibu nilishindwa kuelewa kwani AC au ‘kipupwe’Kiyoyozi kwa jina letu la kiswahili kilikuwa kinafanya kazi yake kama kawaida. Kila nilipomshika kwenye kona za mapenzi nilimsikia akizizima kwa sauti za mahaba, si kwikwi wala kuweweseka zote zilimburudisha. Niliamua kutulia kidogo baada ya kuona mambo yote nilikuwa namfanyia uume wangu hausisimka hata kidogo, tofauti na siku za nyuma busu moja kila kitu kimesisimka, leo mambo yote sikuona hata dalili.

“Oooh.!!! Sweedy unajua mimi sijawahi kuguswa kabisa!”

“Eti!, samahani sijakuelewa mke wangu”

“ Sijawahi kufanya mapenzi toka kuzaliwa. Naomba unifundishe” sauti nyororo na ya simanzi ya Getruda ilinifanya nilie mwenyewe, sikuwa na nguvu za kiume, bali nilitamana kumkabili mke wangu nilishindwa kujua Ugonjwa wa kupooza kwa uume wangu ulitoka wapi na nitamuambia nini mke wangu, na je atanielewa na wakati nishamchezea kila sehemu, nilizidi kulia sikuwa na la kufanya.

“Unalia nini tena mume wangu?” Getruda aliniuliza akiwa kalala chali, kama mgonjwa aliye mahututi . Mweupe mwili wake ulipendeza na kuzidi kung’ara kila nilipomtazama usiku ule, kwa ufupi alikamilika kila idara,nilitamani nimrukie lakini jogoo wangu hakutaka kuwika kabisa. Nilidanganya “Mke wangu nimeshikwa na kichomi cha tumbo sijui ni hiyo AC “kipupwe” niliongea kidhaifu nikiwa nimeshika tumbo, machozi yakiendelea kuchuruzika taratibu, niliamini kwa maneno ya kusema “Naumwa” Getruda angeridhika na kunionea huruma, aliniangalia kwa huruma na kusema

“Basi mume wangu tuzime usije ukapata matatizo zaidi”. Nikaona duh! Acha nizidi kujitetea “Labda upunguze kidogo”Nilisema nikiwa nimekunja sura na kushika maeneo ya tumbo.

“Pole mpenzi” mke wangu alisema kwa sauti ya utulivu.

“Usiku huu tutapata wapi dawa?. Jikaze usilie”Mke wangu alinionea huruma.

“Usijali mama watoto.Huwa natokewa na tatizo la kichomi ninapofikia hatua ya kufanya tendo la ndoa”

“Kwa hiyo utafanya je?”

“Daktari aliniambia tatizo hili litaisha baada ya kuzoea mwanamke”

“Mwanamke gani, mbona sikuelewi?”

“Wewe, Usijali tatizo hili litaisha”Nilizidi kumpa motisha mke wangu.Lakini moyoni bado wasiwasi ulitanda kuhusu jambo hili geni kabisa mwilini mwangu.

Maneno hayo ndio yaliyomfanya Getruda, mke wangu ainamishe kichwa magotini mwangu kama mtu aliyekuwa akisujudu. Sikujua aliwaza nini akilini mwake, lakini nikahisi yote yalikuwa juu ya matatizo niliyonayo.Muda wa dakika takribani tano nilihisi kitu kama maji maji angali yenye uvuguvu yakidondoka gotini kwa tone moja na moja.Matone hayo nilihisi ni machozi ,nikaamua kuinua uso wake kutizama kwamba ni nini hasa.Kila nilipojaribu kumuinua alikaza shingo.Wazo ambalo nilihisi kwamba alikuwa akilia likajidhatiti akilini na kuhisi sikukosea.Pia nilijaribu kwa mara nyingine kumuinua uso wake, safari hii akanisemesha akionekana kukasirika.

“Mume wangu umeamua kunitesa angali unajua unamatatizo. Kwanini usingenieleza kabla, umenitesa naunaendelea kunitesa. Utafanya nini ilikunisaidia, najisikia vibaya sana mwenzio” aliongea kwa sauti ya chini akiwa anadondosha machozi, mwili wake ulikuwa umelegea, macho mekundu na ya kurembua, hakuweza kuvumilia zaidi ya kulia kwa kwikwi, alitamani niondoe hali ya ubikira na kumpeleka kwenye utu uzima. Maneno ya Getruda yaliniumiza moyo wangu, nilimuonea huruma alivyokuwa akijigaragaza kitandani. Machozi yalichuruzika kwa kasi nilizidi kuwaza.

“Au ni kwa vile ndio mara ya kwanza kukutana naye nini?. Lakini hapana sijapaniki” labda ni uzuri wake unanichanganya nini? . Au ni chango la tumbo limesababisha nini?.Sasa tatizo hili litaniumbua” Nilijiuliza bila kupata muafaka wala sikuweza kuhisi kitu chochote zaidi ya ugonjwa wa kawaida. Tuliupitisha usiku huo usio na ladha ya mapenzi, si mimi wala Getruda wote tulihuzunika.

************

Kwa ujumla maisha ya ndoa niliyaona machungu kama shubiri na pengine machungu kama mitishamba. Nilishindwa kuelewa ugonjwa huo ulitokea wapi na umesababishwa na nini? Nyumbani kwangu nilipaona kama jehanamu, sikuona raha kuwa nyumbani kwani mke wangu alikuwa ananilalamikia kila siku , kila dakika kuhusu ndoa yetu. Tofauti na ndoa nyingine zikiwa changa, watu huwa wanatamani wapate hata likizo ya miezi kadhaa ili wawe pamoja na wandani wao, hapo nasemea kwa wale wafanyakazi kama mimi.Mimi Sweedy kama mtu mwenye uwezo wa kutunga uongo basi nilijitahidi kumridhisha kwa maneno matamu niliyoamini yangemfariji. Uwongo una mwisho wake kumbuka hapo. Lakini hata hivyo ni mtu gani atasikiliza uwongo kila siku. “Kuumwa kuumwa ni kuumwa gani hukokusikoisha?”.

Nilikuwa natoka kazini saa kumi jioni, lakini cha ajabu nilikuwa nikitafuta sehemu ya kupoteza muda ili mradi nirudi nyumbani usiku. Nikiamini mke wangu atakuwa amelala. Siku zote nilitumia njia hiyo, hata kunywa pombe nikajifunza ilimradi nikwepe kugungulika udhaifu wangu.Si mitishamba wala hospitali za kawaida kote nilienda bado ikawa si kitu.

Siku moja mke wangu aliamua kuelekea kazini kuuliza kuhusu ratiba ya kazi zangu. Alimkuta Mzee Jophu mwenyewe.

“Shikamoo baba” Mke wangu akamsalimu pale alipofungua mlango wa Mzee Jophu.

“Marahabaa mchumba mzuri”Mzee Jophu akaitikia salamu kamavile anamuona mke wangu mtoto mdogo.

Hata hivo Getruda ,mke wangu hakujali aliona ni utani tu kwani anajua dhahiri ni shemeji yake.

“Shemeji nimekuja ninashida”Getruda akasema na kusubiri kitu ambacho angeelezwa. Mzee Jophu alionekana kutingwa na shughuli nyingi pale ofisini.

Aliinua kichwa chake na kumtizama Getruda kwa macho ya huba.

“Shida gani shemeji?”

“Wala usishituke ni shida ndogo tu”Getruda akasema akiweka pete yake ya ndoa vema.

“Shemu sema kama ni pesa. Nikupatia au nimambo ya familia unataka kunieleza?”

“Ndio, ulijua je?”

“Najua maana nyie wanawake mmeumbwa na aibu sana. Jambo dogo unaweza ukaogopa kumueleza mwanaume”

“Nijambo dogo kwa kulitizama lakini kwa undani nijambo kubwa”

“Sawa ulitaka tukalizungumzie faragha kidogo?”

“Hapana shem. Naomba nikueleze hapa hapa”

“Sawa nimekuruhusu. Lakini nilipendelea tutoke tukazungumze nje ya ofisi kwani mambo ambayo haya husiani na ofisi tunayazungumzia nje ya ofisi”

“Naomba nizungumzie hapa , ni kwamba sitatumia hata dakika tatu”

“Ok, sema”

“Naomba unieleze, mume wangu anatoka kazini saa ngapi?”

“Wewe kwani kakuambia anatoka saa ngapi?”Mzee Jophu hakujibu swali kama alivyoulizwa bali nae aliligeuza swali upande wa Mke wangu.

“Anasema saa tano usiku”

“Basi inawezekana, kwani mama unaweza kuniambia, maana ya kazi?”

Mzee Jophu alimuuliza swali kwa mtego wa kasa

“Kazi kama ninavyoifahamu ni kitu au ni shuhuli inayoniletea kipato,”

“Ahaa kumbe unajua, mama nenda nitakuambia, maana yake siku nyingine ukiwa na muda.”

“Lakini bado hujanijibu mume wangu hutoka saa ngapi kazi kwako?”

“Saa kumi jioni?”

“Kaaa!. Saa kumi jioni halafu hufika nyumbani saa sita usiku?”

“Inamaana Sweedy hurudi nyumbani usiku?”Mzee Jophu alimtolea Getruda macho ya mshangao, huku akishika kiuno kana kwamba haamini maneno ya Getruda.

“Ndio shemeji”

“Siamini kabisa. Siku zingine huwa na mruhusu saa tisa na siku za jumamosi anatoka saa sita mchana”Mzee Jophu alizidi kuongezea chumvi.Nia yake ni kuvunja ndoa yangu ili afaidi yeye.Alipania kuvuruga ndoa yangu.Siku jua hata nguvu zangu ya kiume zilipoisha ni kwasababu yake.Yeye ndiye alituma watu ambao walivaa kama Daktari kuja kunipiga sindano ya kuua nguvu ya kiume.

“Shemeji inamaana maneno yako niyakweli kabisa”

“Shem nikudanganye iliiweje?.Sitaki kukuvunjia ndoa yako lakini ukweli mumeo hakupendi. Anasema sana kila siku hapa kazini kwamba mpaka sasa hajawahi kufanya tendo la ndoa na wewe.Eti mke gani wa kutafutiwa na wazazi.Anampango wa kukufanya kijakazi pale nyumbani kwake….”

“Eti nini?.Shemeji naweza kuyaamini maneno yako kwani ni miezi miwili sasa hajanigusa kabisa. Kila siku anasingizia kuchoka na kuumwa.Raha ya ndoa iko wapi shem?.Naomba unipe ushauri nimechoka kuvumilia na mateso haya”

“Usichoke shemeji vumilia tabia itabadilika. Yule bwana anapenda watoto wa shule sana na mshahara wake mwingi huishia huko.Juzi tu kashikwa ugoni na mtoto wa shulwe ambapo alitolea faini laki saba, huwezi kuamini lakini ndivyo ilivyotokea. Mumeo ni mkware kweli…Naomab ausije ukamueleza maneno haya naomba ufanye siri, nitakueleza mengi siwezi kuvumilia ukateseka bure binti wa watu”

“Ahsante sana. Leo atanikoma nyumbani”Getruda aliondoka akiwa na mawazo chungu zima.Machozi yalimlenga lenga machoni.Moyo uliuuma sana. Waliagana na Getruda, lakini moyoni Mzee Jophu alibaki na sononeko la upendo kwa mke wangu, Na aliamini kumpata, kwa jinsi alivyo nitumia Daktari wanipige sindano ya kuuwa nguvu za kiume, aliamini njia hiyo aliyotumia ya kuuwa nguvu za uume,wangu ungeshindika kumpata Mke wangu basi angeniuwa kabisa

“Yaani Sweedy ndivyo alivyo?.Nimemtunzia boma langu iliawe wa kwanza kulibomoa lakini hataki, anapambana na watoto wa shule?.Haipiti hata siku moja haachi kusema naumwa sijui kichomi mara nimechoka kumbe anachoshwa na hao makahaba wa shule?”Getruda alizidi kuwaza njia nzima .Hakuwa anaelewa sehemu alipokuwa alisha pita nyumba yetu.

Ilikuwa siku ya juma mosi siku hii aliyotokea kazini,hakuweza kuzungumza chochote na mimi.Alionekana mwenye ghadhabu kali . Hakutaka hata kunikaribia, alikwenda kujipumzisha kitandani.Macho yake fika yalinijulisha kwamba alikasirika sana. Nami niliogopa kumuuliza kwani nilijua lazima alichukia kutokana na matatizo yangu.Sikuwa nalingine kichwani.Wakati wa kulala ulipofika ,nilitoka sebleni ambako nilikuwa nikitizama mkanda wa dini, na kuelekea chumbani.Nilijawa na wasiwasi kwamba usiku huo kungekuwa na kitimtim kikali, dalili niliiona toka mapema kabisa.Sikuwa na amani na maisha yangu, hofu kubwa ilikuwa kwa mke wangu ambaye hakuwa na raha kila aliponiona.Sasa hasira yake ikawa kubwa pale alipopewa maneno ya uchochezi na tajiri yangu.Nilitembea kwa kunyata ilitu asisikie kwamba naelekea kitandani.Kwa sasa nikajongea na kukifikia kitanda.Nilipandisha mguu wa kushoto kwa hadhari sana asishituke. Pia nilihakikisha kitanda hakichezi, jambo hilo nililifanya kwa makini zaidi.Wakati huu napandisha mguu macho yangu yalitizama usoni kwamba mke wangu angeshituka ama vipi. Nilifanikiwa kupandisha mguu wa kwanza, sasa nikajaribu wa pili kuupandisha kitandani. Laiti ningekuwa na uwezo ningejitafutia kitanda changu.Ukweli ndoa yangu niliiona chungu na iliyojaa mateso makubwa sana. Nilikuwa mtu wa wasiwasi tupu.Kitu kingine, nilijiona nisiye na dhamani duniani, nilitamani nife kuliko kuishi kwa shida lakini wasiwasi wangu ukawa huko ahera nikukimbiliako je? Ni kwema aba ndio nitakimbilia mateso mengine?.Nilizidi kuzama kwenye dimbi la mawazo.

Nikafanikiwa kupanda kitandani bila mkewangu kushituka,nilihisi angeshituka angetaka tendo la ndoa wakati huo huo.Sikutaka kulala zaidi ya kulala macho wazi, nilijua nikishikwa na usingizi ningeweza kukoroma ambapo mke wangu angeamka, kwani nilijijua toka niliwa shuleni kwamba nimkoromaji mkubwa hata mtu nyumba ya jirani angesikia.

Sikulala kabisa, nilihakikisha simgusi hata kwa shuka ambapo angeamka na kunisumbua.Saa kumi na robo nilisikia jooo za jirani zikiwika nikajua kwamba kunakaribia kupambazuka. Nikiwa kitandani nilishuhudia miale ya mwanga ikiingia kupitia dirishani.Nikajua tayari palisha kucha.Mpaka wakati huo mke wangu hajazugumza kitu chochote na mimi.

Ilikuwa siku ya Jumapili,siku ya mapumziko,nilikuwa nyumbani na Mke wangu lakini maongezi yetu yalikuwa juu ya unyumba wetu,si kuhusu maendeleo.

“Hivi mume wangu umenioa ili niwe pambo lako au kama TV unitizame tu au laa!.Naomba unieleze nimevumilia vya kutosha”Getruda alisema kwa hasira baada ya kunitengea chai mezani.

Nilishindwa hata kuokota kikombe nikabaki nimeduwaa. Nikanyamaza kimya, nilishindwa niongee uwongo gani,kwani kila siku nilikuwa muongo wa kupindukia,mara naumwa, mara nimechoka kazini, mara sijisikii,zote hizo zilikuwa njia za kukwepa aibu.

“Sema”Mke wangu alifoka kwa kunihimiza.

“Kwani baada ya ndoa ni haki kunitendea hivi?Kila siku hupandi kitandani mpaka mimi nishikwe na usingizi………”

Nilinyamaza kwa muda dakika tatu, kichwa nikiwa nimekiinamisha kama kondoo, kisha nikameza mate na kulamba mdomo, kila nilipotaka kuongea nilijikuta machozi yakitiririka kwa kasi,nilihisi labda nililogwa na walimwengu,kweli imani ya kishirikina ilitawala ndani ya ubongo.Niliamua kujikaza na kuanza kuongoa uwongo.

“Mke wangu shughuli zangu nzito sana, halafu ni za usiku mno!huwa nachoka nashindwa kufanya tendo la ndoa na wewe”.

“Eti nini? kwa hiyo kuna wengine unaofanya nao?. Si ndio, hao machangu wa shule ndio wanakusababishia unione kama mboga zilizochacha eee!.Eti nashindwa kufanya tendo la ndoa na wewe”.Mke wangu aliongea kwa kufoka huku akibana sauti na pua akiniigiza nilivyo sema.

“Hapana mke wangu” nilimjibu kwa sauti ya kidhaifu iliojaa uwoga na simanzi. Nilikuwa niiingia baa na kunywa, niliporejea nyumbani uliku usiku wa manane nikiwa chakari. Mke wangu hakuweza kugundua mapema, hata mimi mwenyewe sikujua ugonjwa huu niliupata wapi.

“Mume wangu”

“Naam mke wangu”Nilimwitikia nikiwa nimeangalia chini,kwa mbali mapigo ya moyo yalinidunda.

“Eti unasubutu kuniitikia.Wewe mwanaume kweli?”

Sikutegemea maneno hayo.Nikahisi mwili kufa ganzi.Nilijiona ninaye dhalilisha hapa ulimwenguni.

“Unafurahia nikuite mume wangu,sivyo?”

“Ndio”Nikaitikia kwa sauti ambayo hata mimi mwenyewe sikuisikia vizuri.

Nikanyamaza,nilijikuta machozi yakinitoka.Kwa kweli moyo uliniuma lakini sikuwa na lakufanya.

“Sasa unataka nikuite mume wangu wakati huwezi?”

“Getruda siwezi nini?”

“Kwani umenioa ilinikupikie tu?”

“Hapana”Nilijibu kwa hofu.

“Sasa unategemea mimi nitaishi vipi?”Safari hii Getruda alishika kiuno.

“Mke wangu vuta subira,nitapona”

“Kwani unaumwa?”

“Ndio, sin’shakuambia naumwa?”Nilikuwa na kila sababu ya kumnyenyekea.

“Hivi Sweedy unataka kunifanya mtoto.Kwa taarifa yako nimeshajua siri zako.Juzi umeshikwa ugoni na mwanafunzi ukatozwa laki saba.Na nimepata tetesi kwamba unapenda hawa wa kusoma”Getruda alinishikia kibwebwe.

“Huu ni uzushi wa watu wasipenda niwe nawe.Naomba usisikilize maneno ya wafitini”

“Sio wafitini.Niwatu wanaokujua kwa ukaribu tabia yako”

Zogo lilikuwa kubwa ambalo lilichukua masaa sita.Baada ya hapo mke wangu akaondoka kwenda mjini.

Hakuwa na safari bali aliamua kwenda mjini kununua gazeti la Mwanasport, lililoandikwa mwongozo wa kumridhisha mwenzi kiunyumba, na kuliweka kwenye meza makusudi ilinilione.

“Haya nakuuliza umesoma gazeti nililokuwekea kwenye meza?”

“Gazeti lipi mke wangu?” nilimuuliza kwa sauti ya chini.

“Hili hapa” mke wangu alinionyesha huku akinipatia nisome.

“Mwongozo wa njia za kumridhisha mwenzi kiunyumba”

“Aaaaa! Gazeti hili, kipengele hiki nisha soma….” Nilijaribu kuchangamka kijanja, lakini huzuni ilibaki pale pale.

“Uongo” Getruda alinishupalia

“Haki ya Mungu, nimesoma kipengele hicho tena kinasisitiza swala la unyumba, mume amtendee haki mkewe na mkewe amtendee mume haki yake, tena hii hapa….” Nilijaribu kujitetea kwa unafiki.

Nilichukuwa gazeti lile na kupitisha macho juu juu kwa haraka na kumwambia nimesoma ndani vizuri. Nilifahamu sana nia yake haswa ilikuwa ni nini? Nilimtizama mke wangu kwa masikitiko na kumuonea huruma, lakini ningefanya nini ili kumridhisha, nae aridhike japo mara moja.

“Samahani mke wangu siku hizi na choka kwa shughuli nzito si mchana wala usiku, hata nimesahau kufanya mapenzi nawe”

“Hivi wewe unavyosema siku hivi, ina maana toka tufunge ndoa, tumeshafanya chochote na sasa karibu miezi miwili na nusu?”

“Basi ni samehe mke wangu”

“Nikusamehe kwa lipi?. Usinipotezee muda ninachoomba ni haki yangu bwana”

“Naomba unipe muda wa wiki nzima”

“Sitaki, ninacholilia ni haki yangu.Kwani kanisani uliapa kwamba utanitendea hivi. Ulinioa wanini kama hukunipenda, naomba talaka yangu haraka…”

“Umeenda mbali sana mke wangu…”

“Mimi sio mkeo kuanzia sasa. Naomba uelewe. We mwanaume gani?”Getruda alionekana mwenye hasira ,nikaamua kutulia kama niliyenyeshewa na mvua.

Akrabu za saa zilionyesha saa tisa na robo usiku, mke wangu alijawa na fukutiko la moyo lililokuwa zito, japo alikuwa na hasira lakini alijitahidi kuiondoa ili kunitamanisha. Muda mfupi aliingia chumbani na kufuata kabati lake lenye makorokoro yote ambayo yanampendezesha mwanamke kuwa kivutio mumewe au mchumba au mwanaume rijali. Alichukua muda kidogo akijipodoa na kujipara, mafuta sijui lotion, cream, manukato, wanjaa lipshine nk. Hakuishia hapo alivaa sketi fupo, ambayo wanaita kimini kilichoonyesha mapaja yaliyonona, na kibilauzi kifupi, wengi huita “kitopu” chenye kuonyesha kitovu kilichoumbika sawia, usoni alipaka poda kwa mbali na kujipulizia manukato yenye harufu ya mahaba. Mke mwenye sura mufti, nyororo kwa macho ya kuita japo mke wangu alijitahidi kwa vitu vyote hivyo lakini ilikuwa sawa na kupiga kinyago ukwenzi, nilibaki kama zoba na mbege.

Juhudi zote za kujipara manukato, tabasamum nono! Nilibaki kuwa sikuuwona uzuri ule, kumbe ni kwasababu nilikuwa siyawezi. Uzalendo nae ulimshinda, ndipo alipaanza kuuliza.

“Mume wangu urembo wote nilonao bado hunitamani? niambie unanipenda au hunipendi” “Nakupenda”

“Sasa kama unanipenda mbona hunifa…” alizidi kulalama kila siku, kila dakika, kila sekunde.

“Nisamehe mke wangu ongea taratibu jirani watasikia”. Niliongea kwa sauti ya chini nikiwa nimempigia magoti mke wangu, sikupenda jirani watambue udhaifu nilionao.

“Nirahisi kupata msamaha wangu, lakini nataka ufanye ninachokuambia, umenielewa mume wangu” mke wangu alipunguza ukali kidogo na kuanza kupitisha mkono wake wa kushoto akipapasa kifuani mwangu.

“Haya twende tukatizame mkanda wa X kwenye video ya chumbani” mke wangu aliongea kwa kunibembeleza, aliamini yeye kama mwanamke lazima ambembeleze mumewe,amfanyie vile vitu anavyopenda ili penzi likomaa na kufika kileleni.

Tulifika chumbani nilijitupa kitandani kigoigoi, roho ikiniuma “Ugonjwa huo wa kuuwa nguvu za kiume niliupata wapi? Au huyu mke ni jini nini? Mbona nimemuoa na uume wangu kukosa nguvu, kwanini? Mbona jenifer nilimridhisha vya kutosha. Mama mkwe kaniloga nini?. Hataki niwe na mwanae” Alitoa mkanda kwenye droo za kanda kisha akasema “Mkanda huu nimeaununua kwa ajili yako. Najitahidi kila namana kukuvuta jirani nami mpenzi” Getruda aliongea huku akitoa tabasamu nono.

“Halafu baada ya kuangalia nini kiendeleee?” niliongea kwa wasi wasi mkubwa tena kwa kuropoka, nilihisi kuchanganyikiwa.

“Kwani wewe umenioa niwe nani kwako, au nifanye nini. Niambie sio kuropoka maneno yasiona maana” Getruda alizidi kufoka.

“Vitu vingine vinaleta kero, sijui huyu ni mzigo, au nini?” Getruda alijisemea kimoyo moyo.

“Basi yaishe mpenzi, punguza hasira”

“Ooo! Kumbe ulikuwa unataka tujifunze kitu”

“Ndio, ili tujifunze wazungu wanavyoridhishana”. Getruda alipunguza hasira kidogo yote hayo ni kunifanya nisisimke.

“Kaaa! Pamoja nami?” Kwa kweli nilichanganyikiwa kabisa, nilikkuwa nikiropoka maneno yasiona msingi, hata nilivyomjibu aliniona limbukeni.

“Kwani ajabu, ndio nikae nawe!” Getruda alizidi kushikwa na hasira usiku mzima hatuku lala ni kukoromeana, maneno ya lawama na mengine ya kuomba msamaha.

“Nikae na wewe tu?” nilizidi kumyumbisha kwa maneno ya ajabu ilimradi papambazuke niondoke mikononi mwake. Nilitamani pakuche niondoke niende kazini.

“Hukubali eee!, niambie hutaki?”

“Aaaaa! Na kubali kabisa bila hofu” jibu hilo lilimfurahisha Getruda mke wangu aliamini ningefanya mapenzi muda mfupi.

“Basi vizuri, nitashukuru mume wangu, na nitakupa unachotaka, japo sijawahi kufanya ngono lakini nitakuachia ufanye utakavyo taka.” Mara moja alianza kuimba

“Basi mume wangu Sweedy, wewe ni wewe sina mwingine, kama ni kundi la ndege msituni basi wewe ndio chaguo langu, wengine sioni, nakupenda peke yako naomba uangaze pendo letu ling’are giza,…” Alitunga wimbo wa muda mfupi.

Getruda, mke wangu alinifuata kitandani baada ya kuweka mkanda wa mapenzi, alinikumbatiam tukaanza kuviringishana huku na kule. Lakini wasi wasi ulinijaa pale nilipo kumbuka mapenzi na mke wangu, niliamini hakuna chochote kingeendelea zaidi ya kumtesa Getruda. Wala sikuwa tayari ajue udhaifu wangu, nilihofu pindi angejua basi angeomba talaka, hata hivyo siri ingekuwa hadharani, kila kona ya dunia.

Baada ya kuchoka mabusu, alilala kwa chali akiwa ananitizama, kwa hofu nilitizama pembeni, sikuweza kumuangalia usoni.

“Niangalie basi nijue unanipenda” nilipomtizama kwa kujikaza, nilisikia akisema (Ooooohhh! Honey you look at me, without uttering any word”) “Ooooohhh! Mpenzi unanitizama bila kunena neno!” Nilituliza macho uso mwa Getruda, uso ulijaa ubembe. Ingawa nilifahamu shauku ya mke wangu lakini nilishindwa nimfanyie nini ili nionekane kidume na mume hodari, sio sifa ya kuoa tu ndoa Kanisani. Lakini lazima nimburudishe mke wangu hata kwa kumshika shika maungo yake, ili kumtuliza asionekane mwenye sikitiko moyoni.

Hata hivyo mke wangu hakuchoka na vitimbi vyangu, aliendelea kunishika shika, ili kuniondoa uchovu. Aliona muhimu na dawa ni kwenda na mimi bafuni kuoga, tulienda bafuni na kuanza kuoga pamoja, lakini hakuona uume wangu ukisisimka hata kidogo. Hofu ilianza kumuingia hakuamini alivyonihisi aliona ni uchovu tu wa kawaida. Hakuwa na roho ya kukata tamaa, kule bafuni alijitahidi kuushika na kupapasa maungo yangu, sikuonyesha dalili yeyote ile.

Getruda akaniogesha nami nikamuogesha.Tulipomaliza akachukua sabuni na bush la kuogea tukaelekea chumbani tukiwa tumefunga taulo. Getruda alionekana kuwa na hasira kali moyoni.

“Mume wangu naona hunipendi kutoka rohoni, Bali ulilazimishwa na wazazi wako sio hivi hivi ni miezi miwili sasa inatimia toka unioe hutaki kufanya tendo la ndoa. Heshima ya ndoa iko wapi? Naomba unieleze kama hinitaki niondoke au nini kimekusibu?”

Wakati ananielezea machozi yalikuwa yanambubujika, aliamini kulia sio suluhisho, taratibu alifuta machozi kwa lesso, alinisogelea karibu na kunizungushia mikono kiunoni, huku akininong’oneza “Sweedy kuna kitu chochote nisichokuridhisha mume wangu. Naomba unieleze niweze kujirekebisha. “Tafadhali niambie sasa hivi. Nahitaji kujua, nitaishi vipi bila mapenzi yako?”

“Kila kitu unaniridhisha ila ni…ni…nina…ni….” nilikokoteza maneno yaliyochanganyikanana kigugumizi, nilishindwa kutamka vizuri nilihisi homa kali, nilijua ndoa ingeingia dosari.

“Ila una nini?. Sema mbona humaliziii?” alinikaripia kwa sauti.

“Unaumwa?” aliniuliza.

“Aaaa!, hata kidogo,” nilimjibu kwa sauti ya chini,

“Au…..penginenimekuudhi bila mimi kufahamu…., maana mama husema mimi ni mkaidi na sijui namna ya kumtunza mtu, ni kweli?” Getruda alizidi kunidadisi.

“Hapana” niliitikia kwa sauti ya majonzi.

“Oke, hivi ni kusema kwa sababu ya kazi ndio umenisogeza pembeni?”

“Hivyo ni vibaya mke wangu, nakuahidi nitajitahidi kukupa penzi nono!, ambalo litafuta kumbukumbu zote nilizo kukera”

“Kama sivyo, basi naomba unibusu, nijisikie furaha moyoni” mke wangu aliongea huku akinisogelea karibu zaidi.

Nilisita kidogo kisha nikainamisha kichwa na uso kutokeza upande wa midomo yake na kumbus kwa uvivu uvivu (Kigoigoi). Nilipomgusa tu midomo yake, mara alinikumbatia vilivyo, kwa mikono yake na kuning’ang’ania na mabusu ya mfululizo na muda mrefu na hata aliponiachia hilihisi joto lenye uvuguvugu nikilikosa. Mwanzoni nilimbusu kwa wasi wasi na shingo upande, lakini baadae nikaadhiriwa na mabusu motomoto ya Getruda nikajikuta ashiki zikiwa zimesisimua mwili mzima, nilijibu mashambulizi kwa mabusu ya nguvu huku nikihema roho juu juu.

Baada ya mabusu yaliotuweka hali ya mapenzi, kwani ashiki zilimpanda na kutaka penzi wakati huo huo bila kucheleweshwa. Akrabu ya saa ya ukutani ilionyesha saa kumi na moja na nusu, karibu na kupambazuka. Majogoo yalikuwa yakiwika kila kona ya wafugaji wa kuku.

“Mume wangu sikiliza” Getruda aliniambia, usoni macho yalikuwa yamelegea na kurembua rembua.

“Eee! Sema mama watoto” nilikohoa kinafiki na kusema.

“Karibu kunapambazuka. Nataka uondoe mawazo ya biashara, madeni, sijue kazi mawazo yako yote weka kuhusu penzi langu na wewe, naomba uniridhishe kwa penzi motomoto.Kwani siku sitini sasa toka unioe hujafanya tendo la ndoa na mimi. Hivyo leo ni mwisho, usipofanya tendo la ndoa, talaka yangu naomba, siwezi kukaa kama pambo, katuni ndani ya nyumba yako. Sijaja kukupikia hapa tumbo liende mbele, mimi sio kijakazi wako, uelewe leo, mimi ni mkeo tena wa ndoa” Getruda alibadilika ghafla na hakutaka kucheka na mimi, alikua anahitaji haki yake.

“Hayo yote uliyosema nimeyatia akilini ila naomba unipe mu….” Kabla sijamalizia maneno, nilikatishwana sauti ya ukali ya Getruda.

“Nikupe nini?, mbona sikuelewi?”

“Fahamu kwamba ninahitaji kuwa na mtoto . Nataka nami niitwe mama Fulani, si jina langu Getruda” Getruda alizidi kunifokea, nilishindwa kuelewa ninani aliyekuwa ananitesa kiasi hicho.Niliwafikiria wabaya wangu wote akilini sikupata aliyenitendea ushenzi huo.

“Ndio…” niliitikia kwa sauti ndogo na ya huruma hata mimi mwenyewe sikuamini ilitoka kwenye kinywa changu, wasi wasi ulinijaa moyoni, nilihisi kuumbuka niliwalaumu wazazi walionitafutia mke. Laiti ningelijua kuwa nina matatizo hayo nisinge Kubali kuoa.

“Haya nenda ukazime taa basi basi mpenzi” Getruda alizidi kunifanya miguu ilegee na kukosa nguvu ya kutembea, nafsi ilinyauka kama jani la tumbaku lililosubiri kusagwa, jasho la woga lilinichuruzika. Sehemu ya kuzima taa ilikuwa karibu kama hatua tatu lakini niliona umbali wa kilometer ishirini.

Nilijikamua kikakamavu na kuinuka kwenye kitanda, kwa uvivu nikajongea kwenye swichi ya taa. Kilikuwa kitendo cha sekunde tano lakini nilifanya dakika saba.nilipofika kwenye swichi nilizima taa, mwili ulikuwa ukitetemeka sio kwa baridi bali ni hofu juu ya kufanya tendo la mapenzi na Mke wangu.

Nilitamani kumfukuza mke wangu kwa kero nilizopata si usiku wala mchana, lakini nilishindwa nianzie wapi na niishie wapi?. Licha ya kushindwa kumfukuza,niliogopa siri ingefichuka na kila mwanadamu angenitupia jicho la lawama.

Nilibuni haraka haraka mbinu za kuinusuru ndoa yangu,ili Mke wangu asigundue matatizo niliyo nayo,nilirudi kitandani na kijisogeza ukutani mwa kitanda,taratibu niliingiza vidole vya mkono wa kulia kwenye mkono wangu,mwisho wa kinywa karibu na koromeo,na hazikupita sekunde nane,nilitapika mfululizo. Sehemu ile ya ubavu wangu kwenye kitanda.Niliamini kwa kufanya hivyo mke wangu angeanini kuwa mimi ni mgonjwa. Lakini cha ajabu alianza kunivua nguo zangu badala ya kufikiri njia ya kuondoa matapishi kitandani, alianza kunivua suruali. Alichoka na maneno yangu ya kila siku nikilalamika, kuumwa,mara tumbo, kichomi, kutapika, kichwa nk.

Baada ya kunivua nguo, alivua na za kwake pia. “Maji ukiyavulia nguo huna budi kuyaoga”alisema kwa sauti iliojaa hasira na mahaba. Mapigo ya moyo wa Getruda yalianza kwenda kasi na mwili mzima ulisisimka baada ya kunivua nguo zote.

“Leo lazima, sijali kuumwa kwako au laa!,Kila siku unalalamika, tumbo, kichomi, kutapika, mara uchovu, leo ni leo”. Taratibu alianza kunitomasa wakati huo nilikuwa nimetulia kama yule mdudu kifaulongo na minong’ono ya kuweweseka kama mgojwa niliendelea kuitoa.

“Mume wangu amka basi tufanye.” Getruda alinihimiza huku akiwa amenishika mkono wangu kidogo akininyanyua .

“Subiri kidogo naumwa na homa”

“Imekuwa homa leo” kwa kweli mke wangu alichoka na idadi ya magonjwa niliokuwa nikimtajia kila leo.

“Eti homa, utashaa leo, sikusikilizi ninachotaka ni penzi tu, usiniletee hadithi za riwaya, zile hadithi ndefu za kubuni, sizihitaji kabisa!, wewe mwanaume gani? Hivyooo!” Getruda mke wangu alianza kunidharau baada ya kuona sina lolote. Nilianza kulia nikilaumu ugonjwa ulioniingia nikiwa na ndoa yangu, niliulaani ugonjwa huo nilitamani nikatwe vidole kuliko kuwa na udhaifu wa nguvu za kiume. Kilio changu kilikuwa chungu mwenye na roho yangu. Pamoja na kunywa dawa za mitishamba kutoka kwa wamasai aina ya mchuma mbele bado nizidi kupata mateso ya unyumba.

“Mke wangu unadiriki kunikashifu. Kunitukana mtusi ya nguoni!, kweli umenichoka” nilijaribu kumlaumu mke wangu, lakini haikusaidia kitu.

“Ndio, nimekuchoka, naomba talaka yangu asubuhi hii hii, longolongo sitaki” mke wangu alibadilika ghafla na kunitizama kwa hasira kali, kama kungekuwa na uwezekano wa kuniadhibu basi angeniadhibu ipasavyo. Niliona bila kuwa mpole ndoa ingekuwa ndoano, ingesambaratika na ningekuwa mseja.

“Mke wangu naomba upunguze jazba nikueleze…” niliongea kwa sauti ya unyonge iliyona lengelenge la machozi kunitoka, nikiwa na wasiwasi mkubwa wa kumkosa Getruda. Sikupenda niachane na Getruda mke niliyepewa na wazazi, mke mwenye hali ya ubikira, ambaye hajawahi kuguswa.

“Nimeshachoka na mambo yako ya ajabu, unataka kunieleza nini?”

“Najua utanichukia nikikueleza kilichonisibu pia hutaamini yaliyonikuta mwenzio”. Niliongea machozi yakinilengalenga machoni, roho iliniuma na kujiona nisiye na faida wala umuhimu kuishi duniani, nilitamani kufa ilinisiendelee na mateso. Kilio changu kilikuwa cha huzuni mno!, moyo wa huruma ukamuingia mke wangu, masikini akaniomba nimuelezee.

“Mume wangu haya nielezee kilicho kusibu, usiogope kuwa wazi usinifiche chochote kama kuna uwezekano nitakusaidia mpenzi” sauti ya mke wangu niliisikia na kuifananisha na sauti ya malaika wa neema. Nikajikaza huku nikiwa na churuzika machozi yaliyolowanisha kope machoni.

“Mke wangu hujafa hujaumbika, nisikilize kama mtu asikilizavyo maneno ya Mungu, nilikuwa kiwandani kwenye uchanganyaji wake Kemikali, bahati mbaya kemikali yatindikali ilinidondokea kwenye ngozi karibu na uume wangu na kunisababishia udhaifu mwilini, naomba usiniache mpenzi, naomba unisamehe kama nimekukosea mpenzi, naamini nimekukosea. Sikuyataka bali yametokea bahati mbaya” Niliongea uwongo uliofanana na ukweli, kadri nilivyozungumza ndivyo nilivyozidi kulia, sikupenda kuongea uwongo bali ilinibidi niongee uwongo mtupu ilikuinusuru ndoa na aibu yangu , sikumwangikiwa na tindikali, ni ugonjwa ulionitokea ambao sikujua ulitokea wapi na nani aliyeniletea ugonjwa huo, je ni Jenipher au ni nani?”

“Sasa kama ulikuwa unajua unamatatizo kwanini ulinioa mpenzi?, unanitesa, umepoteza muda wangu bure” Getruda alizidi kulalamika japo alinionea huruma.

“Kumbe ndio maana kila siku ana lalamika na kunitajia magonjwa mengi yote hayo ni kukwepa…” Getruda aliwaza akilini.

“Mke wangu matatizo yalitokea siku tatu kabla ya ndoa, wala sikujua nimeadhirika na tindikali hiyo, ningejua ningehairisha kufunga ndoa ili upate mume rijali” maneno yangu yalimuingia Getruda mke wangu na kuamini kuwa ni kweli nilipata ajali ya kumwagikiwa na tindikali.

“Nitaishi vipi bila kupata matunda ya ndoa, naomba uniambie nitaishi vipi?, nitaishi hivi mpaka lini, sijawahi kukutana na mwanaume, nilitegemea wewe ndiye ungevunja boma langu, sasa itakuwa vipi? Naomba mawazo yako” macho ya huruma yalitua usoni mwangu, niliyekuwa nimetulia kama mtuhumiwa aliyesubiri hukumu ya kunyongwa.

“Mke wangu hilo usitie shaka. Hakuna kinachoharibika nivumilie kidogo”

“Siwezi kukuvumilia tena mume wangu. Naomba talaka haraka”Nilitamani kuondoka , ikiwezekana kuihama nyumba yangu,nikifikiri jambo hilo lingenisaidia lakini nikajikuta nikikatisha mawazo na nafsi.Nilitulia kama sekunde kadhaa hivi nikijaribu kuganga maumivu.

“Uliapa mbele ya mchungaji kwamba utaishi na mimi kwa uvumilivu…”Kabla sijamalizia maneno yangu , nikakatishwa na sauti ya ukali .

“Ndio. Nimevumilia nimechoka, naomba uelewa kwamba namimi nina homoni”Getruda akasema akinitizama kama mtu alieniandalia tusi.

“Nataka niende nchi za nje kwenda kufanyiwa uchunguzi zaidi”

“Nchi gani?”

“Uingereza….” Nilipumua kidogo kisha nikaendelea kumweleza, wakati huu nikimueleza, nilikuwa siamini kwamba angeweza kulielewa lile nililotaka alifahamu na kulitii “Getruda nakupenda na kiliwaahidi wazazi wangu nitaishi na wewe hadi mungu atakapo chukua roho zetu”

“Sweedy unajua maana ya ndoa kweli?”Getruda akaniuliza akiwa amenitumbulia macho.

“Ndio”Nikajibu kwa sauti ndogo na ya upole kabisa,nikiwa nimeinamisha kicha kama kondoo.

“Kama unajua maana yake.Mbona sioni nini maana ya ndoa kati yangu na wewe?”Hapo nikavuta pumzi ndefu na kuziachia kwa nguvu, “Ooooopphhhh”.Ikafikia wakati mwingine hata kujionea mwenyewe huruma.

“Si nishakuambia tatizo langu?”Nilizidi kutukutika moyoni.

“Basi kama unataka nisivunje ndoa yetu nitafutie ndugu yako aniridhishe kimapenzi mpaka utakapo pona”

“Sina ndugu yangu wakiume mke wangu.Kwa nini usiwe na subira?”Machozi sasa yakaanza kunidondoka kama maji ya dripu, nilihisi kudhulumiwa haki yangu , ingawa nilitaka njia ya amani kati yangu na mke wangu.

“Ngoja ngoja yaumiza matumbo”nilimtizama Getruda, mke wangu nikagungua hakuwa na nafasi tena ya kunisubiri. Macho yake tu, yalikuwa jawabu tosha kwamba angeondoka kwenda kutafuta mume mwingine.

“Nasubiri unijibu upesi, sitaki mzaha tena. Ushanipotezea muda mwingi sana Sweedy”Sauti ya kupaza niliisikia ikigonga ngoma za masikio yangu, nilijaribu kumtupia macho ya huruma,kuwa pengine angepunguza maneno. Sikuweza kumjibu chochote,badala yake nikabaki kimya kama niliyeletewa habari ya msiba wa ndugu yangu wa karibu.

“Dharau yako itakuponza. Wala sitaki talaka yako.Naondoka, narudi kwetu mwili wangu bado unaniruhusu kuolewa.Kama ni bikra bado ninayo kama ni kuzaa ndio kabisaa.Kwanini nikose mume.Uzuri wangu tosha nishahidi kwamba sitokaa kwetu mwezi bila kuolewa”Getruda aliongea na kunyanyuka kitini ambako alielekea chumbani. Nilibaki nikimtizama bila kunena neno juu yetu.Sikutarajia kuona kile kilichopo mbele yangu wakati huo.Nilimuona Getruda akiwa kabeba begi kubwa languo akitoka nalo nje varandani.

“Mke wangu tafadhali naomba uweke begi chini tuongee.Unapochukua uamuzi huo si suluhisho. Ni busara kusuluhisha mgogoro ili kuhuisha uhusiano mwema ,tangu kuumbwa kwa familia hakuna hata moja isiyopata ubishi na mgogoro ndani ya nyumba…..”nilivuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu ,ni dhahiri nilichoka kuitetea ndoa yangu isianguke.Wakati huo Getruda alinitupia jicho, begi lake akiwa kalishikilia mkononi.Nikavuta hatua na kumfikia karibu, nilimshika mkono nikijaribu kumbembeleza, “Tafadhali usinishike.Muda wa kuishi nawewe umeisha.Mume gani usiye…”Nilimkatisha maneno yake, “Ni samehe mke wangu,nitaendelea kukuita mke wangu kwa sababu nakupenda, naomba uwe na subira. Unyumba nikuvumiliana, kuna leo na kesho, kumbuka hujafa hujaumbika, jambo hili linaweza kukukuta hata wewe,pengine ukapata ajali.Sikupenda kuwa hivi mpenzi…. hili ni jambo la kawaida, muhimu ni jinsi ya kutatua mikwaruzo hii.Mfano ungekuwa wewe mwenye matatizo haya ungelifanya nini?”

Niliongea taratibu na kwa busara nikijaribu kumshauri Getruda , mke wangu. Alivuta pumzi na kuzishusha.

“Naomba unipe uhuru.Utakubali niwe naingiza mume mwenzio ndani?”

“Hapana. Utakuwa ni unyanyapaa wakijinsia.Getruda unataka kuniumiza moyo wangu.Nakupenda na nimekuomba uwe na subira,pengine nimajaribu ya mungu”Nilivumilia kulia ikashindikana,machozi yalinitoka bila kutegemea.Nilitamani nibaki peke yangu ,ingawa sikuweza kuamini kama kweli Getruda angenihifadhia siri yangu.Angeenda kuwaeleza nini wazazi wake.Kuna mtu anaweza kuvunja ndoa bila kufarakana, migogoro ya kiunyumba?.Mawazo hayo yalizidi kuniumiza na kunikera moyoni.

“Chagua moja….”Alitulia , akalamba midomo yake kisha kunitizama kwa dharau.Dharau hiyo niliigundua kwamba nikwa vile aliniona si lolote si chochote kwake.

“Unasema unanipenda sana?”

“Kwani hujui hilo?”

“Sijui kwa sababu wewe mwenyewe hujanionyeshea upendo wako kwangu”

“Hivi umesema unanipenda vile?”

“Ndio…najua umekuwa wimbo”

“Naomba unichagulie maisha nitakayoishi kuanzia sasa”

“Basi nitakuacha uchague unachotaka mpenzi bora usinidhalilishe.”

“Sina chaguo lingine zaidi ya kunitafutia ndugu yako yeyote”Alisema tena akionekana siriasi.

“Kuna rafiki yangu mpenzi ambaye tupo karibu .Yeye ndie mwandani wangu, siri zangu ni zake na zake ni zangu nitamueleza kilio changu. Naamini atakisikiliza na kulichukulia kama kilio chake na atanisaidia shida ndogo ndogo za unyumba wetu. Mtu huyo ni tajiri yangu anayeitwa Mzee Jophu. Itakubidi unihifadhie aibu hii moyoni mwako. Ndiye ambaye siku ile ulivyoletwa na Baba niliwaacheni nae nikiwa na maongezi ya faragha na Baba.” Nilijaribu kumueleza mke wangu kuwa pengine angekubali kutembea na rafiki yangu mkubwa badalaya ndugu , na aendelee kinitunzia heshima yangu kama mumewe. Japo roho ilikuwa inauma kumkabidhi mwenzangu boma langu. Wala sikuweza kugundua kuwa mzee Jophu ndiye aliye panga na Daktari anipige sindano ya sumu.

“Kama una matatizo ndoa ya nini?.Suluhisho ni kuivunja ndoa kwa amani sitaki kujidhalilisha kwani wanaume wameisha duniani? Isitoshe nilishakutaarifu kwamba sijawahi kuguswa, bado nina nafasi kubwa ya kuolewa, wameolewa machangudoa sembuse mimi kigoli. Siwezi kukuelewa kabisa ninachotaka ni talaka yangu. Kuishi na wewe ni sawa na kulinganisha kifo na usingizi” Mke wangu alinibadilikia ghafla, sikuweza kuamini maneno hayo yaliyotoka kinywani mwake . Hali hiyo ilininyima amani na kijikuta nikilia kama mtoto mchanga aliye hitaji ziwa la mama yake baada ya kulikosa kutwa nzima bila kunyonya.

“ Sijali kulia kwako kwani mimi ndiye niliye kumwagia tindikali? Mlaumu aliye kumwagia na sio mimi.Kweli ving’aavyo vyote si dhahabu. Najuta kuolewa na watu waliochelewa kuoa, huenda ni matatizo uliokuwa nayo toka zamani”. Getruda alizidi kuniumiza moyo.

“Sawa najua sina faida ya kuishi duniani,nitawaachia ninyi wenyewe umuhimu na hii dunia, lazima nife …….sio muda mrefu utaniita marehemu sio Sweedy tena ,” Nilijikuta shetani mbaya akiniingia kichwani na kuiteka akili yangu, nikaamua kujiua tu, sikupenda kuishi na mateso. Niliondoka na kuingia chumbani kwetu, nilijifungia kwandani na kutafuta kamba tayari kutoa uhai wangu. Nilikusudia kujiua na niliamua kufanya kama mawazo yalivyo nituma, sikupenda kuishi kwa manyanyaso, mateso ya unyumba.

Nilikuwa chumbani na tafuta kamba ya kujinyonga, Getruda, mke wangu muda mfupi tu, angeniita marehemu badala ya Sweedy. Getruda akiwa kwenye mtiririko wa mawazo alisikia sauti yangu, (LORD YOU KNOW MY TRIBLES)” “Mungu unajua mateso yangu”Wakati nasema maneno yale ,nilishafunga kitanzi juu ya paa la numba.Nilikuwa nimepanga stuli mbili zikiwa zimebebana,nikaanza kuingiza shingo kitanzini, nilihakikisha kamba haitakatika. Iliyofuatiwa sauti nyingine nikimuaga. “Getuuuuu! Kwa heri niagie ndugu wote, nimeamua kufa sipotayari kunyanyaswa na udhaifu wangu, hata mungu anajua”. Taratibu nilianza kusukuma stuli nilioikanyaga ili idondoke na nijinyonge, Muomba kifo hakosi basi stuli ilidondoka kamba ikaninyonga.

“Ahiiiii”nilitoa sauti moja kwa shida sana.Kutoa neno la zaidi,nilijijigeuza na nikawa natapatapa kama mfa maji.

“Haraka Getu aliamka na kuekekea sauti ilipotoka, aliamini nilikuwa nianajiua akajuta na kujilaumu kwanini alinipa maneno ya ukali badala ya kunifariji.

“Dhambi zote ni mimi, isingekuwa mimi asingejiua, yanipasa nijitahidi kumnusuru na kifo,” Getu alianza kuniita kwa sauti ya huruma, “Sweedy…Sweedy… naomba unisikilize mkeo naongea. Niwie radhi nilikuwa na kutania nimekubali kuwa na rafiki yako. Naomba unielewe mpenzi nitalitunza penzi lako na siri yako. Kama nikujiua basi nisubiri tuongee nitakuacha uendelee kujiua.” Getu aliendelea kuniita bila ya kupata kujibiwa. Kilikuwa kitendo cha haraka alichukua uamuzi wa kuvunja mlango na kuingia ndani, alinikuta nikiwa nimeningia mapovu ya kitoka puani.Aliona kisu kilichokuwa mezani,Hakupendakupoteza muda ,kwa mwendo wa umeme alikata kamba na nikadondoka chini kama gunia la maharage, aliponigusa alipeleka mkono kifuani kuona kama nilikuwa hai. Ajabu ni kwamba hakusikia mapigo ya moyo ya kienda. Miguu ndio ilikuwa nikiitupatupa huku na kule, ulimi ukiwa nje kama wa kenge. Hali iliyomfanya asijidanganye kuwepo hai tena na kuamini zisingepita dakika kumi ningepoteza uhai.

Uzito wangu haukuwa kigezo kikubwa cha kumfanya Getruda ashindwe kunibeba, alijitahidi alivyo weza kunitoa nje ambako alipiga simu kwa dereva teksi aliyemfahamu. Dakika takribani mbili ,alisikia gari likiegeshwa nje ya jengo letu.

“Vipi shem. Imekuwa je?”Dereva teksi aliuliza.

“Wee achatu.Hebu tumuwahishe hospitali mazungumzo baadaye”

Walinibeba juu juu hadi kwenye gari, dereva akafungua mlango wa nyuma ambako walinilaza chali na kufunga mlango.Hawakukawia kufika hospitali ya rufaa Mount meru kwa matibabu zaidi.Getruda aliniingiza ofisi ya dakitari wa zamu.

“Anasumbuliwa hasa na nini?”

“Amevamiwa na majambazi ambao walimnyonga kwa kutumia kamba”Getruda alidanganya wazi wazi.Huku akiuma mdomo wa chini kana kwamba alijawa na dhahabu kali.

“Sasa umeripoti polisi?”

“Daktari mbona unaniuliza maswali ya sio na msingi kabisa.Wewe unataka ripoti ama kumtibu mgonjwa?”

“Hatuwezi kutibu bila kupokea karatasi ya PF3 kutoka polisi”

“Dokta kipi bora .Kuokoa maisha ya mgonjwa ama kumwacha afe kwa sababu ya PF3?”

“Kuokoa maisha yake”Dokta akajibu akichukua vipimo vyake.

“Basi kumbe unajua. PF3 baadae, nisamehe kama nimekuudhi”Getruda alimwomba radhi Dokta.

Dokta alinishughulikia kwa haraka.Nilitibiwa kwa makini na baada ya saa nzima nilipata ahuen.Ila kooni nilihisi maumivu kwa ndani.

**********

Zikawa zimepita Siku mbili toka nilipookolewa na Mke wangu,Getruda pale nilipokuwa najiua kifo cha taabu.

“Mume wangu nilikuwa nikikutania . Tafadhali usijaribu kujiua tena. Nimekubali mlete huyo rafiki yako leo nimuone kama sura yake ina tapisha au laa!” Getruda hakupenda kufanya hivyo aliamua kukubali ili kuninusuru kifo. Sauti ya Getruda ilipenyeza kwenye ngoma ya masikio yangu fundo kali la sononeko liliingia moyoni.Nikajivuia kulia kwa nguvu zote lakini nilijikuta machozi yakichuruzika taratibu bila kujua.

“Sawa mke wangu utamuona nitakapomleta jioni,” Ilikuwa asubuhi na mapema, majira ya saa moja na nusu.

“Mmmm! Lakini Getruda unanipenda.Isingekuwa wewe basi nilikuwa mfu”Nilimweleza Getruda.

“Kumbe unalijua.Mkojo ulishaanza kukutoka”

“Masihara hayo.Inamaana nilikikojolea kama mtoto”

“Ndio”Getruda alinijibu akainuka kitini na kuelekea kwenye jokofu ambako alilifungua na kunipatia Juisi baridi ya machungwa.

“Karibu mpenzi”

“Ahsante mpenzi”Niliipokea na kumtolea tabasamu,lakini nilipokumbukla kwamaba nahitajika kumtambulisha bosi wangu.Moyo ulisingaa na kunyauka kama jani la tumbaku lililosubiri kusagwa.

“Mpenzi nataka kwenda kujipumzisha kidogo”

“Sawa,ila usisahau kwenda kumleta rafiki yako jioni”Nilishituka na kutulia kama sekunde kadhaa ,kisha nikageuka kumtizama mke wangu.

“Utaniamsha baada ya saa moja.

Ok, bye”Nilijikaza kutoa tabasamu ambalo pengine lilionekana dhahiri la kulazimisha, huku moyo ukiniuma kama kutu inavyokula chuma taratibu na kukiozesha chote.

“Nije tujipumzishe wote?”Getruda alinieleza wakati nikiwa nimempa mgongo.

“Poa. Ukipenda”Nilimjibu damu zikienda mbio ,ungeweza kuhisi nimekimbia umbali mrefu bila kupumzika.

Getruda alinifuata chumbani kama alivyoomba.Nilijitupa kitandani kiuvivu uvivu nae akajibweteka kwenye sofa moja lililomo chumbani.Ingawa nilifumba macho lakini sikuwa hata na lepe la usingizi, mawazo yangu yalimezwa na taswira ya maisha ya unyumba.Nilijiuliza bila kupata jawabu sahihi kwamba ugonjwa huwa niliupata wapi na nani aliyenipa?.

Nikiwa nimelala nilihisi vidole laini zikitalii mwilini mwangu.Hata hivyo sikushituka kwani nilihiosi alikuwa mke wangu.Vidole hivi vilizunguka huku na kule bila kupumua,nilihisi kama kero ama mdudu fulani akinitembelea akini kwarua. Sikuona raha zaidi za mateso tu.

“Hallo Sweedy”

“Na..a.amu”Nilikokoteza maneno,nikiwa nimetulia utadhani mbwa anayetolewa kupe.

“Unanipenda?”

“Saaana tu”

“Kwanini hunipi haki yangu kama kweli unanipenda?”

“Haki ipi?.Si una jua matatizo yangu sasa unataka nini tena”

Nilihisi Getruda akinitibua akili yangu.Niliinukla na kutoka nje.

“Getruda unanitesa. Tumepanga nini na wewe unataka nini?”

Nilitulia kidogo nikaendelea, “Moyo wangu unasononeka sana. Laiti ningelijua nisingeoa, maisha gani haya yananitesa kiasi hiki?”Nilijikuta nikilia ovyo kama toto jinga lenye kudeka ovyo.Kilio changu lilikuwa rohoni.na aliyejua alikuwa muumba pekee.Getruda alikuja kunibembeleza kwa hofu kwamba ningechukua maamuzi ya kijinga tena. Aliniandalia chakula mezani.Tulisali kisha tukala .

Saa nane mchana baada ya kupata mlo wa mchana nilimuaga Getruda nikiwa naelekea ofisini kumueleza Mzee Jophu yaliyosibu katika unyumba wangu. Lakini cha kushangaza Mzee Jophu baada ya kumueleza kila kitu,nilimuona uso ukiwa umejawa furaha badala ya kunionea huruma. Hali hiyo aliisubiri kwa hamu hata hivyo alishanga kuona mimi kuchelewa kumuelezea shida zangu toka mwanzoni.Alijifanya kama hataki kuchangia mapenzi ilinimuone mtu mwema,

“Sasa Jophu unakataa nini na wakati nimekuambia mke wangu hajaguswa”

“Inamaana siku zote hizo mlikuwa mkilala tu?”

“Ndio”nilimjibu nikahisi machozi yakinilengalenga, hata hivyo nilijikaza kiume.

“Matatizo haya yalikupata muda gani?”

“Siku ya kwanza toka nifunge ndoa na mke wangu”

“Usinitanie Sweedy. Ulijaribu kwenda hospitali?”

“Ndio.Nilichunguzwa kwa makini.Daktari alinieleza kwamba nilipigwa sindano yenye sumu.Nilikataa kwani sijawahi kupigwa sindando yeyote toka uliponiajiri. Na sasa ni miaka karibu ishirini na tano. Nakumbuka sindano ya mwisho nilichomwa nikiwa na chuoni. Na siku nyingine niile nilipokuja kutolewa damu”

“Kutolewa damu si kupigwa sindano labda una matatizo mengine kiafya.Vipi kuhusu chango?”

“Sina chango,mzee”Nilimjibu nikiwa nimetizama chini.

“Mzee, naomba unisaidie kuokoa jahazi la ndoa yangu”Nilimweleza nikimpigia magoti.Sikuwa najua kwamba mzee Jophu ndiye aliyetuma watu wanipige sindano ya kuua uume wangu.Wakidai wana nitoa damu ilinikapimwe virusi vya ukimwi.Hata hivyo ilikuwa kazi kumgundua mbaya wangu,jinsi alivyoonyesha kutokutaka kuchukua jukumu la kumridhisha mke wangu.

“Mkeo atakubali kwenda kupima damu zetu?”

“Sina uhakika kama atakubali au laa. Ni vizuri kimpigie simu”Nilitoa simu yangu ya kiganjani na kubonyeza namba za Getruda, mke wangu.

“Hallo, mpenzi”alipokea tu baada ya kuona namba zangu juu ya kioo cha simu yake.

“Oooo!, vipi upo salama.”

“Ndio. Sijui wewe”

“Shwari kabisa.Mmmm…utakubali kupima Virusi vya ukimwi?”

“Tangu lini kigori akawa na Ukimwi?”

“Sijambo la ajabu kwani ukimwi unaambukizwa kwa kujamiana tu?”Getruda aitafakari akajiona kweli alibugi sana.

“Sawa, nimekubali kupima afya kwa manufaa yetu sote”

“Ok, jiandae nakuja sasa hivi nyumbani”

“Ok, bye bye”Alinaga na kukatasimu.

“Nilimtizama mzee Jophu na kumwambia, “Amekubali kupima”

Kwambali niliona tabasamu la mzee Jophu lililonifanya nione meno yake ya rangi rangi, nafikiri kutokana kunywa maji ya Arusha tokea utotoni mwake.

“Sasa Sweedy”Alitulia kidogo na kukohoa kinafiki,nilimtizama kwa makini niwezekujua alichotaka kusema,aliendelea “Kwa vile wewe ni rafiki yangu sina budi kukusaidia.Ila nakuomba usimweleze mtu yeyote ‘Especial my wife’,Umenielewa. Narudia tena naomba iwe siri moyoni mwetu”

“Sawa, mzee.Usihofu kitu”nilimjibu kwa upole kabisa.

Mzee Jophu aliongea moyoni akiwa amejawa furaha kubwa mno, “Kile nilichokitaka kimekamilika. Sasa kazi kwangu kurina asali nitakavyo””

Mzee Jophu kunajambo la muhimu nimelikumbuka. Nilimdanganya kuwa nilimwagikiwa na tindikali. Akikuuleza mueleze ni kweli”Nilitulia kidogo, ingawa alijaribu kuficha furaha niliiona , Nikatulia kama niliyewaza kitu ,Machozi yakaniwakia pale nilipokumbuka nguvu zangu nilipokuwa Nchini Thailand “Lakini boss na shindwa kujua ugonjwa huu niliupata wapi na nani aliyeniletea”

“Usijali muombe mungu akuondolee. Hatamimi ninafanya tu, kwa vile wewe rafiki yangu wa damdam, lakini kwa maulana ni dhambi kuzini nje ya ndoa,” Mzee Jophu aliongea ilinimuone mtu wa busara kama alivyoonekana kuwa ni mtu wa busara kumbe ni muungwana wa ngozi tu, lakini rohoni ni muuwaji. Maneno yake ilikuwa vigumu kumgundua kuwa yeye ndiye mbaya wangu, aliyeamua kunitesa iliamfanye mke wangu wake.

Mazungumzo yetu ya ofisi yalikuwa ya muda mrefu. Tulipo maliza jioni iliwadia tuliongozana na Mzee Jophu moja kwa moja hadi nyumbani kwangu.

“Lakini Sweedy kama ameoa mke mwenye uso wa mbuzi mimi sitamkubali atakuwa wako mwenyewe”

“ Hakika mke wangu utamkubali. Amekamilika kila idara. Utamsahau mama Jacob nakuambia” Nilimueleza.

“Yote tisa, kumi tutaona. Nitaamini unajua kuchagua,”

“Lako jicho, yanini ni kusifie?” Niliposema, nilitamani Mzee Jophu ardhike na ombo la Getruda, lakini kitu kilichoniuma zaidi ni jinsi gani ningemuunganisha mwanaume mwenzangu na mke wangu niliyemlipia mahari.

“Inawezekana huyu mshenzi akamkataa mke wangu. Midomo yake imejaa dharau”nilijisemea kimoyomoyo huku nikibonyeza kitufe cha geti.

Getruda Kimario alifika getini na kufungua, mtu wa kwanza kuingia akiwa Mzee Jophu.Shauku yake haikufichika ,alimtupia Getruda jicho la lilo jaa ubembe.Ni hapo ndipo nilipohisi Mzee Jophu kumkubali mke wangu. Alikuwa na shauku ya kumbusu Getruda, nikipindi kirefu toka wapoteane pale ofisini kwake, na Getruda alimkumbuka kuwa yule alikuwa yule aliyempa mama yake mzazi shilingi laki tano za kitanzania iliamuowe yeye. Walitupiana macho yaliyojaa furaha macho ya matamanio ya Getruda yalizidi kumchanganya Jophu. Aliyekuwa na shauku kuupitisha usiku mwanana na binti aliyemlipia shilingi laki tano. Aliamini alikuwa na haki yakujivinjari jasho lake.

Mwanzoni nilihisi hawakumbukani,kumbe kumbukumbu alikuwa nazo na alishuhudia mama yake akipokea hizo hela.

Ulifikia muda muafaka wakuweka mambo hadharani ili nitatuliwe shidayangu. Kabla sijazungumza chochote nilipandisha pumzi na kushusha kwa nguvu kama mtu aliyechoka na pilika pilika za kutwa nzima ,”ooooooophhhh!”Kisha nikasema kwa sauti ya chini kama mgonjwa,ni kweli niliyotaka kusema yaliniuma sana.

“ Nafikiri mke wangu nilisha wahi kukutajia jina la rafiki yangu kipenzi. Ila ni vema nikalirudia leo ukiwa una muona . Aliye kaa hapa mbele ndiye Mzee Jophu. Sio Mzee kweli ni kwaajili ya mali zake ndio maana watu wanampa jina la heshima ya mzee. Huyu ndiye mwa ndani wangu ukimuona yeye ndio umeniona mimi. Shida zake ni zangu, zangu ni zake,”Nilikohoa kidogo ni kumgeukia mzee Jophu. Kijasho kilizidi kuchuruzika kwa kasi kuliko mwanzoni, nilihisi midomo kufa ganzi na kuwa mizito, nilijikuta sauti ikipotea ghafla pale nilipofikiria kumuachia mzee Jophu mke wangu.Tena hajawahi kuguswa na mtu yeyeto maishani. Kwa kweli inatia uchungu sana heri ningekuwa nimezaliwa na udhaifu huo kuliko kunikuta nikiwa mtu mzima.

“Mzee Jophu huyu ni mke wangu, kwa upande mwingine naweza kusema ni mkeo. Nina matatizo ya,,,,,,” hasira kali iliniingia moyo nikashindwa kumaliza, nilijikuta nikiangua kilio. Moyo uliuma sana.

“Kweli kweli na muachia Jophu kigoli wangu?”Nilimtizama Getruda kama vile nikimuaga, sikuweza kukwepa jambo hilo tena.Kwa kuwa lilishakuwa kero katika familia yetu.

“Naomba uwe karibu na mke wangu, kama ulivyo karibu na mkeo, lakini,,,,,,,,,,naomba unifichie siri yangu, heshima iwepo msije mkachukulia muda huo kunidharau, nami sikupenda kuwa hivi,,,”Nilikokoteza maneno kwa ujasiri .

“Ok, nashukuru kumfahamu mkeo, na nitaendelea kumfahamu vizuri, zaidi kadri siku zinavyo zidi kwenda” Mzee Jophu aliongea huku akinyanyuka kuelekea alipo Getruda. Alinishika mkono na kuunyanyua usawa wa midomo yake, hakuchelewa nilisikia sauti ya busu kwenye kiganja cha mke wake wangu. Busu hilo lilimchanganya mke wangu na kujikuta mwili ukimsisimka, vinyweleo na nywele zilisimama kwa shoti ya busu la mzee Jophu.Nilibaki nimeduwa, midomo ikiwa wazi kama sekunde kadhaa.Bila hofu wala haya, walijikuta wamekumbatiana na Mzee Jophu alisogeza midomo yake karibu kabisa na sikio akimnong’oneza.

“Kweli kwenye miti hakuna wajenzi, nitakutunza kama mlima Kilimanajaro unavyotunza Seluji yake, nitakupa chochote unachotaka, ikiwezekana nitakuoa kabisa, nakupenda siko tayari kukuacha, naamini unanipenda” Sauti ya Mzee Jophu ilizidi kumtekenya Getruda, alijikuta akitikisa kichwa ishara ya kukubali.Alishindwa kujizuia kutoa sauti za kizizima, taratibu kwa jinsi maneno ya Jophu yaliyokuwa yakipenyeza sikioni angali yana uvuguvugu, kwa wimbi lenye joto nadhifu.Mzee Jophu alimwachia na kuketi karibu nae.

Mambo yote niliyaona. Kwa jinsi roho ilivyoguguna niliondoka sehemu ile na kuingi chumbani, nilimpenda sana mke wangu, sikupenda awe mke wa shirika wala sikupenda kuona akishikwa shikwa na mtu zaidi yangu. Japo nilikuwa na wivu lakini nilishindwa kwa sababu nilipata udhaifu, ikanilazimu kuvumilia na kuhamisha macho, na kutizama pembeni.Pia hilo lilinishinda nikaamua kujiondokea kiunyonge kama kifaranga asiye na mama.

Kuondoka kwangu, ulikuwa mwanya wa Jophu na mke wangu kupanga mambo yao.

“Oke nimeamini umeumbika sawa, kama asingekuwa Sweedy basi ningekuoa mimi. Bado sija chelewa. Nina nafasi kubwa ya kukuoa”Huo ndio ulikuwa mwanzo wa usaliti wa ndoa.

“Hata mimi nakiri umbo lako ni zuri na lakuvutia. Najuta kuolewa na huyu mchovu asiye na umuhimu wowote ndani ya ndoa”

Mzee Jophu alidakia “Ni kweli, sio vyote ving’aavyo dhahabu. Vingine aluminiamu ama bati,”alitulia kidogo na kumkodolea macho yaliyojaa ubembe, kisha akanyanyua mkono wa Getruda na kumbusu kiganjani, akakohoa kidogo na kusema “Sawa, tupange tukutane wapi?”Ilikuwa ni sauti ya nzito ya Jophu ikinguruma varandani kwangu.

“Mimi naona tukutane Hoteli yake Sweedy mwenyewe, pale sea breez inn hotel ili tuwaonyeshe watu na hata wafanyakazi wake kuwa Sweedy ni dhaifu”Mke wangu alianza dharau akitaka wakutane kwenye hotel yangu, ili kunidhalilisha.

“Kesho saa kumi jioni, nafikiri utakuwa muda muafaka wa kujipumzisha,”Getruda alizungumza huku akimtolea Jophu macho ya kurembua na ya unyenyekevu.

“Aaaa!, kesho mbali. Ok kumbe saa hizo karibu giza. Sawa usikose mpenzi”Walipigana mabusu ya kuagana na Mzee Jophu alimalizia .

“Niote njozi njema usiku. Tena zilizo jaa mahaba”

“Usijali mpenzi, zote nzuri zitakuwa juu yako”Mzee Jophu alitoka na mke wangu alirudi na kunifuata kule chumbani, kwa kusema kweli moyo wangu ulipata sononeko la roho, nilibaki nikiyaganga maumivu ya moyoni.

Walipanga sehemu ya kukutana bila ya kukosa, wote walikuwa na shauku moja. Ilikuwa jioni tulivu watu walikuwa wana kunywa na kula. Alionekana Mzee Jophu akiingia na mke wangu SEA BREEZ INN HOTEL. Waliongozana hadi mapokezi, na kuandika jina la kunikashfu kwenye kitabu cha wageni, bila aibu mbele ya wafanyakazi wangu. Hata kama walifanya hivyo wasingefanya kwenye hoteli yangu, wangeenda sehemu wasio julikana.Yote walionifanyia ni kunidhalilisha.

“Jina tuandike nani Mzee” muhudumu aliongea kwa wasiwasi, baada ya kumwona mke wangu, ambaye alikuwa kama bosi wake.Mzee Jophu aligeuza shingo kumtizama Getruda, Kabla hajajibu kitu mke wangu alidakia “Andika Sweedy dhaifu”

“Hapana bosi, anatakiwa kuandika jina lake kamili .Hilo sio jina kamili” aliongea kwa sauti ya chini huku akitetemeka. Alihisi mawili, kupokea tusi ama kibao.

“Sio jina kamili.Unafahamu jina lake?”

“Sifahamu”

“Kama hufahamu , mbona unasema si jina lake kamili?”Yule kijana akaanza kutizama chini kwa hofu.

“Nimekuambia uandike jina nililokutajia,upesi”

“Mama .Siwezi kuandika jina hilo”

“Wee, mpumbavu nini!.Nimekuambia andika, kama hutaki huna kazi. Fungasha virago uondoke,”Getruda alizidi kumuamrisha sambamba na kidole alichoelekeza jichoni.

Ilimbidi akubaliane na matakwa ya bosi wake, kwa kuwa hakuwa na sauti na alijua Getruda ni mke wangu, asingefanya hivyo kibarua kingeota nyasi haraka.Walichukua chumba, kila aina ya vinywaji viliingizwa chumbani humo bila ya aibu.Kijana alishindwa kuvumilia yote aliyoyaona.Aliumia rohoni na kuona kama yaliyotendwa alitendewa yeye.Hakupenda kuona mke wa tajiri yake akifanya mambo ya kishenzi, tena ofisini kwake bila aibu.

Chumba changu kilijaa utulivu uliovunjwa na muziki wa taratibu uliosikika redioni.Nilikuwa nimejipumzisha kitandani chali, nikiwa nasikilisa mwambao ambao uliniwezesha kusikia mtu ambaye angeponyeza kitufe cha kengele getini. Mawazo yangu yalilenga matatizo yaliokabili mwilini mwangu.Hasa gonjwa ambalo limenifanya nimruhusu mke wangu awe na bosi wangu. Mara simu ilianza kuita,nilishituka na kutizama mahala nilipoiweka.Nilipoiona, nikanyoosha mkono kwenye droo ya kitanda na kuiokota upesi.Sikutizama hata kwenye kioo kuona namba za aliyepiga,niliipokea mara moja na kuipeleka sikioni.

“Hallo Sweedy hapa. Nani mwenzangu?”

Nilisikia upande wa pili ukijibu kwa kuhemea juu juu.“Mimi John naongea, Mzee nimemuona mama amechukua chumba yupo na Mzee mmoja, ameandika jina la mgeni Sweedy dhaifu” sauti ya John iliingia lakini hata hivyo nilihisi masikio kuchuja herufi.Nilishituka na kubaki mdomo wazi nikiwa nimetoa macho kwa mshangaa mkubwa.Nilihisi mapigo ya moyo yakienda kasi zaidi.

“Umesema umemuona mke wangu wapi?”

Sikuamini nilirudia kwa ukali kidogo.

“Hapa hotelini kwako,mzee”

“Khaa,nisubiri nakuja.Wala usiwashitue”

“Sawa,mzee”

Nilikata simu kwa ghadhabu kali.Sikupenda kupoteza muda, nilichukua bastola na kuificha kibindoni. Nilifungua mlango kwa upesi na kutoka varandani, nilionekana kuchanganyikiwa .Nilipofika varandani nikajikuta sikuwa nimevaa viatu.Ndipo niliporudi kuvaa.Nikiwa nje ya jengo ,nilimpigia simu dereva wa teksi niliyefahamiana nae aje kunichukua.Haikuchukua muda , niliona gari jeupe lililo pigwa msitari mweusi katikati likiegeshwa nje kwangu,nilitambua ni gari la bwana Jangala, yule dereva mashuhuri wa teksi pale soko kuu Arusha.

“Bw.Jangala naomba unifikishe hotelini kwangu.Nimesahau kidogo,hivi nikiasi gani?”

“Mzee,umsahaulifu kweli.Unaonekana mwenye mawazo mengi.Kutoka hapa njiro mpaka pale Sakina ni sh,elfu tano tu,mzee”

“Hakuna tabu.Washagari twende.Samahani nina haraka,hivyo ikakupasa kutembea mwendo wa kasi”

“Sawa, mteja kwangu ni mtukufu”Jangala alisema akikanyaga mafuta, wakati huo gari likizunguka ‘Kiplefti’ ya kwanza kutoka kijenge juu.Nilielekea moja kwa moja ilikushuhudia uzalilishaji.

“Ama zangu ama zao, heri niwaue nami nife”Nilitulia kidogo nikitafakari ,nimbinu gani nitumie ilikuwa kuwanasa wote kwa mpigo.Yaani kumkabidhi Jophu imekuwa nongwa.Ajabu ni kwamba hazijapita hata siku mbili ananidhalilisha? Kweli rafiki mkia wa fisi.

***********


Nilionekana kuchanganyikiwa badala ya kuingia chumbani nilijikuta naingia chooni nilistuka ndipo akili ilipo rejea vema. Nilichomoa bastola yangu na kuelekezea mbela tayari kwa vitachumba walichochukua kilikuwa cha mwisho kabisa. Nilipokaribia chumba, nilisikia sauti za kilio kikubwa chumbani humo.

“Oooooo! Jophu unaniumiza unaniua jamani!niachecheeeee!…nakufa!”Sauti ilikuwa nzito ilioitikia

“Tulia mpenzi niku………kuku…….tengeneze.Unana……najua….wewe ..ni mzuri sana lazima nikuoe”Mzee Jophu alikokoteza maneno kwa kigugumizi kikali akiwa kifuani mwa Getruda.

Sauti hiyo ilinilegeza viungo,nikajikuta kuishiwa na nguvu.Machozi yalianza kuchururuzika kwa kasi nilijaribu kuyafuta kwa leso lakini bado haya kukoma.Nilipitisha mkono kuhakikisha kwenye mpini wa bastola kuhakikisha kwamba ipo.Nilipoigusa nikahisi ipo,nikaitoa na kuitizama kwa uchungu sana.Nikasogeza risasi kwanye kifyatuo cha kuruhusu itoke,ilipoitikia ‘Katan’g..katan’g’Nilitikisa kichwa kwa fuhara ya kukusudia kufanya lile nililofikiri kulifanya kwa wakati huo.Nilitembea kwa hadhari mpaka dirishani walimo Getruda na Mzee Jophu.Nilijaribu kuchungulia lakini sikufanikiwa kuona ndani kwakuwa kulikuwa na pazia nzito.Lakini kwa kelele zile ,nilifikiri nikipiga risasi kwa kuhisi ningewaua kwa pamoja.Nilipozidi kusikiliza kelele zao ,niligundua walikuwa karibu na lile dirisha niliposimama.Niliuelekeza mdomo wa bastola yangu aina ya G3 rafles dirishani.Nikaingiza kidole ambacho nilitegemea kuwaulia .Kabla sijafyatua risasi,nilishikwa mkono na mtu aliyekuwa nyuma yangu.

“Kaka usiwaue.Utajiingiza matatani bure.Nenda kapumzike nyumbani,hasira hasara kaka”

Mtu huyo alinisihi akiwa ameing’ang’ania bastola.Kwanza aliniomba nitoe risasi zote zilizomo ndani ya bastola.Nilipofikiri nikaona hakukuwa na ulazima wa kubishana nae.Nilizitoa,akasema “Kaka naomba unipatie hizo risasi .Najua unahasira unaweza kufanya lolote”Nilimpatia nikijua kama ni kujiua basi naweza kutumia njia nyingine.Nilipompatia alizihifadhi mfukloni mwake. Kila nilipofikiria, niliona kuwa sio suluhisho heri kufa mimi kwa aibu niliondoka eneo lile, wahudumu walikusanyika wakinitazama kwa huruma, wengine waliniomba niende niachane nao.

Waliendelea kuvuta raha na wote waliyafurahia mapenzi yao, hasa Getruda aliamini amepata mwanaume bora, ambaye asingemdhulumu haki ya unyumba. Alitumaini na alitamani kuzaa na mzee Jophu ili kuondoa maneno ya mtaani kuwa ni mgumba, alitegemea msaada mkubwa na juhudi za Mzee Jophu ili naye aitwe mama.

Niliona Dunia chungu mithili ya shubira, kila nilipo kumbuka maneno ya Getruda na Mzee Jophu nilitamani nisitishe uhai wangu, sikuwa njia nyingine ya kuwepuka aibu ile, wakati na waza nafasi nyingine ilininyima kufanya uamuzi huo na kunitaka niwe na subira. Niliamua kunywa pombe ili kupunguza mawazo lakini mawazo yalizidi kutawala ubongo wangu kadri nilivyokunywa, niliamua kusitisha kilevi, Sononeko liliendelea kunitawala, nikajiona ni mtu dhaifu kuliko watu dhaifu wote duniani. Muda mwingine nilijaribu kufariji kuwa ipo siku mungu atasikia kilio changu na kunipa nguvu za ajabu,Maneno, “MUNGU UNAJUA MATESO YANGU” yakawa gumzo akilini kila siku.

“Yaani mke wangu ananidhalilisha kiasi hiki? Kweli yote haya ni kwasababu ya udhaifu wangu,naamini mungu atasikia kilio cha mja wake na ataniponya gonjwa hili na kunipa nguvu ili kuinusuru ndoa yangu isivunjike”Niliongea huku nikiwa nimefumba macho, kichwa nikiwa nimekiinamisha, kikiwa kina saidiwa kushikiliwa na viganja vya mikono.

Pamoja na mawazo, hasira za kudhalilishwa. Bado nilikuwa na mpenda mke wangu, nilimsubiri aje tukajipumzisha chumbani na kuongea utofauti uliojitokeza. Kila nilipotizama saa ya ukutani, niliona mshale kama unaenda mbele na kurudi nyuma, hali ile iliniadhiri kisaikolojia. Nilikuwa nikiingia chumbani na kutoka, chooni na kutoka bila kufanya chochote. Nilitamani kulala lakini sikupata hata tepe la usingizi. Nilijikuta kutomlaumu tena mke wangu,kwani yote ni kwa sababu sikuweza kumtimizia haki yake, nafsi nyingiune ilipinga na kusema “Matendo aliyofanya ni ukosefu wa adabu na kutoheshimu unyumba, kwanini asifanye siri?”.Kila nilipokumbuka macho yalijaa machozi.

*****************


Ulikuwa usiku wa saa sita na nusu, usiku mzito,Mwezi ukiwa umefunikwa na wingu zito na ukungu mkubwa ukiwa mbele yake, mwili wake ulionekana kuchoka mno!,akiwa anachechemea,mwendo ambao ulikuwa tofauti toka kumuoa.Alinyanyua mkono sambamba na jiwe alilookota na kuanza kugonga mlango kwa kishindo.Sikugonga tu pia kinywa chake kilipayuka maneno machafu bila kujali alionitende.

“Wewe mlinda nyumba umelala au upo macho?. Katika wasio na faida mmojawapo ni wewe,wajanja wameondoa boma la mapenzi. Wewe unafananishwa na shoga, mlinda nyumba. Funguaaaa”

Dharau na maneno ya kashfa niliyasikia kwa usikivu wa masikio yote mawili, maneno yalikuwa angali ya moto, nilihisi homa kali ikinitetemesha mwili, nafsi ikakata tama ya kuishi kwa maisha ya manyanyaso, udhalilishaji na matusi.

Nilifikiria na kumfungulia mlango na kumuamuru aingie ndani, Getruda aliingia kwa miondoko ya maringo huku akivumilia maumivu aliyoyasikia kwenye via vya uzazi. Macho ya dharau yalinitizama kuanzia unyayo hadi kichwani na kunipindulia midomo iliyojaa dharau kem! Kem!, hakuishia hapo alinisonya na kutema mate pembeni, akijifanya anasikia kinyaa kunitizama.

“Mambo baba wa nyumba”, akimaanisha mimi ni kama mlinzi wa kulinda nyumba, sina mamlaka na penzi lake wala siwezi kutia neno kuhusu kuchelewa kwake kufika nyumbani.

Niliitikia salamu yake kwa shingo upande, sikupenda kumuudhi mke wangu, nilitambua jinsi gani mtu anavyoumia pindi apatapo sononeko la roho. Kwa sauti ya chini na ya upweke, hasira ikiwa imenikaba kooni.

“Mke wangu umetoka wapi saa hizi, na ulikuwa unafanya nini?” Nilijizuia ili mke wangu asijue kuwa nilikuwa na hasira, hata hivyo nilishindwa kujizuia kulia, mwili mzima ulitetemeka, macho yakabadilika rangi kuwa mekundu.

“Nimetoka SEA BREEZ INN HOTEL kukagua mahesabu ya leo”. Getruda alijaribu kuongea uwongo mtupu!, bila kupepesa macho, mboni wala kope za macho, macho maangavu yasio na siri hata chembe.

“Nakubali umetoka SEABREEZ INN, lakini sio kukagua mahesabu, bali umeenda kwa mambo ya ufuska.” Hasira ilizidi kupanda kila nilipomtizama, mwili ulizidi kutuna kwa hasira na jasho lilitoka kila sehemu yenye vitobo vya vinyweleo mwilini.

“Hapana mume wangu sikuwa nafanya ufuska” maneno yake yalinichanganya, nikaamua kuchukua uamuzi ambao haukuwa akilini, niliamua kumuua mke wangu na nilikuwa na sababu za kumuua, sikuwa tayari kutupiwa jicho na jamii kwa udhaifu wangu.

Nilitoka nilipokuwa, nikaingia ndani upesi, sikupenda kupoteza muda niliokota jambia lenye makali kila upande, lenye kuwaka waka hata gizani, nililitizama na kuamini kwamba ningelipitisha mara moja ningeachanisha kichwa na kiwiliwili cha Getruda.

“Hakuna tena kumuuliza. Sio matangazo ya vifo.Nikifika ni kuachanisha kichwa chake”. Niliondoka nikimfuata alipo.

“Lazima nimuue Malaya huyu.Tukose wote, siwezi kujiua lazima nimuue leo leo”.

Nilipofungua mlango, aliniona nikiwa na jambia lenye makali, aliamini kunusurika na kifo ni asilimia mbili na zilobaki zilikuwa kifo, hapakuwa na upenyo wowote wa kukimbilia kujinasua na mauti, “Haaaa!” Alihamaki na kujikuta anapiga kelele za kuomba msamaha.Ili nisitishe zoezi la kumuua bila mafanikio yoyote, sana sana niliongeza mwendo nikimfuata, jambia nikiwa nimeliinua juu tayari kutawanyisha shingo na kiwiliwili.

“Mume wangu naomba unipe nafasi ya mwisho nikueleze yote yaliyotokea. Naomba unisamehe usitoe uhai wangu, naamini utaridhika na matokeo. Kumbuka kuna Mungu nae anayaona unayotaka kunifanyia” aliendelea kulia, akiomba msamaha huku akirudi kinyume nyume taratibu.

Nilikusudia kumuua na sura yangu ilibadilika na kuonyesha dalili za kuua tu!, moyo wa huruma uliondoka; kwania ya kumchinja kama kuku anavyochinjwa na kisu chenye makali. Nilizidi kumfuata alivyokuwa anarudi nyuma, hasira ilitawala machoni. Ilikuwa si rahisi kumsamehe kamwe!. Wakati Getruda anarudi nyuma aliikwaa kwa nyuma na kudondoka chini kwa chali, hakuwa na njia nyingine ya kujinasua na mauti, aliamua kusubiri mauti yamfike.

Nililikamata jambia vizuri kwenye mpini wake kwa mikono miwili.Kitendo chakutakakulishusha Getruda alishituka na kuzirai pale pale, aligeuza macho, nilisitisha kumuua.Nilitaka kumuua akiwa na nguvu zake zote na nilitaka afe kifo cha mateso.Nikaweka jambia pembeni na kuinama kuhakikisha kama alizirai kweli ama ilikuwa janja ya nyani.Niliposikilizia mapigo yake ya moyo yalikuwa mbali sana. Sikutaka kumpeleka hata hospitali nilitaka afe mwenyewe, si tena kumtibu, nilimchukia Getruda kwa mambo aliyonitendea.

Nililiokotajambia langu nakulirudisha chumbani.Nilimuacha pale sakaruni akiwa kalala chali.Nililitupa uvunguni kwa kitanda na kikajitupa kitandani kifudi fudi. Muda mfupi usingizi ulinichukua, niliposhtuka ni ndege waliokuwa wakiimba alifajiri. Niliamka na kufungua mlango waVarandani. Nilipochunguli niliona bado Getruda alikuwa vile vile alivyodondoka usiku. Nilishindwa kujua kuwa alikwisha kufa au laa!.Kwa vile nilikuwa mbali kidogo. Sikupenda hata kumsogelea, nilifunga mlango, nikakiendea kitanda kuendelea na usingizi.

Nikiwa usingizini nilishituliwa na mlio wa simu, nilipoipokea nilisikia sauti ya mwanaume na sauti hiyo haikuwa ngeni masikioni mwangu.

“ Hallo, vipi Bw. Sweedy?”alisema tu baada ya kusikianimepokea.

“Poa, nani unaongea”Nilimwuliza.

“Mimi Jophu, nauliza jana mkeo amerudi salama?”

Sikujibu kitu zaidi ya kuikata simu.

Baada ya saa moja hasira ilipungua, moyo wa huruma uliniingia, nilitoka na kumfuata Getruda alipo, hali yake ilizidi kuwa mbaya, damu zilimtoka puani, mapovu mdomoni. Nilimpigia simu mteja wangu Jangala aje nimpeleke Getruda hospitali,Kama kawaida Jangala hachelewi alifika na tukampakiza Getruda.

“Vipi?.Mkeo ana matatizo gani?”Jangala aliniuliza wakati akifunga mlango wa nyuma alipo Getruda.

“Anasumbuliwa na shinikizo la damu”

“Oooo! Pole sana Bw, Kachenje”

“Nishapoa”

“Tunampeleka hospitali gani?”

“Naona tumpeleke Hospitali ya rufaa Mount Meru”

“Poa”Alijibu na kuondoa gari kwa kasi,huku likiwa limeacha vumbi zito nyuma.

Nilimfikisha hospitali ya Mount Meru kwa matibabu. Aliingizwa chumba maalum cha wagonjwa waliozidiwa ACU na muda mfupi aliwekewa mashine ya kumsaidia kupumua. Walipomaliza walimtundikia maji ya mwili. Daktari walijitolea kuokoa maisha ya Getruda kadri walivyoweza. Muda mfupi nikiwa kwenye benchi, niliona mlango ukifunguliwa, alitoka nesi mmoja mwenye asili ya kiarabu, kwa haraka nilijikuta moyo ukinipasuka. Nilimfananisha na Jenifer niliyekutana nae nchini Thailand. Alinifuata pale nilipokuwa, kitu kilichokuwa tofauti ni kwamba yeye alivaa magwanda meupe, “ Halo, kaka wewe ndiye muuguzi wa Getruda Kimario?” nilishindwa kumjibu midomo ilibaki wazi, niliamini kwa hali mbaya ya Getruda nesi aliniletea taarifa mbaya.

“Kwani kuna nini nesi!…naomba unieleze!”niliongea mwili ukinitoka jasho pamoja na mambo mabaya Getruda aliyo nitendea lakini nilimpenda sana.

“Usiogope kaka. Niambie wewe ni muhusika?” Alisema tena kwa sauti ya chini.Nibaki nimeduwaa kama sekunde kadhaa.

“Ninani kwako?”Aliuliza tena ,lakini safari hii alionekana kukasirika. Nilishindwa kumwambi nilibaki machozi ya kinichuruzika, “Hata nikisema ni mke wangu sijawahi kukutananae kimwili, sasa ni mwambie mimi ninani wake?.Nikiwa nawaza, nikajikuta naropoka.

“Ni dada yangu” niliongopa

“Ok, pole sana mungu amemsaidia. Sasa ananafuu”akatulia kidogo na kunitupia tabasamu pana lililoshiba midomoni mwake.Kisha akasema “Tunategemea kumpa ruhusa kesho. Mungu akipenda”Nilipandisha pumzi na kuishusha kwa nguvu”oooophhhh!” nikajifuta jasho.

Kesho yake Getruda aliruhusiwa kurudi nyumbani.

*****************


Tukiwa sebuleni nilianza kumueleza Getruda. Moyo uliniuma kila nilipo kumbuka aliyonifanyia “Mke wangu kama ingenipasa kusema, nini kinacho ikera nafsi yangu ni kuni dhalilisha ndani ya kadamnasi, sio wafanyakazi wangu wa wageni, wote wanafahamu ulilolifanya, na isitoshe ile ni hotel yangu unadiriki kufanya mapenzi ukitoa kashfa ili kuinufaisha jamii, kumbuka aibu si yangu pekee, ni yetu wote.”

Sijui ni mkate sikio au nimpe kilema kwenye via vya uzazi ni mchome na moto wa umeme (hita)asiweze kufanya tendo la ndoa maisha?.Ndio itakuwa fundisho,kiherehere kitamuisha”wakati na waza cha kumfanyia, nilikatishwa na sauti.

“Mume wangu kumbuka wewe ndio uliyenitafutia mwanaume wa kuniridhisha kimapenzi, ilinijisikie nina mume, basi kama ni hivyo nami sitaki penzi la mtu mwingine wa nje. Nataka penzi lako nilikubali kwa kukuheshimu. Mwanamke kawaida hatafutiwi mume, anatafuta mwenyewe, hisia zote nilizoweka kama nipo na wewe, iweje useme na kudhalilisha, kama utashindwa leo kesho nataka talaka yangu,asubuhi na mapema, umenielewa?”Getrudaalinisemesha kwa ukali.

“Sio nimekukataza usiwe naye, kinachonikera ni kunidhalilisha na kutoa siri ya unyumba wetu, sina wivu na mapenzi yako.Ninachotaka unihifadhie siri moyoni mwako”niliinamisha kichwa chini kama kobe.

“Mume wangu nakutunzia heshima kuliko mtu yeyote duniani, nashangaa!unapo sema nainfaisha jamii. Kama angekuwa msichana mwingine asinge vumilia hata wiki moja, na washukuru wazazi kunifundisha uvumilivu ndani ya nyumba”Aliendelea kuongea,asijue nina mawazo nini moyoni.

Tukiwa kwenye mazungumzo,nilisikia simu ikiita,nilijipapasa kama ilikuwa simu yangu.Nilipotizama pembeni nilimuona Getruda akitoa simu yake kwenye pochi ndogo ya rangi nyeusi iliyojaa nakishi nyingi.

“Hallo, uko wapi?”Getruda alipokea tu,baada ya kuona jina juu ya kioo cha simu.Niligutuka nikahisi mtu huyo anamfahamu,ndio maana alimuuliza aliko.

“Aaaa..nipo Makutano bar hapa napata moja baridi moja moto.Vipi mume bwege yupo?”

“Yupo anakusalimia”Getruda alisema na kunitupia jicho ,akacheka kidogo na kuendelea, “Utakuja kutusalimia?”Getruda aliongea akiniongoa wasi wasi.

“Ninani huyo unaongea naye?”Nilijikuta nikisema wakati Getruda anaongea na simu.

“Wivu umekuzidi mume wangu.Kila kitu unataka kujua hebu chukua basi uongee naye”Getruda aliibadilikia kwa ghafla,alinyoosha mkono wake akitakakunikabidhi simu.

“Sihitaji kuongea nae,nimekuuliza kwani vibaya?.Nilifikiri ni mama amekupigia simu”

“Hapana.Nirafiki yangu”Kisha akaendelea kuongea nae.

“Samahani kwa usumbufu uliojitokeza.Mume wangu anwivu ilembaya”

“Sasa wivu wanini wakati hayawezi?”Sauti nzito upande wa pli ilisikika ikisema.

“Hata mimi nashangaa!”Getruda alidakia na kuangua kicheko kikubwa.

“Mpenzi sikia…..naomba ufike sasa hivi hapa Makutano bar”

“Mama anaumwa sana!.Ehhe mmempeleka hospitali?”Getruda aliongea maneno hayo akiwa tayari kesha kata simu.Aliendelea kuongea simu ikiwa imekatika ilimradi anipumbaze “Ana umwa na nini hasa?” alitulia sekunde mbili hivi akaendelea, “Ooo! My god .Kuna uwezekana wa kupona?”

alitulia tena sekunde kadhaa hivi, “Sawa.Ninakuja sasa hivi huko”Akajidai kukata simu.

“Vipi mbona jasho linakutoka?.Mama anaumwa na nini?”

Nilimwuliza sekunde chache alipokata simu. “Mama alidondoka ngazi akiingia kanisani”Getruda aliongea kiupole kabisa, akionekana kujizuia kulia.

“Kanisani?”

“Ndio.Na hivi sasa yupo amepelekwa hospitali ya Kcmc kwa matibabu” Safari hii alifura na alifanya kulalamika chini chini.

“Ooo! Pole sana mke wangu.Unaonaje nikaoga tukaenda wote?”

“Utanichelewesha sana”

“Basi siogi tena. Ngoja nivae twende,tena nina siku nyingi sijaenda kumsalimu”Niliongea nikiamka kitini, tayari kwa safari.

“Hapana.Nitakuletea taarifa ya hali yake.Nyumba tutamuachia nani?”

“Hilo halina shida.Nisubiri”

“Sitaki bwana. Wee kila mahali unataka kuongozana na mimi.Nimeshachoka, ngoja niende kisha kesho nikirudi nitakuja kukuchukua kwani hata kupajua hupajui.Unapafahamu pale tulipokuwa tukiishi zamani” Nilisimama kama mlingoti ,nikavuta pumzi na kuzishusha kwa nguvu.Nikatikisa kichwa na kusema “Sawa.Kama hutaki nikapajua kwenu leo ….hata kesho nitapajua”

Niliona Getruda akitoa tabasamu kubwa ,hakuishia hapo alinifuata nakunibusu shavuni “Mwaaaa”Kisha akaokota kipima joto chake,na kutoka kwa haraka akionekana mwenye wasi wasi mkubwa.Alipofika mlangoni aligeuka na kunitizama kama akinihurumia vile,sikugundua kitu ,nilibaki nimeduwaa.Akanipungia mkono na kusema “Bye bye”Nami nikapunga kono langu zito kigoigoi bila tabasamu.

Getruda alimpigia simu mteja wetu wa kila siku katika usafi,si mwingine bali Jangala. “HalloJangala tafadhali naomba unichukue hapa nyumbani”alisema baada ya simu kupokelewa.

“Sawa.Namshusha abiria hapa mjini nakuja”

“Ok”Alijibu na kukata simu.

Kama kawaida yake Jangala huwa hakaidi na hana tamaa.Aliingia na kusimama mbele ya Getruda binti Kimario.

“Shem vipi.Wapi leo pa kula kuku.Si unaelewa wiki end”Jangala alimtania Getruda.

“Ndio. Wiki end lakini kwangu imenijia vibaya .Nimepata taarifa mama yangu mgonjwa.Naomba unifikishe karibu na Makutano bar nikampe taarifa shangazi yangu.Kisha utaendelea na safari yako.Mimi nitakupigia kama nitakuhitaji tena”Getruda alidanganya.

“Sawa.Riziki ndogo ndogo hizi usininyime shem.Pole sana kwa kuuguliwa na mama yako”

“Nishapoa shem”Alimjibu kiunyonge.Getruda hakuuguliwa wala nini.Alipokuwa akienda ni Makutano bar kukutana na Mzee Jophu Kundy.

Katika mazungumzo yao walijikuta kufika Makutano bar, “Tafadhali nishushe hapa.Kuna uchochoro gari haliwezi kuingia huko.Shilingi ngapi?”

“Elfu nne zinatosha shem”Jangala alisema akimtizama Getruda.

“Punguza shem.Hujui mimi mteja wako?”

“Petroli imepanda bei sana shem. ‘Any way’ nipe tatu unusu”Jangala alisema .

Getruda alimpatia Jangala elfu tatu na mia tano,akashuka garini. “Usihaike shem.Nitafunga mwenyewe mlango.Mteja kwangu ni mtukufu”Jangala alisema baada ya kumuona Getruda anataka kufunga mlango. Getruda alijidai kama anaingia uchochoroni ili Jangala aondoke zake.Alipogeuka aliona gari la Jangala likiishia bali kabisa.Aligeuka na kurudim kuelekea kule Makutano bar.

*****************


Ndani ya makutano bar,alionekana mwanaume wa makamo.Kwa kumtizama ungeweza kukisia anamiaka hamsini ama hamsini na tano.Kichwa chake kilikuwa na mvi za kuhesabika.Uso wake ulisha anza kuwa na makunyanzi ya uzee.Alivaa suti ya kahawia,na viatu vya pembe nne ‘Four angile’.Shingoni alinyonga tai ya bluu iliyozidi kumfanya maridadi.Mkononi alivaa saa ya seiko 5 ya dhahabu.Meza aliyoketi ilijaa vyakula na vinywaji.

Mara kwa mara aliinua mkono wake wa kushoto akitizama muda,alipomaliza aligugubia glasi ya bia mdomoni na kuirudishia glasimezani.Pia muda wa kuiacha pombe ishuke vema tumboni alitupa macho yake lako la kuingilia wateja.Safari hii ilikuwa mara ya kumi kutizama lango hilo,alipohamisha macho aliyapeleka kwenye glasi ya kinywaji,akaona kama bia ilishaisha glasini,alikamata chupa ya bia na kumimina kiasi kwenye glasi ya bia.Hakuchelea aligugubia kama mikupuo miwili bila kuishusha mezani,alipomaliza akacheua kama mara tatu hivi,alihisi kilevi kikipanda vema ndani ya ubongo.Akajikuta akicheka mwenyewe

“Mimi ndiye.Mwingine hakuna”Alisema nakutizama simu yake.Aliiokota nakujaribu kupiga,simu aliyopiga iliita bila kupokelewa.

“Shiit.Kwanini hapokei?”alipayuka kwa ghadhabu.

Hakuchoka akapiga mara ya pli,iliita tena,akasikia ikipokelewa “Hallo Prety girl.Uko wapi mbona hupokei simu yangu?”

“Nakaribia jengo la Makutano hapa”

“Sawa. Nakusubiri kwa hamu wa moyo”Walikata simu.Mzee Jophu akawa habandui macho lango la kuingilia,alitaka kumwona Getruda akiingia kwa madaha.Ghafla aliona mlimbwende akiingia kwa mapana na kumfanya kila aliyeko mle ndani kumtupia jicho.Getruda hakuwa mzuri sana wa sura,lakini umbo lake na makalio ndio kichochezi kwa wanaume rijali.Kila alipovuta hatua ,makalio yake yalitikisika mithili ya mawimbi baharini.Nafiki jambo hilo ndilo lililomfanya Mzee Jophu ammezee mate mke wangu.Si kwamba na msifia kwa vile ni mke wangu,hapana.Njoo kwangu Arusha ushuhudie, ukweli wangu.Lakini kwa sasa ni mzee sana.

“Kaaaa, kakaka!”alionekana kijana mmja aliyeko nyuma ya mzee Jophu akihamaki,mfdomo ukiwa wazi kwa mshangao na mkono ukiwa umeshika mdomo wa chini,Jicho likiwa limemtoka kama ndulele iliyoiva.

“Mkindu wavona ilo ibora ledha aho”Kijana huyu alimwambia mwenzake kwa kilugha.

Akimaanisha “Mkindu umeona lisichana hilo linalo kuja hapo?”

“Nikirumo ilo!”Mkindu alijibu.

“Hilo ni balaa!” Wakacheka.

Mzee Jophu alimsindikiza Getruda kwa macho ya matamanio hadi alipomkaribia kabisa.

“Vipi.Mbona umechelewa ?”

“Mume bwege alikuwa akinichelewesha”Getruda aliongea akivuta kiti kilicho wazi.

“Achana nae.Ukisha mkabidhi fisi bucha unamatarajio gani?”

“Kuokota mifupa”Getruda alidakia.

“Hakuna kinachobaki.Fisi gani anakuachia mfupa!”Wakacheka na kupigana mabusu.Kisha akagonga meza.

“Muhudumuuu”aliita.

“Nakuja”sauti ilisikika kwa mbali kidogo.

“Kuja haraka.Watu wanapesa zao hazina pakwenda”Alisema akijiamini kabisa.Getruda alimtizama akagundua mzee Jophu alishaanza kulewa.

“Mpati wa moyo wangu kinywaji chochote anachotaka upesi”Muhudumu akaitikia sawa.

“Dada nikupatie kinywaji gani?”

“Henken ya kopo.Usisahau mrija tafadhali”

“Ya baridi au moto?”

“Aaaa! Vuguvugu.Nitapata?”

“Usihofu,utapata”Muhudumu aliondoka.

“Mpenzi nimekuita nina jambo muhimu la kukueleza,hivyo basi naomba uwemsikivu”Alitulia kidogo na kuokota glasi ya bia,hakuchelewa alimimina bia yote na kurudisha glasi tupu.Akacheua mara mbili nakuendelea “Kwanza kabla ya yote. Napenda unihakikishie kwamba unanipenda”

“Nakupenda sana mpenzi inamaana hujagundua bado?”

“Ninyi wanawake mnabadilika sana.Lazima kila tunapokutana tuulizane jambo hili”

“Si wote bwana.Unajua ninyi wanaume mkionyeshewa kama mnapendwa sana vichwa huvimba na kujiona mna matilaba ya kufanya lolote juu ya mwanamke”

“Ni baadhi ,si mimi Jophu”Akasema na kusogeza kiti jirani na Getruda.Kabla hajaendelea tayari vinywaji vililetwa,Henken ya Getruda na safari ya Mzee Jophu.

“Karibuni”Muhudumu alisema.

“Ahsante”Getruda akajibu.

“Wee binti mwite mchoma nyama tafadhali”Hakukawia kufika mchoma nyama. “Kata nyama ya kidari,ile laini…umeelewa?”

“Ndio,bosi”

“Haya futikaa”Alisema kiulevi ulevi.Akamgeukia Getruda, “Wife,sasa tuendelee na mazungumzo yetu”

“Kama umenidhihirishia unanipenda utakuwa upande wangu kwa lolote lile,si ndivyo”

“Ndivyo”

“Nikisema kitu kwa manufaa yetu lazima tusaidiane,sivyo?”

“Ndivyo”alijibu kiupole hakujua ni jambo gani anataka kuelezwa wakati huo.Kwa sasa Mzee Jophu akapunguza sauti akamweleza Getruda kwa sauti ya chini kabisa.Nafikiri alihofu watu kung’amua maneno yake.

“Getruda naomba iwe siri kubwa sana.Nataka tumuondoe Sweedy Duniani”Getruda alishituka sana kama aliyeamshwa usingizini. “Heee!”

“Usishituke laazizi wangu.Nimeamua hivyo kwa manufaa yetu pia.Kila siku kujiiba iiba ,tutajiiba mpaka lini?.Heri afe tupate uhuru….”

“Haiwezekani Jophu.Unajua dhambi ya kuua lakini?”Getruda aliuliza.

“Acha ujinga, nani kakuambia kuna dhambi.Nani aliyeenda akarudi akasema kuna adhabu kali?.Niambie”

“Kwenye maandiko takatifu,maneno hayo yapo.”Getruda alijibu akimtizama Jophu.

“Kumbe nimaandiko yaliyotungwa kama hadithi tu.Nitajie nani alikufa akafufuka na kutuonyeshea adhabu alizopata ahera?”

“Bwana acha mizengwe yako.Uhusiano wetu hauwezi kuzuilika kwa sababu ya Sweedy”

“Nitakupa chochote lakini tumuue Sweedy.Uko tayari?”Getruda alikaa kimya,safari hii alishindwa kijibu. “Nijibu basi?”Mzee Jophu alimhimiza.

“Nikujibu nini?”

“Kwani hujui.Sina jibu lolote.”Akamtizama Mzee Jophu ,na kuvutakumbukumbu ya siku ya kwanza tulipokuwa kanisani,alikumbuka maneno mengi ya mchungaji.Akanikumbuka nilipompiga busu la kwanza nikiwa namvisha pete ya ndoa.Pia akakumbuka maneno ya mama yake akimweleza juu ya unyumba wetu.Machozi yakamtiririka mashavuni bila kujijua.Akapandisha mkono wa kuume ulioshika leso na kujifuta. Mzee Jophu alinyoosha mkono na kumpatia funguo Getruda.

“Kuanzia dakika hii.Land cruiser iliyoko nje ni mali yako.”Getruda alishangaa hakuamini kile alichokuwa akikiona wakati huo.

“Mpenzi ni kweli ama ni mipombe inakusumbua akili?”

“Sijalewa wa moyo.Ninachohitaji sasa hivi, ni kutoa uhai wa huyu hanithi”Akatulia kama nukta tano hivi ,kisha akasema,“Sawa sawa?”

“Sawa”Getruda alijibu mapigo ya moyo yakimwenda mbio.Alifikiri na kuona kwanza alishachoka kukodi teksi kila siku.Naye alitaka kutembelea gari la kifahari.Alitamani akawatambishie mabinti wenziye aliosoma nao pale Mkuu Rombo.Watajuaje kwamba naye nitajiri pasipo kutembea na gari la kifahari?.Aliamini mtu akiwa na pesa huheshimika kuliko hata kitu chochote duniani.Akajikuta moyo ukipamba na furaha kali, “Acha afe bwana kwani nini bwana. Mtu kama furushi la nguo, heri afe , wangapi wameuawa na kuwaacha wake zao na mapesa kibao.Mungu nisamehe”aliwaza akilini.

Waliendelea kunywa na kula nyama choma pale.Getruda alimaliza bia yake na kuongezwa zingine mbili,tayari ubongo ukafa ganzi.Alianza kuongea sana,tena bila kujali kwamba alisikiwa na watu. “Mpenzi wangu nasema hivi…nitamuua kwa mikono yangu mwenyewe.Haina haja ya kuishi wakati hana sifa ya kumfanya hai. Eti mume, mume gani bwege kilasiku hapandi kitandani mpaka nishikwe na usingizi ndio nae apande!!!!”

“Hatakama ingelikuwa mimi.Ningetumia akili hiyo hiyo.Unafikiri ni kazi ndogo hiyo…fedheha bwana!”

Mzee Jophu na Getruda alikunjwa na kuondoka zao.Walielekea nyumba moja ya wageni ambako waliingiza gari la Gertuda na kujipumzisha.

**************


Katika maisha yangu nina kijitabia fulani cha kutotoka siku za mwisho wa wiki,isipokuwa jioni tena nikiwa na mke wangu ,Getruda. Huwa natoka katika matembezi mafupi na kurudi nyumbani.Juma pili hii ilikuwa ngumu kwangu.Kwanza mke wangu hakuwepo,usishangae nikimuita mke wangu japo sikufanikiwa kufanya tendo la ndoa.Ni mke wangu kwa sababu nimefunga ndoa kanisani.

Mawazo bado yalinizonga sana akilini,niliwaza safari ya ghafla ya mke wangu.Nilitamani sana nijue maendeleo ya wazazi wake huko mkuu Rombo.Kingine ni tatizo linaloniletea utata ndani ya ndoa yangu.Nilizidi kuwaza ,kwanini ugonjwa huo uwe kwangu tu.Kwanini usiwe kwa fulani?.Nilitamani kunywa bia lakini lakini nikaona si kutatua tatizo zaidi ya kuliongeza.

Nikiwa kwenye dimbi la mawazo,nilisikia simu ikiita,nilishituka sana.Kwa haraka nikaiendea simu ambayo niliiacha Varandani juu ya meza.Nilifikiri mambo mengi ,nikahisi aliyepiga simu alikuwa mke wangu akinipa habari za mama yake,nilitegemea kupata habari mbaya kutokana na maneno aliyoniacha nayo Getruda jana alipokurupuka akionekana wazi kuchanganywa na hali ya mama yake.Nilipofika nikaiokota simu upesi na kuipokea , “Hallo mume wangu.Umzima ?”

“Ndio.Vipi kuhusu hali ya mama.Anaendeleaje?”Nilimwuliza.

“Kidogo amepata ahueni.Kuna uvimbe gotini unamsumbua”

“Utakuja lini?”

“Aaa kesho jioni.Namsaidia kumuuguza hospitalini”

“Sawa.Nimebaki mwenyewe kama mkiwa”

“Usijali mpenzi.Upo nyumbani, na hutoki leo?”

“Ndio,nipo sitoki bila wewe.Kwanza najisikia vibaya kabisa sijui ni kwanini mpenzi”

“Pole sana mume wangu,bye”

Getruda akakata simu.

*********************


Kulikuwa na kundi la patao watu watano,aliyekuwa msemaji mkuu akiwa mzee Jophu.Pembeni aliketi Getruda na kushoto kwake mwanaume mmoja mwanye umbo kubwa,unaweza ukamfananisha na mcheza mweleka.Mikono yake minene iliyojaa na kujengeka misuli.Kushoto kwa mwanaume yule alikuwepo kijana mwingine,mrefu mwembamba lakini anasura ya kukatili.Ukimuona lazima ungemtambua kama ni muuaji.Huyu aliweka bastola kibindoni,bastola aina ya Revolver.Aliyebaki alionekana mdogo sana,ukitadhimini umri wake ni miaka kumi na tano,alionekana alikulia mitaani.Huyu ni kibaka mzoefu ,achilia mbali bangi ,sigara na dawa za kulevya, kuvuta petroli na gundi ya viatu kwake si tatizo.Mtoto huyu walimtumia sana katika matukio ya ujambazi na upelelezi wa wapi kuna pesa ,wapi tukaibe leo.

Walicheka muda mfupi tu baada ya Getruda kukata simu, “Anasemaje huyo maiti”Mzee Jophu aliuliza akiwa anamtizama Getruda kwa udadisi.

“Anasema leo yupo nyumbani hatoki,ni jambo ambalo liko wazi bila mimi habandui mguu wake.Hivyo kazi yake imeisha”

“Patamu sana hapo.Naomba vijana wangu waingie kazini.Kama nilivyo waelekeza na mfanye kwa tahadhari sana msije kubainika kama ninyi ndio mlioua.Mmenisikia?”

“Mzee usitufundishe hii ndio kazi yetu kama kazi nyingine.Tumeua sana na tutaendelea kuua.Pesa ya kazi mbele”Alisema jambazi mmoja nene lenye kifua kama pipa,lilitambulika kwa jina moja tu ‘Man Kaugo’Man Kaugo ana kasumba moja hataki kufundisha kazi ya uuaji,nasema anaielewa vema na ujuzi huo kwake ume komaa.

“Naona mchukue lita arobaini za petroli.Mzungushie nyumba yake yote na muitie kiberiti”

“Eeee!kuna vitu vyangu vya muhimu.Kwanini msimuue bilakuchoma nyumba”

“Vitu vyako nitakulipa.Tatizo ni nini?”

“Nyumba yamgu.Nilitaka mumuue nibaki na nyumba”

“Nyumba nitakununulia njiro”

“Haya, usinidanganye mpenzi”

“Sikudanganyi.Mimi na wewe kwani wa tani?”

“Hapana”

“Sasa kumbe…” akatulia kidogo kisha akasema, “Nafikiri tumemaliza makomando wangu”

“Pesa zetu bado.”

“Kiasi gani ?”

“Milioni tatu kwa kichwa kimoja”

“Ok,subirini kidogo nakuja.”


Mzee jophu alitia gari moto na kuondoka zake.alielekea benki ambako alichukua milioni tano na kuzihifadhi.Hakuchelewa alirudi. “Kamata milioni tatu hizi.Naomba mharakishe tafadhali”

“Sawa mzee.Utasikia mwenyewe mambo yakijibu”Wale vijana waliondoka zao.

Nilisikia kama watu wakiongea nje ya jengo langu,kila nilipojaribu kutega sikio kwa makini,nilishindwa kun’gamua mazungumzo yao.Nilitunguza redio kabisa ,japo nilikuwa macho lakini nilihisi bado kiko usingizini,watu hao walinikaribia dirishani ,kwambali nikasikia mmoja wapo akisema “Hili ndilo dirisha lake”

Mwingine akasema “Basi hapa tumwage petroli nyingi iliafe haraka”kilikuwa kitendo cha haraka nilisikia petroli ikimwagwa dirishani,nilikurupuka na kushituka ,nilipofungua macho kumbe nilikuwa nikiota njozi mabaya kabisa.Kukurupuka kwangu hata mke wangu Suzan ambaye tulibahatika kupata mtoto wa kiume aitwaye Samji ,alinisikia nikipiga kelele, “Nakufaaaaa”

“Nini mume wangu?”Suzan, mke wangu aliniuliza akiwa na masalio ya usingizi.Nilihisi mapigo ya moyo yakinienda mbio utadhani nilikimbia umbali mrefu bila kupumzika.

“Baba samji,ni nini mbona umepiga kelele kiasi hicho?”

“Ndoa yangu inanitesa”Niliropoka nikipikicha macho, sikuamini yale niliyoyaona nikiwa usingizini.

“Ndoa yako inakutesa kivipi?”

“Nafikiri nilikuwa nikiota ndoto ya mateso kabisa”

“Ndoto?.Nilikusikia hata wakati mwingine ukilia ukiwa usingizini.Nilikutingisha lakini huku shituika, ulikuwa ukisema Getruda Getruda .Getruda ninani?”Nilitulia kidogo nikajaribu kumkumbuka, “Getruda ni huyo mwanamke niliyemuoa, akawa ananitesa”

“Usinidanganye mume wangu.Madhambi unayofanya na mahawara wako ,ndio unayaota usiku?”

“Basi nisamehe mke wangu,ni ndoto tu.Sina mtu nimpendaye zaidi yako.Sijui njozi ya ajabu namna hii imetokea wapi.Yote niliyoota hakuna hata kimoja kilichowahi kunitokea”

Ilikuwa usiku ,majira ya saa kumi na moja.Suzan, mke wangu alinisamehe na tukaanza kusali.


MWISHO



  FAHAMU MAMBO MUHIMU YANAYOZIDISHA UPENDO KATIKA MAPENZI

katika Mapenzi kuna vitu vingi unaweza kumfanyia Mpenzi wako ukamfurahisha na kumfanya azidishe Mapenzi ila katika safu hii nitazungumzia Mambo machache muhimu yatakayokusaidia kuboresha na kudumisha penzi lako kwa umpendae 
1.KUMNUNULIA ZAWADI MPENZI WAKO:
» Zawadi ni moja ya sehemu husika katika Mapenzi inayoweza kufanya penzi likawa bora na lenye kupendeza siku zote, faham kwamba hakuna mtu asiependa kupewa zawadi na kila anaepewa zawadi siku zote hujihisi kama ni mtu anaependwa na anaejaliwa na kuthaminiwa hususani katika ulimwengu wa Mapenzi unapompa mpenzi wako zawadi basi faham ya kwamba utamfanya mpenzi wako ajione kama ni wapekee kwako na anathamani kubwa kwako hivyo hatosita kudhihirisha mapenzi yake kwako, kikubwa zingatia pindi unaponunua zawadi kwa ajili ya kumpa mpenzi wako jitahidi kuwa mbunifu na uwe ni mwenye kubadilika sio kila siku zawadi zile zile zinajirudia kwa kufanya hivi utamboa mpenzi wako kuwa mbunifu na jaribu kumpa mpenzi wako zawadi zenye kutunzika mfano kama Card, maua, nguo n.k. Utamfanya azidi kukupenda zaidi na zaidi.
2. MSIFIE MPENZI WAKO:
» Sifa zinaleta changamoto katika mapenzi. Unapaswa kutambua kuwa usiwe mchoyo wa sifa kwa mpenzi wako usisubiri watu wapembeni wamsifie mpenzi wako pindi anapofanya jambo zuri na lenye kupendeza chukua nafasi hii wewe kama kioo chake unadhani usipo msifia mwenza wako unataka nani amsifie?! Jitahidi kudhihirisha sifa kwa mpenzi wako kwa mfano umemuona mpenzi wako kapendeza basi usisite kumwambia "Sweetie nimependa vazi lako la leo ama hakika umetoka sex nakutamani zaidi ya siku zote navyokutamani ingawa siku zote unaziteka hisia zangu ila leo ni zaidi" unaweza kumpa maneno kama haya na mengine mazuri ya kuvutia, sifa zipo nyingi mbali na kumsifu mavazi yake hata tabia n.k. Kwa kufanya hivi utamfanya mpenzi wako azidishe mapenzi kwako kwani atahisi kampata mtu anaejali ubora na uhalisia wake kimaumbile na kimatendo. ZINGATIA:- Usitoe sifa ilimradi sifa zisizo na ukweli.
3. EPUKA KUMUUDHI MPENZI WAKO:
» Sote tunafahamu kuwa hakuna binadamu aliekamilika na hakuna alietolewa nyongo kila mtu anakasirika na anakosea ila solution kubwa ni kudhibiti hasira na kurekebisha makosa na kusuluhisha hususani kwenye mapenzi, katika mapenzi hakuna jambo baya linalopunguza upendo kama ugomvi na kumuudhi mpenzi wako mara kwa mara. Ili kuboresha mapenzi na kulifanya penzi lako liwe imara na lenye kuvutia basi jitahidi kuepuka kumuudhi mpenzi wako na pindi ikitokea umekorofishana na mpenzi wako jaribu kutafuta suluhu mwite kaa nae muombe samahani iwapo kama unakosa na hata ikitokea kosa si lako pengine kakuudhi na bado unamuhitaji usikae na kinyongo wala usiumize nafsi yako kaeni muyamalize muendeleze mahusiano yenu na msiwe watu wa kuzungumzia tofauti zenu kwa watu wa pembeni. Kwa kufanya hivi daima mtakuwa ni mfano mzuri wa kuigwa na mapenzi yenu hayatofika kikomo zaidi yataendelea kushamiri.
4. MFANYIE YATAKAYO MFURAHISHA:
» Kuna mambo mengi mazuri na yakuvutia katika mapenzi unaweza kuyafanya kwa mpenzi wako yakamfurahisha kwa mfano unaweza kusoma tabia ya mpenzi wako na ukajua ni nini anapenda na kipi hapendi kufanyiwa ukajitahidi kujilinda kumtendea asiyoyapenda na ukaufungua moyo wako kwa kumridhisha kumfanyia kile anachokipenda. Katika mapenzi watu wengi hupenda kutolewa Out, kupewa ofa ya lanch, kupewa zawadi zenye mvuto na zenye hamasa nzuri kwenye mapenzi. Unaweza kufanya vitu vizuri vyenye kuvutia kwa mpenzi wako vikamvutia ikawa ni nafasi nzuri kwako kumfanya azidishe mapenzi.
5. KUWA MTU WA UTANI KWAKE:
» mpenzi msomaji ninapozingumzia mapenzi na maanisha mazoea yaliyoambatana na upendo, siku zote mapenzi hujijenga moyoni kwa mtu kutokana na ukaribu na mazoea yaliyopo baina ya watu wawili, katika pointi hii ya mwisho nataka nizungumzie utani katika mapenzi unafaida gani. Mpenzi msomaji fahamu yakuwa utani ni moja ya sehemu katika mapenzi na utani unasaidia kuboresha mapenzi ila utani ninaotaka kuuzungumzia hapa ni utani wa kawaida na sio ule wa kuvuka mipaka. Elewa wazi kabisa unapokuwa na mpenzi wako na ukawa ni mtu wa utani inakusaidia wewe kumfanya mpenzi wako akuzoee na awe anajisikia kuwa karibu nawewe muda wote kwani utakuwa unamfurahisha kutokana na utani wako. ZINGATIA:- Usivuke mipaka ya utani, usimtanie kupitiliza, mtanie kutokana na mazingira, usiwe utani unaofanana nakweli, mtanie kwa faida.

MAPENZI HUWA IMARA PALE YANAPOJENGEWA NJIA YA KUTOKA NA KUINGIA -3

MPENZI msomaji, naendelea kuelezea ‘topiki’ inayoelezea namna mapenzi yanavyokuwa imara yakijengwa. Tuwe pamoja hadi nitakapoishia.
Mwenzi wako atakuheshimu mno kama nawe unamuonesha utiifu. Hata wasaliti wengi, wamejikuta wakisalitiwa baada ya kuwaonesha wenzi wao jinsi wasivyo waaminifu.

Onesha utu ili uendelee kufaidi upendo na huduma. Mwenzi wako amekuwa akitumia fedha nyingi kukuhudumia, jambo unalodaiwa kwake ni utu.

Hakikisha unampa faraja mpaka hajutii kile anachokitoa kwake. Faraja siyo mapenzi ya kitandani peke yake.

Unapaswa kutuliza akili na ujue mwenzi wako anahitaji nini kutoka kwako. Ukishakifahamu, ni juhudi yako kuhakikisha hakikosi. Kufanya hivyo ndiyo utu na ndivyo utakavyoweza kumteka zaidi na zaidi. Atakapokuwa anakutendea lakini maombi yake huyapokei vizuri, unakuwa unamkatisha tamaa.

Kadiri unavyomkatisha tamaa ndivyo unavyoelekea kumvunja moyo. Tambua kwamba moyo unapovunjika inakuwa ni ngumu mno kuurejesha kwenye hali yake ya kawaida. Kwa maana hiyo unakuwa umepoteza upendo na huduma zote ulizokuwa unazipata kutoka kwake.

Mapenzi ni mchezo wa nipe nikupe. Nipe upendo na wewe nikupende. Inawezekana yeye ndiye alianza kukupenda ndiyo maana akafanya juu chini mpaka mkawa pamoja. Baada ya hatua hiyo ni muhimu kwako kuhakikisha unaonesha upendo kwa sababu mmekubaliana kupendana.

Kupenda siyo maigizo, kusema utamfanyia magirini mwenzi wako ili utimize matakwa yako fulani. Kila aliyeingia kwenye uhusiano kwa malengo tofauti na upendo alifeli. Unaposoma makala haya, ikupe njia nzuri ya kutimiza wajibu wako kwenye mapenzi halafu umuache naye atimize kwa upande wake.

Unapokuwa unatimiza wajibu wako, hebu jiulize naye anafanya nini? Ni hatari sana kuendelea kuonesha unampenda na kumjali, wakati yeye hakujali kwa chochote. Mapenzi siyo tu kwamba yapo, ila yamekuwepo kwa ajili ya kupeana faraja.

Kama mwenzi wako hakufariji maana yake unatakiwa uhame hapo ulipo. Jinsi utakavyokuwa unazidisha upendo, haitakusaidia, kwani ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa. Badala ya kukushukuru, yeye atakuona zezeta uliyekufa kwake. Unatakiwa kuutetea moyo wako.

Naomba nikushauri kuwa akili yako iwe hai kila siku. Uwekezaji wako uendane na kile ambacho wewe unakipokea kutoka kwa mwenzi wako. Kufanya zaidi au pungufu ni kosa kubwa. Kufanya zaidi maana yake unakuwa unaunyanyasa moyo wako na pungufu unakuwa humtendei haki mwenzio.

Labda nisisitizie kitu. Sina maana kwamba kama wewe unatoa fedha ni sharti naye awe anakupa, la hasha! Uhusiano bora wa mapenzi huboreshwa na namna ambavyo wahusika wanavyohudumiana. Kila mmoja kuhakikisha anakuwa jirani na mwenzake wakati wote.

Mmoja anaweza kuwa na matatizo ya kipato, ni vizuri sasa mwenzake kuwa naye karibu kuhakikisha changamoto hiyo inakwisha. Ni ajabu pale mtu anapokabiliana na hali ngumu ya muda mfupi na anahitaji tu faraja kutoka kwa mwenzi wake lakini akawa hapati.

Hizo ndiyo dalili za unyonyaji. Kama wewe matatizo yako ya kifedha unayaweka mstari wa mbele na unatatuliwa, iweje mwenzako umeshindwa kumfariji wakati wa shida zake? Hiki ni kipengele kibaya ambacho kimewafelisha wengi. Baadhi wamepoteza wapenzi bora kwenye maisha yao.


KUNA MFANO KHALID NA GIFT

Khalid akiwa na upendo wa dhati kwa Gift, alimtabiria mema na kumtegemea kwamba ndiye atakuwa mke wake wa ndoa. Walipokuwa wanaanza uhusiano, Gift alikuwa amemaliza kidato cha sita Shule ya Sekondari Mwanza, wakati huo, Khalid alikuwa ni mfanyabiashara wa mitumba, Soko la Mlango Mmoja (Langolango), Mwanza.

Walifahamiana kwenye daladala, siku ambayo Khalid alimkuta Gift akiwa kwenye muonekano wa kukata tamaa ya maisha. Alikuwa amepata alama ambazo asingeweza kuendelea na chuo kwa udhamini wa serikali. Hilo lilimkatisha tamaa, ndoto zake za kuwa daktari bingwa wa kike aliona zimefika ukingoni.

Hata mwanzoni Khalid alipojitahidi kuzungumza na Gift amueleze tatizo lake, alimdharau. Alimuona wa kawaida, asingeweza kumpa msaada wowote. Kwa maana hiyo alimdharau lakini Khalid aliongeza juhudi kujua kilichopo ndani ya mrembo huyo.

Baada ya mzunguko wa muda mrefu, ikabidi Khalid aombe japo mawasiliano. Wakabadilishana namba za simu. Tangu siku hiyo, Khalid aliendelea kumfikiria sana Gift, aliwaza vitu vingi. Kubwa zaidi alihisi kuna  kitu kikubwa kipo ndani yake, alijihisi kumpenda mrembo huyo.

Kingine kilichomsumbua Khalid ni hali ya Gift, alihisi kuna tatizo kubwa ndani yake. Siku moja akamtafuta kwenye simu, alipompata alimuomba wakutane, akamkatalia. Akaendelea kumjaribu mara kwa mara, akawa anagonga ukuta lakini baada ya wiki mbili, Gift alikubali kukutana na Khalid.

Walikutana kwa mara ya kwanza Ilemela, Tunza Beach, wakazungumza mengi, wakaweza kufahamiana. Gift akatambua kwamba Khalid ni mfanyabiashara wa mitumba, vilevile Khalid akaelewa nini hasa kinachomtesa Gift. Khalid akaamua kulibeba tatizo la Gift kama lake.

JAMANI MIE UKAHABA SASA BASI" PART 6

INAENDELEA HAPA: Kipindi Mr. Brown anampiga mke wake Mrs. Brown ghafla wakatokea wazazi wa Mr. Brown ambao ni wakwe wa Mrs. Brown walikwenda kuwatembelea wakakuta kuna vurugu kwa watoto wao walichokifanya wazazi wale waliamua ugomvi na kuwaweka chini na kuwasikiliza kwa umakini watoto wao chanzo cha wao kugombana ni nini? Wakaanza kuelezea ilivyokua. Wazazi wa Mr. Brown wakatumia busara na kuwasihi wasigombane na wakawapatanisha watoto wao pale pale Mr na Mrs. Brown wakamaliza tofauti zao wakawa na amani wakajumuika pamoja na wazazi wao mpaka ilipofika jioni wale wazazi wakaondoka huku nyuma Mr na Mrs. Brown walikaa na kujadili njia nyingine ya kumsaidia binti yao Jenifer aweze kuendelea na masomo shule wakaona ni bora wamtafutie tu binti yao shule nyingine ili aweze kuendelea na masomo yake, baada ya siku kadhaa Mr. Brown alijitahidi kuhangaikia shule ili aweze kumpeleka binti yake JENIFER aweze kuendelea na masomo akiwa na dhamira ile ile aliyokua nayo tangu awali kuwa binti yao JENIFER wakimsomesha
baadae atakuja kuwasaidia katika maisha yao, mungu alisaidia Mr. Brown akajitahidi akafanikiwa kumpatia nafasi binti yake JENIFER katika shule moja iitwayo KILIMANJARO SECONDARY SCHOOL na binti yao akajiunga na shule hiyo akaendelea na masomo yake. JENIFER alipokua shuleni hapo tabia yake chafu haikubadilika aliendelea na tabia yake ile ile ya kua na marafiki ambao tabia zao zilikua ni chafu na ikafikia hatua JENIFER akawa anamahusiano ya kimapenzi na waalimu wa shuleni hapo tena kwa kuwachanganya alikua anatembea na MWALIMU MKUU (head master), MWALIMU MKUU MSAIDIZI (Second master) na MWALIMU WA TAALUMA (Academic master) tena bila ya walimu hao kutofahamu kama wanachangia penzi moja kwa binti huyo, Sasa siku moja Mwalimu mkuu wa Shule hiyo ambae ni mpenzi wake JENIFER alimuita JENIFER ofisini kwake na kuanza kumshika shika ofisini hatimae wakafanya nae tendo chafu la ngono ndani ya ofisi na hawakufunga mlango wa ofisi hiyo, ghafla Mwalimu mkuu msaidizi
akafungua ule mlango wa ofisi ya mwalimu mkuu, alikua anampelekea ma faili mwalimu mkuu alipovamia akamkuta mwalimu mkuu na JENIFER wakiwa katika tendo, mwalimu mkuu msaidizi alishtuka sana kuona vile hakuongea kitu alitoka nje haraka.

JAMANI MIE UKAHABA SASA BASI" PART 5

 INAENDELEA HAPA:
Baada ya kuvutana sana kati ya Mwalimu mkuu na Mr. Brown ofisini ikabidi mwalimu mkuu akubali kuwa mpole na kurudisha pesa japo sio zote ilibidi mwalimu mkuu atoe nusu ya pesa zilizolipwa, Mr. Brown alilipa ada Shilingi laki moja na nusu ikabidi mwalimu mkuu atoe nusu ya pesa hizi Shilingi elfu sabini na tano na kumpa Mr. Brown. Mr. Brown akapokea zile pesa Shilingi elfu Sabini na tano akamchukua binti yake JENIFER wakaondoka na kuelekea nyumbani kipindi wapo njiani wanaelekea nyumbani, Mr. Brown alikua na hasira sana akamwambia binti yake JENIFER "We mtoto leo tukifika tu nyumbani chukua nguo zako na uondoke nyumbani kwangu sitaki kukuona, mshenzi wewe!". Walipofika nyumbani tu Mr. Brown akaanza kumuhadithia mke wake Mrs. Brown yaliyotokea shuleni kuhusu binti yao JENIFER na akamwambia Mrs. Brown kuwa hataki hata kumuona aondoke nyumbani kwake lakini kwa maamuzi haya ya Mr. Brown mke wake Mrs. Brown hakuafikiana nayo akamwambia mume wake
"SASA MUME WANGU UNAMFUKUZA MTOTO AENDE WAPI WAKATI HAPA NDIO KWAO, UNADHANI ATAENDA WAPI? KAMA MAJI YAMEISHAMWAGIKA MAKOSA NDIO KISHAFANYA HAKUNA JINSI NI KUMSAMEHE NA TUKAE TUSHAURIANE TUJUE TUNAFANYAJE MUME WANGU PUNGUZA HASIRA". Mr. Brown akamjibu "HAIWEZEKANI MIMI SITAKI HATA KUMUONA HUMU NDANI AONDOKE SITAKI KUMUONA". Mrs. Brown nae akamjibu "KAMA UNATAKA HUYU BINTI AONDOKE HUMU NDANI BASI JUA NITAONDOKA NAE SIWEZI KUKUBALI BINTI YANGU AONDOKE AKAPATE SHIDA WAKATI KWAO ANAPO, UKIMFUKUZA JUA NAMIMI NAONDOKA HUMU NDANI" Baada ya Mrs. Brown kumuambia Mume wake Mr. Brown maneno hayo ghafla Mr. Brown alisema kwa sauti kali ya juu "SAWA MKITAKA MUONDOKE WOTE, SIWEZI KUFUGA UPUMBAVU KAMA UNAONA NAMUONEA MTOTO WAKO MFUATE MUONDOKE WOTE PUMBAVU!". Mrs Brown akamjibu "EH E! TAFADHALI BABA WEE, USINITUKANE NGOJA TUKUPISHE UBAKIE NA NYUMBA YAKO SIO UNIFOKEE. MPUMBAVU MWENYEWE!. Ghafla Mr. Brown alikurupuka na kumvamia mke wake Mrs. Brown na kuanza kumpiga makofi huku akimwambia
"YANI WEWE UNADIRIKI KUNIAMBIA MIMI MPUMBAVU, WAKATI JENIFER KAFANYA MAKOSA DHAHIRI. HIVI MIMI NINAVYOHANGAIKA KUTAFUTA PESA ZA KUMSOMESHA HALAFU ANALETA UPUMBAVU UNAFURAHIA ETI EEH!"

JAMANI MIE UKAHABA SASA BASI" PART 4

 INAENDELEA HAPA: Mwalimu KABAVAKO aliwachapa kila mmoja fimbo nne nne, kisha akawarudisha ofisini kwa mwalimu mkuu walipofika ofisini kwa mwalimu mkuu, mwalimu mkuu aliwaambia inabidi awape adhabu ya kukaa nyumbani mpaka uongozi wa shule utakapo kaa kikao na kuwafikiria na kujadili kosa lao ndio wafanye maamuzi ya kuwasamehe au kutowasamehe. Mr. Brown baba yake na JENIFER alijitahidi sana kumbembeleza mwalimu mkuu awasamehe ili waendelee na masomo lakini mwalimu mkuu alikataa katu katu na akamwambia Mr. Brown kuwa "MZEE KOSA WALILOFANYA HAWA WATOTO NI KUBWA SANA TENA AFADHALI YA HAWA WENGINE KULIKO HUYU BINTI YAKO JENIFER, JENIFER KWANZA HANA HESHIMA KADIRIKI KUMSINGIZIA MWALIMU WANGU KUWA KAMTONGOZA WAKATI SIO KWELI HUONI KAMA HUYU MTOTO ANAWEZA KUJA KUTUCHAFULIA SIFA YA SHULE YETU? NI BORA NIWASAMEHE HAWA WOTE LAKINI KWA BINTI YAKO JENIFER SIWEZI KUMSAMEHE" ghafla mwalimu mkuu akabadilisha mawazo pale pale akawaambia wale rafiki zake na JENIFER "NYIE NIMEWASAMEHE NENDENI NYUMBANI MKAVAE NGUO ZA SHULE NA MJE DARASANI MUENDELEE NA MASOMO ILA JENIFER SINTOWEZA KUMSAMEHE SAWA?!" wale wanafunzi watatu ambao ni rafiki zake JENIFER walifurah na hawakuamini kama wamesamehewa wakamshukuru sana mwalimu mkuu na wakamuahidi kuwa hawatorudia tena, wakaondoka ofisini na kuelekea majumbani kwao kuvaa nguo za shule. Huku ofisini mwalimu mkuu akanyanyua simu yake ya mezani akampigia Secretary wake na kumuamuru achapishe barua ya kumsimamisha shule mwanafunzi wake JENIFER. Mr. Brown alijitahidi sana kumbembeleza mwalimu mkuu amsamehe binti yake mpaka machozi yakawa yanamtoka Mwalimu mkuu akamwambia Mr. Brown "MZEE HILI NATOA FUNDISHO ILI BINTI YAKO AJIFUNZE SIWEZI KUMSAMEHE MTOTO MSHENZI SANA HUYU" Mr. Brown alimbembeleza sana mwalimu mkuu lakini mwalimu mkuu alimkatalia katu katu kumsamehe JENIFER na akawaomba Mr. Brown na Binti yake JENIFER watoke nje ya Ofisi wasubirie barua ya kusimamishwa shule binti yao. Baada ya muda Secretary alimaliza kuchapa barua na kuipeleka ofisini kwa mwalimu mkuu, mwalimu mkuu akamwita kiranja mkuu wa shule akamwambia aende kupiga kengere ya dharura ili wanafunzi wote wakusanyike mstarini aitoe barua ile hadharani mbele za wanafunzi. Kengere ilipigwa wanafunzi wote wakatoka madarasani na kuelekea mstarini wakakusanyika wanafunzi wote na walimu wote wa shule hiyo, mwalimu mkuu akaanza kuelezea yote yaliyojiri kwa JENIFER na kuwajulisha wanafunzi kuwa kasimamishwa shule baada ya hapo wakateuliwa walimu watatu wamchape fimbo JENIFER kila mwalimu amchape fimbo tatu, kisha wanafunzi wakaruhusiwa waende madarasani kuendelea na masomo yao. Mr. Brown alijisikia aibu sana kwani binti yake JENIFER alichofanya ni kitu cha ajabu hivyo alikua na hasira sana kilichomuumiza ni Ada aliyoitoa shuleni hapo ya kumlipia binti yake akifikiria jinsi alivyoipata pesa katika mazingira magumu ilimradi binti yake asome lakini JENIFER yote hakujali, sasa kivumbi kikaanza kwa Mr. Brown na Mwalimu mkuu, Mr. Brown akaanza kudai pesa ya ada ya mwaka aliyolipa shule akataka arudishiwe pesa yake ukaanza mzozo ofisini kati ya Mwalimu mkuu na Mr. Brown hatimae wakaanza kushikana mashati ofisini, Mr. Brown anataka pesa mwalimu mkuu anasema hatoi pesa ikawa vurumai ofisini

JAMANI MIE UKAHABA SASA BASI" PART 3

INAENDELEA HAPA:
Ilipofika kesho yake asubuhi siku ya Ijumaa tatu JENIFER na baba yake Mr. Brown walifunga safari mpaka shule, walipofika shuleni hapo moja kwa moja wakaenda mpaka ofisi ya mwalimu mkuu wa shule hiyo (HEAD MASTER) walipofika ofisini kwa mwalimu mkuu wakamuomba JENIFER atoke nje na aelekee mstarini baada ya hapo aende darasani kusoma. JENIFER akatoka nje na kuelekea mstarini huku ofisini akabakia mwalimu mkuu na Mr. Brown wakizungumza. Mr. Brown alimuelezea kwa kirefu mwalimu mkuu kuwa kuna mwalimu wake hapo shuleni anaitwa MWL. KABAVAKO anamtaka binti yake kama alivyoelezwa na binti yake JENIFER, baada ya mwalimu mkuu kuambiwa vile alichokifanya akamtafuta kiranja wa shule akamtuma aende kumuita JENIFER pamoja na huyo Mwalimu KABAVAKO wafike ofisini hapo kwa mwalimu mkuu. Yule kijana ambae ni kiranja akaenda kuwaita JENIFER na Mwalimu KABAVAKO walipofika ofisini mwalimu mkuu akamuomba JENIFER aelezee ilivyokua kuhusu mwalimu KABAVAKO. JENIFER akaanza kuelezea kama alivyowaelezea wazazi wake kuwa mwalimu KABAVAKO anamtaka kimapenzi lakini yeye hamtaki na amekua anamtesa sana shuleni hapo, na amemuahidi kuwa atafanya kila njia ili amfukuzishe shule pia kuna wanafunzi aliwakamata disco usiku mwalimu KABAVAKO akamuahidi Jenifer kuwa atamuingiza nayeye katika hilo kosa la hao wanafunzi ili wafukuzwe wote shule. Ndivyo JENIFER alivyojitetea kwa kusema haya mbele ya baba yake Mr. Brown, mwalimu mkuu na mwalimu KABAVAKO. Mwalimu kabavako alipigwa na butwaa akabakia anashangaa kutokana na maneno aliyosingiziwa lakini alikua ni mwenye busara na subira akamuacha JENIFER azungumze mpaka alipomaliza ikafika zamu yake mwalimu KABAVAKO ajielezee alichokifanya mwalimu kabavako akamuuliza swali JENIFER "JENIFER WEWE HAPA SHULENI UNA MARAFIKI?" Jenifer akamjibu "NDIO NINAO" mwalimu KABAVAKO akamwambia "UNAWEZA KUNITAJIA MARAFIKI ZAKO WATATU MUHIMU AMBAO NI WAKARIBU SANA?!" Jenifer akaanza kuwataja marafiki zake watatu ambao ndio yupo nao karibu sana na katika hao marafiki watatu aliowataja JENIFER ndio wale ambao mwalimu KABAVAKO aliwakamata wako wote na JENIFER usiku, baada ya hapo mwalimu KABAVAKO akamuuliza baba yake na JENIFER "MZEE SIKU YA IJUMAA MOSI BINTI YAKO JENIFER ALILALA NYUMBANI?!" Baba yake na JENIFER akajibu "MWALIMU MBONA SIKUELEWI TUNAULIZANA MASWALI KAMA TUPO KITUO CHA POLISI?" mwalimu KABAVAKO akamjibu "MZEE PUNGUZA JAZBA MIMI NINAKUULIZA HIVI NINA MAANA YANGU" baba yake na Jenifer ikabidi amjibu mwalimu "KILA SIKU YA IJUMAA MOSI MWANANGU HUWA ANATOKA ANAENDA KUJISOMEA NA WENZAKE USIKU KUCHA ASUBUHI ANARUDI NYUMBANI" baada ya mwalimu KABAVAKO Kumuuliza maswali JENIFER na baba yake kisha akatoka nje na kumtafuta mwanafunzi kisha akamuagiza yule mwanafunzi aende ofisi kuwaita wale wanafunzi watatu aliowakamata wakiwa Club usiku pamoja na JENIFER, yule mwanafunzi akaenda kuwaita wale rafiki zake na JENIFER walikuwa wamevaa mavazi yao ya nyumbani waliyokamatwa nayo wakaelekea mpaka ofisi ya mwalimu mkuu. Walipofika ofisini mwalimu KABAVAKO akawauliza "NYIE WANAFUNZI MNAMJUA HUYU MWANAFUNZI MWENZENU?" wakajibu "NDIO MWALIMU TUNAMJUA ANAITWA JENIFER" akawauliza tena "KWANINI NYIE MMEKUJA SHULENI MKIWA MMEVAA HIZO NGUO ZA NYUMBANI TENA FUPI?" wale wanafunzi wakajibu "MWALIMU WEWE SI ULITUKAMATA SIKU YA IJUMAA MOSI USIKU CLUB UKATUAMBIA TUJE LEO OFISINI KWAKO NA HIZI NGUO PAMOJA NA WAZAZI WETU?" mwalimu KABAVAKO akawauliza tena "NILIPO WAKAMATA HIYO SIKU YA IJUMAA MOSI MLIKUA NYIE NYIE WATATU PEKE YENU AU?" wakajibu "HAPANA MWALIMU TULIKUA PAMOJA NA JENIFER" pale pale JENIFER nguvu zikamuishia akajua tayari kishakamatwa hana jinsi akaanza kulia ofisini kwa mwalimu mkuu. Mwalimu mkuu akamwambia JENIFER "JENIFER TAFADHALI USINIFICHE NIELEZE UKWELI UKINIDANGANYA NAWEZA KUKUCHAPA HAPA MBELE YA BABA YAKO NA NITAKUFUKUZA SHULENI KWANGU, NIELEZE UKWELI SI UNAONA WENZAKO WAMENIELEZA UKWELI? HAYA NAWEWE NIELEZE UKWELI WAKO, MWALIMU KABAVAKO ALIKUKAMATA CLUB KWELI?" JENIFER akajikuta anasema ukweli "NDIO MWALIMU ALINIKAMATA JUZI IJUMAA MOSI USIKU NIKO NA HAWA MARAFIKI ZANGU CLUB" mwalimu mkuu akamuuliza tena "NA JE, NIKWELI MWALIMU KABAVAKO AMEISHAWAHI KUKUTONGOZA?" JENIFER akakosa jibu akakaa kimya, ghafla JENIFER akasema "BABA NAKUOMBA UNISAMEHE NILIKUDANGANYA MWALIMU HAJAWAH KUNITONGOZA ILA NILITAKA NIJITETEE UKWELI NIKWAMBA ALITUKAMATA CLUB USIKU" pale pale Mr. Brown nguvu zilimuishia akamwambia mwalimu KABAVAKO "MWALIMU NISAMEHE MIMI KWA YOTE HAYA, KUMBE HUYU MTOTO NI MUONGO SINA LA KUSEMA NAOMBA MUMPE ADHABU YOYOTE ILE NIKO TAYARI, MSHENZI SANA HUYU MTOTO" mwalimu mkuu akamwambia mwalimu KABAVAKO atoke nje na wale wanafunzi watatu pamoja na JENIFER akawachape fimbo kisha arudi nao ofisini kwake. Mr. Brown akabakia na mwalimu mkuu wanaongea!

JAMANI MIE UKAHABA SASA BASI" PART 2

INAENDELEA HAPA: Baada ya JENIFER na wenzake kukamatwa na mwalimu na kupewa adhabu hiyo ya kwenda na wazazi wao shuleni siku ya Ijumaa tatu na kupelekea kupoteza mudi ya kuendelea kufurah usiku huo ikawabidi waondoke kabisa sehemu hiyo ya CLUB usiku huo huo na kwenda kulala kwenye chumba cha rafiki yao CHRISTINA waliekuwa nae katika kundi lao usiku huo, ilipofika kesho yake siku ya ijumaa pili asubuhi kila mtu alirejea nyumbani kwao huku wakiwa na sura za hudhuni na mawazo kibao kichwani wakijiuliza itakuaje kesho yake ambayo ni siku ya Ijumaa tatu wanatakiwa waende shule na wazazi wao?!. Jenifer alipofika kwao moja kwa moja alielekea chumbani kwake na kujilaza kitandani huku akiwa na mawazo kibao hata chakula hakuweza kula siku hiyo muda wote alikua kajifungia chumbani analia. Ghafla akasikia mlango wa chumbani kwake unafunguliwa aliposhtuka akamuona mama yake Mrs. Brown. Mrs. Brown alimsogelea binti yake Jenifer kuanza kuzungumza nae kama ifuatavyo:-

MRS. BROWN:
"Jenifer binti yangu mbona unaonekana leo hauko sawa, nini tatizo mwanangu?! Na mbona unalia?

JENIFER:
"Hapana mama, wala usijali hamna kitu chochote naomba uwe na amani mama yangu, niko sawa tu!"

MRS. BROWN:
"Jenifer mwanangu lazima kutakuwa kuna kitu ila unaficha. Mwanangu nakuomba unieleze usinifiche niambie tu mwanangu wala usiogope"

JENIFER:
"Mama wala usijali hakuna kitu chochote kile"

MRS. BROWN:
"Sidhani binti yangu kama kweli hakuna tatizo sasa mbona unalia, Au umepata ujauzito?!

JENIFER:
"Mama bora ningekua nina ujauzito ila kwa hiki kilichonipata mama yangu najuta tena najuta hata sijui kwanini mlinipeleka shule mama yangu"

MRS. BROWN:
"Mwanangu mbona unasema hivyo kwani kuna tatizo limetokea shule?!

JENIFER:
"Ndio mama, kuna mwalimu shuleni alinitongoza nikamkatalia sasa kila siku huwa ananichapa fimbo bila makosa na ananitesa sana shule na kaniahidi kuwa atanitafutia kosa lolote la uongo ili nifukuzwe shule anikomoe na juzi siku ya Ijumaa kuna wanafunzi kawakamata usiku CLUB akawaambia kuwa atawafukuza shule sasa kaniambia namimi ataniingiza katika hilo kosa la hao wanafunzi kesho shuleni ili nifukuzwe namimi"
MRS. BROWN:
"Haiwezekani mwanangu wewe nyamaza acha kulia tumsubiri baba yako aje nimuelezee ikiwezekana kesho akupeleke shule akamkomeshe huyo mwalimu, wala usiwaze sana mwanangu Jenifer looooo, huyo mwalimu hana hata aibu"

Baada ya Jenifer kutumia uongo wa kumdanganya mama yake Mrs. Brown kwa dhumuni la kujitetea kutokana na kosa alilolifanya usiku wa jana yake walipokutwa na mwalimu wao wa shule CLUB ikamlazimu kumpa kesi ya uongo yule mwalimu kwa wazazi wake ili wasimuone yeye anamakosa. Mama yake na Jenifer Mrs. Brown alihamaki na kuingiwa na hasira akawa anamsubiria mume wake arudi ili amuelezee kilichotokea. Ghafla baba yake na Jenifer Mr. Brown akaingia nyumbani kwake na kumkuta mke wake Mrs. Brown akiwa na binti yao Jenifer, Jenifer alipomuona baba yake Mr. Brown akaanza kuangua kilio huku akisema "BABA NAJUTA MIMI MWANAOO, NAJUTA BABA HIVI KWANINI ULINIPELEKA NIKASOME ILE SHULE BABA YANGUUUUUU" Jenifer alikua analia huku akitoa sauti kubwa ya kumlalamikia baba yake. Mr. Brown alipigwa na butwaa hakujua nini kinachoendelea ikabidi akae chini na kumuuliza mke wake "MKE WANGU NINI KIMEMPATA BINTI YETU JENIFER?" Mrs. Brown akamjibu mume wake "MUME WANGU NENDA KWANZA KAKOGE KISHA ULE HALAFU NDIO NIKUELEZEE KILICHOTOKEA" Mr. Brown nae akamjibu "HAPANA MKE WANGU NIELEZEE KWANZA NIJUE TATIZO NINI?". Mrs. Brown ikabidi aanze kumuhadithia kama alivyohadithiwa na binti yao Jenifer kuwa kuna mwalimu wa shule alimtongoza binti yao akamkataa sasa huyo mwalimu anamtesa sana Jenifer shuleni na kamuahidi atamfanyia njama yoyote ili binti yao afukuzwe shuleni. Pale pale Mr. Brown nayeye akapandwa na hasira akamnyamazisha binti yake Jenifer na kumwambia "JENIFER BINTI YANGU NYAMAZA, KESHO IJUMAA TATU ASUBUHI TUTAKWENDA WOTE MPAKA SHULENI KWENU UKANIONESHE HUYO MWALIMU. ATANITAMBUA" baada ya hapo wakatawanyika Jenifer akaingia chumbani akaanza kushangilia peke yake kimya kimya akiwa na imani kuwa kishamaliza kesi aliyokuwa nayo na akawa na furaha tele akaendelea kufanya mambo yake kama kawaida.

JAMANI MIE UKAHABA SASA BASI" PART 1

 AMANI MIE UKAHABA SASA BASI ni Hadithi inayomuhusu binti wa kitanzania alietunukiwa uzuri wa asili na mvuto wa kipekee aliojaaliwa na mungu ama hakika uzuri aliokuwa nao ulikuwa ni kishawishi tosha kwa mwanaume yoyote aliemtazama binti huyu na kutamani kuwa nae kutokana na mvuto aliokuwa nao binti huyu anaitwa Jenifer na amezaliwa katika familia duni ya Mr. Brown na Mrs. Brown yenye watoto watatu (3). Ambao ni Peter, Joseph na Jenifer na katika watoto hawa watatu mwanamke alikua ni Jenifer peke yake na ndie alikua mtoto wa kwanza kuzaliwa katika familia hii yenye watoto watatu ambapo Peter na Joseph walikua ni wadogo zake na Jenifer na walikuwa bado ni wadogo sana. Na wazazi wa Jenifer Mr. Brown na Mrs. Brown walitokea kumpenda sana binti yao Jenifer kwani ndio mtoto pekee wa kike hivyo walionesha upendo mwingi kwa binti yao kwa kumtimizia mahitaj yote muhimu na kumpa kila alichokitaka binti yao ili wamridhishe na kuhakikisha wanampa malezi bora na kujenga upendo imara kwa binti yao. Kutokana na hali ya ngumu ya maisha iliyokuwepo katika familia hiyo ya Mr. Brown na Mrs. Brown, wazazi hawa walikaa na kujadili njia sahihi ya kuweza kukabiliana na umasikini walio nao na kuweza kujikwamua kimaisha wakapata wazo la kumpeleka shule binti yao Jenifer ili hapo baadae aje kuwasaidia wazazi wake kupitia elimu atakayoipata shule hivyo wazazi wakakubaliana na kuanza mipango ya kumuandikisha shule binti yao ili aanze kusoma, wazazi wa Jenifer walijitahidi kutafuta pesa kwa hali na mali ikapelekea wazazi wa Jenifer kujiunga na kampuni zinazotoa mikopo ya fedha lengo kupata pesa waweze kumtimizia mahitaji binti yao aweze kuanza shule. Mungu alileta kheri kwa wazazi hao na kufanikisha kuipata pesa ya kumpatia binti yao kwa ajili ya matumizi madogo madogo ya shule na binti yao akafanikiwa kuanza elimu ya msingi akasoma darasa la kwanza mpaka darasa la saba lakini alipo maliza darasa la saba matokeo yake hayakua mazuri hivyo hakuweza kuchaguliwa katika shule za serekali kwa ajili ya kuendelea na elimu ya sekondari lakini wazazi wa Jenifer hawakukata tamaa na waliendelea kuwa na moyo wa kumsaidia binti yao Jenifer kwa vyovyote vile mpaka waone mwisho wake kwani malengo yao binti yao asome mpaka daraja la juu afike mpaka chuo kikuu, baada ya Jenifer kumaliza elimu ya msingi na hakufanikiwa kufanya vizuri katika mitihani yake ikabidi wazazi wajipange upya kutafuta ada ya kumlipia binti yao ili aweze kujiunga na elimu ya sekondari kwa dhumuni la kuhakikisha binti yao Jenifer anaendelea na elimu. Mungu hakuitupa familia hii ya Mr na Mrs. Brown aliwajaalia wakafanikiwa kuipata pesa ya kumlipia ada binti yao na wakamuandikisha katika shule ya kulipia ya sekondari iliyofahamika kwa jina la "GARDEN SECONDARY SCHOOL" Jenifer alijiunga na shule hii na kuanza elimu yake ya sekondari lakini kama ilivyo kwa vijana wengi wa kisasa kutofahamu umuhimu wa elimu na kushindwa kujua nini wanapaswa kukifanya pindi wanapo kuwa shule ndivyo ilivyokuwa kwa Jenifer. Jenifer hakujua umuhimu wa elimu na hakuona juhudi za wazazi wake kwake za kutafuta pesa kwa ajili ya kumlipia ada ili aje kuwasaidia baadae na kuwasaidia wadogo zake Peter na Joseph. Kipindi Jenifer alipokua shuleni hapo akiendelea na elimu ya sekondari tabia yake ilibadilika akawa anautumia muda wake mwingi wa shule kujichanganya na marafiki ambao hawakuwa na msaada mzuri kwake na wakati mwingine alikua akiaga kwao anakwenda shule lakini alikua hafiki shule alikua anakwenda kwa marafiki anashinda na kurudi nyumbani wazazi wake hawakujua kinachoendelea kwa binti yao. Wakati mwingine Jenifer alikuwa ni mtu wa kupenda sana kwenda kwenye kumbi mbali mbali za starehe wakati alikua anatoka nyumbani kwao usiku akiwaaga wazazi wake kuwa anakwenda kwa marafiki zake anaosoma nao wanakwenda kukesha wakisoma na kujadiliana yale waliyofundishwa shuleni, wazazi wa Jenifer hawakuwa na kipingamizi kwa binti yao walikua ridhwaa kukubaliana na kila anachohitaji binti yao ili mradi kumridhisha na kumfanya awe huru ili mwisho wa siku aweze kutimiza ndoto za wazazi wake hivyo wazazi walikua wakimpa ruhusa binti yao atoke usiku wakidhani anaenda kusoma na wenzake kumbe Jenifer alikua anatumia muda huo kutoka na kwenda CLUB (kumbi za starehe) na marafiki zake wanaenda kujirusha na alikua anarudi nyumbani kwao kesho yake asubuhi, na ilikua kila ikifika siku ya Ijumaa mosi ndio anatoka usiku na wenzake, siku moja kama kawaida yake Jenifer na wenzake wametoka na kwenda kwenye kumbi za starehe huku nyumbani wazazi wanajua watoto wao wameenda katika masomo yao kama ilivyozoeleka, kipindi wapo CLUB kuna mwalimu wao wa shule alikuwepo katika ukumbi huo wa starehe na akakutana na kundi hili la wakina dada kama wanne akiwemo na Jenifer wakiwa wamevaa mavazi mafupi ya ajabu kama machangudoa wanaojiuza, yule mwalimu wao alichokifanya akawaita kisha akawaambia "NAOMBA SIKU YA IJUMAA TATU MKIFIKA SHULE CHA KWANZA NAOMBA NIWAKUTE OFISINI KWANGU KAMA MLIVYO WANNE TENA MJE MKIWA MMEVAA HIZI NGUO MLIZO ZIVAA NA KILA MMOJA WENU AJE NA MZAZI WAKE" kisha mwalimu akawaambia wawe huru waendelee na mambo yao ila ikifika siku ya Ijumaa tatu siku ya shule wafanye kama alivyo agiza mwalimu huyo pale pale Jenifer na wenzake wakakosa amani na mudi ya kuendelea kufurahi usiku ule ikatoweka na kila mmoja wao akawa anawaza itakuaje hiyo siku ya Ijumaa tatu na wataanzia wapi kuwaeleza wazazi wao juu ya kosa hili walilofanya mpaka wamekutana na mwalimu kawaomba waende shule na wazazi wao.....?!
ITAENDELEA USIKOSE

MBINU ZA KUDUMU NA STAA KWENYE UHUSIANO!

UMEWAHI kujiuliza; kwanini mastaa wengi hawadumu na wenzi wao? Nimeamua kuchambua mada hii kwa sababu tunao mastaa wengi kwenye jamii yetu ambao wana uhusiano ama na mastaa wenzao au watu wa kawaida.

Pia, wapo watu ambao wanatarajia kuwa na uhusiano na mastaa, wakati kuna ambao tayari wapo ndani ya penzi na watu maarufu. Pamoja na hayo yote, wengi huwa wanashindwa kudumu kwa muda mrefu na mastaa kwa sababu za hapa na pale.
Katika mada hii ambayo nimeifanyia utafiti wa muda mrefu, itakufanya mpya katika uamuzi wako, ndani ya uhusiano na staa au staa ambaye yupo katika uhusiano na mwenzi asiye staa.
Labda tuwekane sawa kidogo, hapa namzungumzia mtu maarufu katika jamii, maarufu kwa maana ya kujulikana sana. Ustaa wa mtu unaweza kusababishwa na kazi au sanaa. Mathalani, sanaa za maigizo, soka, ndondi, riadha, siasa, urembo, utangazaji, uandishi wa habari, mitindo, utunzi, uchoraji, uchongaji, biashara nk.
Siwezi kutaja moja kwa moja majina ya mastaa, lakini naamini nimeeleweka vyema kuwa nawazungumzia watu wa aina gani. Watu wanaojulikana sana katika jamii kulingana na kazi zao za kila siku.
WASIKIE MASTAA
Wakati naandaa mada hii, nilipata bahati ya kuzungumza na baadhi ya mastaa ambapo walitoa maoni yao. Kwa bahati mbaya sana, wote niliopata kuzungumza nao, walipojua mazungumzo yetu yangeishia kuwa mada gazetini waliomba kuhifadhiwa majina yao.
Hebu wasikilize: “Kiukweli kaka Shaluwa, naweza kusema sisi wanawake wenyewe ndiyo wenye matatizo...asikudanganye mtu, ustaa kazi. Ukishakuwa maarufu, unataka mambo mengi; vipodozi, gari, nguo mpya, kujirusha, simu iwe na full vocha nk.
“Sasa kama unakuwa na boy ambaye anajifanya anakuchunga sana, inakuwa ngumu kudumu na sisi tulivyo jeuri, akikuacha asubuhi, jioni kiwanja unakutana na mwingine.”
Huyu ni staa wa muziki wa dansi nchini kama alivyozungumza nami jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
“Kiukweli huwa tunaacha sana mademu, lakini siyo suala la umalaya hapo brother Shaluwa. Kuna mambo mawili makubwa; kwanza, mwanamke anakuwa anapenda ustaa wako na siyo penzi la dhati, pili anakubana na kukupangia sana ratiba...niseme kwamba, wivu unazidi!
“Unajua unapokuwa msanii, unakuwa na mambo mengi, shoo kibao kila week-end, safari za mikoani nazo hazina idadi, club ndio usiseme, sasa kwa hali hiyo, lazima uwe na mwanamke smart kwa kila kitu.
“Tuongee ukweli, hakuna mtu anayekubali kuwa na mpenzi tapeli, sisi hatuna matatizo, lakini kama umefuata jina langu au pesa, nitakushtukia soon na hapo ndipo nitakapompiga kibuti na maisha yanaendelea,” ndivyo mmoja wa kinara katika Bongo Fleva anavyosema.
Hebu sikia kauli ya msanii huyu wa filamu: “Wanawake wanapenda umaarufu wetu, kwahiyo ukiwa naye siku mbili, ukimshtukia unamtema, hapo ndipo penye tatizo bro. Mimi sihitaji mtu anayependa jina langu, nahitaji penzi la dhati.”
TATIZO NI NINI?
Kikubwa ni katika KUELEWA na kutofautisha mapenzi na ustaa. Kama umempenda, umpende kwa mapenzi ya dhati, achana na ustaa wake, lakini lazima umjue mwenzi wako na uende naye jinsi anavyotaka.
Mapenzi ya kitapeli au kufuata mali na umaarufu hayana nafasi kabisa katika maisha ya sasa, yote yanawezekana lakini kwa kukubali kujifunza na kubadilika kulingana na mwenzi wako alivyo.
UPO KWENYE UHUSIANO NA STAA?
Kama nilivyotangulia kusema awali, sina maana kwamba mastaa wote hawawezi kuishi na wenzi wao bila kuwepo kwa migogoro, ni baadhi yao! Pamoja na kuwa na migogoro hiyo ambayo mwisho wake mara nyingi imekuwa ni kuachana, hakumaanishi kwamba, mastaa hawafai kuwa na wapenzi.
Hapa nataka kuzungumza na wale ambao tayari wapo katika uhusiano na mastaa na wale ambao wanatarajia kuwa na wenzi wenye majina makubwa kwenye jamii. Hebu pitia vipengele vifuatavyo;
Usiwe na wivu sana!
Ni kweli kwamba, kati ya alama za mapenzi ya dhati ni pamoja na wivu, lakini unapokuwa na uhusiano na mwenzi staa, lazima upunguze wivu. Hii haina maana kwamba, umuache awe kicheche, awe na mapatna wengi, hapana!
Mara nyingi mastaa huwa wanaiga mambo ya Kizungu, mathalani husalimiana kwa kukumbatiana, kuandikiana sms kwa maneno ya mapenzi kama dear, sweetie, mpenzi n.k, ukikutana na mazingira kama hayo, kuwa mpole, lakini fanya uchunguzi wako taratibu bila ya yeye kujua. Penye ukweli, uongo hujitenga.
Nafasi yangu kwa leo imeishia hapa, wiki ijayo tutaendelea.

No comments:

Post a Comment